CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Chavala Ideas Platform to launch "LADIES TALENTS BATTLE" on 13rd OCt 2013 in Dar!!!




“LADIES TALENTS BATTLE” Series
IDEA CONCEPT NOTE
What is it?
This is the special project aiming to discover, nature, nourish, brand and place on market board, different talents such as singing; playing different music instruments; dancing; dramatizing; fashion and designing; story telling; poetry; comedy; moderation and all other natural talents that are lying within ladies’ natural potentials along with spreading the good news, new hopes and new motivation to themselves (Ladies at large) and the whole community concerning different sensitive issues that are termed as challenging challenges within the society of ladies and at the end to leave them with clear understanding and confidence about themselves for the Glory of Kingdom of God.

Why is it?
Because they have talents and their talents are real, why not creating the room/platform for them to manifest fully?.... Yes! no more hiding, no more trying, it the time to it for real! Personally I believe that giving them a unique and zoomed platform for them to show what they have, it will encourage many of them who are still hesitating to start doing something; it will enforce those who are doing to be more serious and it will give the society a special eye (consideration) to them.

Why now?
It has to be done now because the right time is always now and the vision has come very clearly for now generation. In the other side there are several groups of NGOs, world religions and the so called Gender activists are very busy feeding our ladies with negative information, negative beliefs and negative perspectives about them and that may yield the society of lesbians and women who has completely negative perceptions toward their husbands if they got married, and so we ought and we must do something for the sake of our future. One Wiseman said “The triumph of evil grows when good people are doing nothing”

How will it be?
All of our activities in this project will be done in a form of a special campaign by which there will be special Concerts and tours in different places such as churches, schools and higher learning institutions. Furthermore there will be a special TV program/show that will comprise different issues including feedbacks of concerts and tours from different fields, hope that will help millions of ladies to be informed all over the country. There will also be a magazine and small bulletins with different information that can help them read slowly and understand.


Where to be done?
It is to be done in Tanzania and we have choose to start in the largest city of Dar es salaam; all activities and tasks will be done in Tanzania and all requirements we need will be found in Tanzania, Local media to be used and the magazine and bulletins will emanate from Tanzania.

Objectives;
There are vast of objectives but here are major of them;
v  To discover, nature, equip, coach, exercise, brand and market all the natural talents that are lying within ladies potentials
v  To zoom and place different ladies with different potentials on top where everybody can see, and thus whoever will be in need of such potentials will easily sight out.
v  To equip them with truth, moral and our country’s civilization as they grow and understand more about themselves and their roles in their society.
v  Life coaching; Carrier guidance and individual capacity building
v  To nature and produce true patriot of African natural beauty, who are futuristic and have bet to remain pure until when they got legal permit (Marriage)
v  To prepare brave leaders who can stand for what they know and believe is true and legitimate, ladies who can utilize the ample of their potentials to educate themselves and others in the society and the whole society at large.

Expectations;
To see ladies who are proud to be who they are, proud of their talents and other potentials that they have, ladies who can’t abase themselves and can’t compromise to ungodly matters; ladies who can’t trade their humility such as offering sex in order to get what they deserved to get by just who they are such as Jobs that they are qualifying to, pass mark in schools and access to different leadership posts. To see ladies who are proud of their natural African beauty, patriot of their culture, ladies who have pledged to remain pure and the one who have aimed to be good women and best wives in future; To see ladies who will say NO! to western cultures and abase whites’ civilization which abuses our civilization, ladies who will work hard than harder and not ladies who will wait to receive from men because that might be very lazy society.

Participants;
Everybody in our society has to be part of this project for the results of it will benefit the whole society….let the church be ahead in praying for them and wishing good for them to succeed……let ladies with different talents and potentials be ahead on stage and others be down watching and learning from them and from what they are doing…let others support the project in all spheres such as financially, morally, intellectually and psychologically….let the parents encourage their children especially their daughters to work hard on their talents and to have sense of future with whatever they are doing….let the government support them by any means possible and practical……let the media be ahead on promoting such talents and airing the contents of presentations and the society as the whole will be participating by altering positively what they have learned!

Author’s note
This is the vision that has come to me very clearly that we have to do something to support this natural potentials which most of them are living unutilized and are buried unleashed. It is true that there are different few platforms where gifts and talents are being natured and traded but that is not enough compared to reality, it is the fact that female mankind is bigger that male mankind but in manifestation of different potentials female mankind are not clearly seen while they are the one who shape the future of any society for what they feed their babies;
 Sex business, drug abuse, moral deterioration, early pregnancies and artificial beautification is the result of Identity crisis among our people including this group (ladies) now we can’t just stay idle complaining but we have to do something about it, I believe if female mankind will be empowered, motivated, natured and well informed then the whole society will be strong and futuristic. It is my desire to see different gifts and talents by Tanzanian ladies excelling and shinning out to the world, promoting our country, our culture and our God!
Personally I have strong trust over ladies and women for my mother has proven it into my life, I have seen the need (other call it a challenge), I have sited out a solution and I am ready to invest my intelligent, my creativity, my time and my finance over this matter just to see a better futuristic society that will cater, maintain and keep our true values in generations to come for the sake of the Glory of God in Tanzania.
It might be very minute to the world but I am sure it will mean a lot to someone who will be the beneficiary of this project, I won’t stay idle complaining to issues that I am capable of doing something, so no matter what I will do something anyway and THIS IS IT…my purpose is my destiny, I am a solution to whatever challenge that counterfeit with my natural potential, YES! I live for mankind!

Conclusion;
Hope the idea is clearly understood and you are already challenged and you are thinking to do something, Yes! This is the right time and you must do something that is lying within your capacity. Whatever opinions, advise and contributions that you think can be of great importance to this project, please you are welcome and above all you are very invited to be part of this new movement.




Idea & Concept note by
Chavala Ideas Platform
Fredy E. Chavala <King Chavala-MC>
+255 713 883 797

SOUL BREAKFAST MEETING NOW IS FOCUSING TO LOCKED POTENTIALS!!!

Here is the special moment for youth and young proffessionals especially students from secondary schools to higher learning institutions, every last saturday of the month there are these gatherings at VCC Victoria for free plus free breakfast, and this coming one we will be looking on howa someone can UNLOCK HIS/HER POTENTIAL in a wider perspective!
Come and learn from live testimonies from A businessman Daniel Mikenze who started very low and now is among big employer of his agement and the Founder and King of Stand up Comedy,Fredy Chavala who is still growing with a great foundation.
Come one come all, we will have Music artists like Sarah Shilla, Bomby Johnson and Rivers of Joy Juniors, i am sure your mind will be shaked on 31st August 2013, you need not to miss this!!
YOU ARE ALL WELCOME!!!

@Sponsored by Chavala Ideas Platform
+255 713 883 797

Papaa On Tuesday....Kuku anayetaga Huwa Hachinjwi!!!!


Kwenye kiswahili kuna methali, nahau na Misemo ambayo huwa inatupa tafakari ya kina kuhusu maisha. Na hii misemo yote ni kwa ajili ya kutufunza kile wahenga wanachodhani ni busara kwenye kizazi chao, Chetu na kinachokuja kujifunza kutoka kwao katika yale waliyoyapitia. Kwenye mila za Kiafrika kuku huliwa wakati wa sikukuu ama anapokuwa anakuja mgeni. Ukiacha siku hizi kwenye huu ujio wa Kuku wa Kizungu enzi hizo wakati Nahau zinatungwa kulikuwa hakuna wazo kama kuna Kuku aina nyingine watakuwepo duniani kila nyumba ilikuwa na utamaduni wa kufuga kuku hasa kwenye jamii za wafugaji, inapotokea kuna ugeni katika nyumba fulani basi ndio wakati muafaka sana wa kuku kuchinjwa. Katika banda kulikuwa kuna jogoo na wale wanaotaga kwa ajili ya kutotoa kuongeza uzao. Kuku wanaotaga walikuwa wanahifadhiwa kwa ajili ya manufaa ya baadae ndipo wahenga wakasema "Kuku anayetaga huwa hachinjwi".


Kuna mambo kadha wa kadha ya kujifunza kupitia kuku wa kutaga na suala zima la kuchinja kuku. Kuchinja ni kuondoa uhai wa kuku na kupoteza faida ambazo mfugaji angeendelea kuzipata iwapo angeendelea kufuga yule kuku. Tunachangamoto kubwa sana ya kujua kwenye maisha yetu nini ni kuku anayetaga na lini pia achinjwe. Wengi tumekuwa tukichinja kuku anayetaga na kupoteza kabisa dira za kwenye maisha. Fursa ambazo huwa zinakuja kwenye maisha yetu ni nadra sana kuzirudia kwa sababu mbalimbali tumekuwa tukizipoteza ama kuziharibu kwa kutokujua kuwa yamkini fursa hizo zingetusaidia kwa mambo mengine kwenye maisha.


Mara kadhaa nimeongea kwenye hadhara ambazo nimekuwa na fursa ya kuzungumza kuhusu Kizazi tulichonacho kisivyoweza kuziona na kuzithamini fursa tulizonazo. Wengi wetu ni ngumu kuzikabiri changamoto tunazokutana nazo kwenye maisha iwe ajira, iwe mahusiano, iwe kitaaluma iwe chochote kile kizazi hiki tumejifunza kuchukua maamuzi ya hasira kuliko busara, wengi tunaamini tunaweza ishi bila yeyote,na tunaweza fanya chochote pasipo msaada wa yeyote mwisho wa siku tunakwama kwenye mambo mengi kwa sababu tulidhani sisi ndio kila kitu. Ndio maana leo mtu akiwa na hasira anaweza ukashangaa alikuwa anafanya kazi kutokana na namna moja ama nyingine anakasirishwa na mazingira ya kazi anaamua kuongea yote, anafunguka kupita maelezo utamsikia "kazi itakuwa hii bana, kazi zipo za maana, kaofisi gani haka" anaongea mwisho wa siku anaamua kuacha anarudi nyumbani hasira zikiisha anagundua kuwa alitukana Wakunga wakati uzazi ungalipo alimchinja kuku anayetaga tena kwa kisu butu.

Maamuzi ambayo tunayafanya kwenye maisha hutugharimu iwapo hatutajua matokeo ya maamuzi hayo maana tunao uwezo wa kuchagua nini cha kufanya hila hatuna uwezo wa kuamua namna ya matokeo iwapo tu matokeo yanajulikana na unapaswa ukubaliane nayo. Unao uwezo wa kuchinja kuku anayetaga ama asiyetaga. Asilimia kubwa ya watanzania tunaishi katika nyumba za kupanga unaishije na majirani zako, unaishije na watu wanaokuzunguka. Mkorofi hana dini wala kabila dini yake na kabila lake ni Ukorofi. Ukiona majirani hawakushirikishi katika mambo yao mengi ujiulize unaishije na walimwengu. Ukitaka kujua kipimo kidogo cha wewe unavyoishi na walimwengu subiri ikifika jambo lako uone walimwengu watalipokeaje na kulichangamkia kiasi gani. Kama wewe kila msiba uko busy ama kila mambo ya wenzio uko busy basi subiri ya kwako yakifika na ukagundua unawahitaji watu wawe na wewe. Biblia inasema unavyotaka watu wakufanyie wafanyie wewe kwanza. Jirani na nilipokuwa nikiishi Block 41 enzi hizo kulikuwa na mdada ambaye alikuwa na gari yake full tinted, anaweza akapita kijiweni wala asisalimie ingawa salamu haipotezi chochote, anaweza akakukuta barazani atataka wewe ndiwe umuanze alikuwa anajua hawahitaji wale watu wa mtaa ule yeye level nyingine siku ya siku gari lake likaingia kwenye mtaro, dada wa watu akashindwa kushuka kwenye gari akahangaika mwisho akashuka watu wamekaa kwenye vibaraza vyao wanamtazama, akaenda kuomba vijana wa kijiweni wamsaidie wakamuuliza "hivi leo ndo unajua sisi ni watu"??pamoja na kutangaza angetoa fedha watu wakamkatalia, akadhani atashinda vita ya wema kwa nyodo akachukua simu akampigia boyfriend wake aje nae alipofika hakuwa na msaada ikabidi apige kaka wa watu aombe radhi kwa niaba ya mpenzi wake ili kupata msaada wa kusukuma gari lile, ajabu wale vijana wakasukuma gari na wakakataa kuchukua hela, tangu siku ile maisha ya mdada yalibadirika salamu mbele kama skafu ya Chama Cha Maskauti.

Kwanini tufanya maamuzi ambayo hata kama yatatugharimu baadae lakini tuchague kwa busara. Kwanini kuvunja simu ya mumeo au mpenzio kwa sababu eti umekuta sms usizozielewa. Kwani tatizo ni simu ama ni mtu wengi tunapambana na matokeo ya tabia tukidhani tunadhibiti chanzo cha tabia. Juzi kati nimesikia kuna mtu amechoma gari la mumewe baada ya kukuta kwenye gari la mumewe kuna Condom. Sasa ukichoma gari ndio unakuwa umemaliza tatizo la usaliti??Usiharibu leo wakati unajua kesho utahitaji ama utawahitaji hao watu ama mtu. Kizazi chetu ni kizazi cha Maamuzi ya hasira wapenzi wakikosana solution ya kwanza ni Kuchuniana, baada ya masaa 600 ndio wanakuja kuanza kuongelea mgogoro wao wa mapenzi. Kiwango cha kukabiriana na changamoto kinadhoofishwa na maamuzi wa haraka haraka tunayoyachukua huku tukiwa bado tunauhitaji wa kile ambacho tunataka kukipoteza leo. Tumechinja kuku anayetaga wa kazi zetu, tumechinja mahusiano yetu, tumechinja biashara zetu wenyewe wakati bado tunavihitaji.


Idadi ya watu wanaoweza kuamini inazidi kupungua, kila mtu anajihami na mwenzake kisaikolojia ama kivitendo kabisa, kwenye ajira mabosi wa kikaburu na wafanyakazi wa kibongo full stress, wanandoa wanawake walishaamini hakuna mwanaume ambaye ha-chit wote wanachit sema hatujui tu, wanachit kwa sms, wanachit kingono, wanachit ki fedha, marafiki wanaoaminiana wako wachache wengi wetu wanaishi bila na kuwa best friend, wengi wanaishi maisha ya wenyewe wenyewe wakidhani wakikaa wenyewe ndio watakuwa salama zaidi. Nani anamwamini nani kiasi cha kwamba akafunguka asilimia 500 hata wachungaji hawaaminiwi itakuwa waumini. Ukimkopesha mtu fedha leo unaweka na asilimia za kuamini kuwa utazungushwa kuipata hela yako. Kuna wengine kwa ajili ya kukopa kopa wanashindwa kabisa kuaminiwa hata kama wanashida kubwa na ya ukweli. Kuna siku walichinja kuku wa kutaga matokeo yake hana tena msaada kutoka kaw watu. Ukifika saa ya wewe kukopa basi kila mtu atatoa sababu utasikia "yaani sasa hivi hapa nimelipa ada".

Kila maamuzi unayoyachukua leo yatakugharimu either kwa heri ama kwa shari. Ukiamua kuchinja kuku wa kutaga basi jua unapoteza kuku na mayai, na vifaranga. Busara katika kuamua ndio msingi wa maendeleo. Inawezekana leo ukaamua jambo ambalo wengi wasijue maana yake. Inawezekana una kuku mmoja ndo huyo huyo ambaye anataga hata angekuja mgeni gani huwezi mchinja huyo kuku sababu una hakika kabisa nikimuacha leo baada ya siku chache nitakuja kuwa na kuku wengi. Maamuzi ya kutokuchinja ni maamuzi yako na sio maamuzi mepesi lakini maamuzi ya kutokufanya sasa yana faida zaidi kuliko ukaamua kuchinja leo. Kuna mambo mengi sana kwa sababu ya marafiki, sababu za tamaa zetu, sababu za Kutafuta sifa kwenye maisha tumejikuta tumechinja Kuku anayetaga na kusahau kuwa yamkini huyu kuku angetufaa baadae. Majuto ni Mjukuu wa Baba anayeitwa maamuzi na mama anayeitwa wakati sahihi. Ukiamua jambo sahihi wakati sahihi unaitwa una hekima kama sio busara, ukikosea hapo utakutana na majuto mtaa wa mbele.

Kukua wa Kutaga Huwa Hachinjwi.
Ze Blogger

0798020110.

Papaa On Tuesday Kwa Hisani Ya Friends On Friday.

NI MARUFUKU....KUVAA NGUO KIPUMBAVU!!!!

#....NI MARUFUKU!#
*Kwa kijana yeyote wa kiume kuvaa suruali chini ya makalio eti kata kei ama mlegezo....maana hiyo ilianzishwa na wafungwa wa marekani na ilikuwa dalili ya kiburi na Afrika kusini walikuwa wanavaa hivyo wafanyakazi wa Boers ili kurahisisha zoezi la kupigwa mihuri hapa juu ya matako baada ya kazi,na kwa sasa wanaume wasio riziki wa mashariki ya kati na ulaya wanavaa ili kuwavutia wateja wao kabla hawajaolewa....sasa wewe unavaa sasa hivi unamaanisha nini? Tena wengine unakuta boxer chafu kama nini....ukimuona kijana wa namna hiyo hata awe nani ama maarufu kiasi gani,ujue HAJITAMBUI!


 
 *Kwa kijana yeyote wa kike kuvaa nguo za kulalia,nguo za ndani ama nguo zinazomdharilisha yeye na wasichana wengine wote....yaani mtu anatembea mjini na skintight tu,mwingine anatembea ameyaacha maziwa nje,tena makusudi...acheni ujinga ninyi,kama nguo ni ya ndani vaa ndani,thamani yako haiongezeki kwa kujichoresha na kuacha maziwa nje,kila mmoja anajua kilichopo ndani so kifiche tu,by the way chenye thamani hufichwa.....hizo ni tabia za makahaba na night stripers sasa wewe unayevaa hivyo una malengo gani? Wengine maumbo mabaya na wengine miili imejaa makovu,jamani ficha tu.

 
 Sasa haijalishi ni nani wala nani,nimesema marufuku! Kama una akili timamu utazingatia hili lakini kama wewe ni mpumbavu basi unaweza kuendelea na nakuhakikishia usipobadilika mwisho wako utakuwa wa majuto...na kama utakuwa na watoto basi ndio utakuwa umeshawaharibu hata kabla hawajazaliwa!
SALAM HIZI NAZILETA BAADA YA MFUNGO KUISHA MAANA NAJUA KUNA WENGINE NDIO KAMA VILE WALIKUWA KIFUNGONI KUFANYA MEMA SASA WAMEACHILIWA KURUDI KULEKULE!
Na hata kanisani tusikuone na huo ujinga wako unless kama wewe ni agent na umetumwa kuharibu kanisa,potelea mbali ukinikasirikia lakini najua jambo moja tu.....MAMBO YOTE YATAPITA LAKINI NENO LA MUNGU HALITAPITA KAMWE!!


Na King Chavala MC
+255 713 883 797

Ujumbe huu unakujia kwa Udhamini mkubwa wa; 
http://chavalamedia.blogspot.com
(c)2013

MSAADA WA DHARULA WA CHAKULA UNAHITAJIKA KWA WOTOTO YATIMA WA HOCET!!!!

 
SHALOM!
HABARI ZENU WAPENDWA!!
NINAAMINI MNA MOYO WA UPENDO, TENA WA KUWAJALI WENGINE KULIKO NINYI, NA HATA ZAIDI BIBLIA INASEMA UPENDO WA KWELI NI ULE WA KUWAPENDA WENGINE ZAIDI.
*****HANANASIFU ORPHANAGE CENTRE (HOCET)....HAWANA CHAKULA KABISAAAAA NA WEWE NA MIMI PEKEE NDIO TUNAWEZA KUWALISHA KWA SIKU 120, KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA****
LEO NINALO OMBI MAALUM KWENU, NI MUHIMU SANA SANA....KUNA KITUO KIMOJA CHA KULELEA WATOTO YATIMA (WATOTO WA MUNGU), KITUO KINACHOENDESHWA NA WATU TU WALIOJITOLEA, NA HAPO AWALI KILIKUWAQ KINAFADHILIWA NA WAZUNGU FULANI, LAKINI BAADA YA KUONA WATOTO HAO WAMEKAZANA NA MUNGU NA HAO WAZUNGU (WAFADHILI) WAKAWEKA MASHARTI, ETI KAMA WAKITAKA WAENDELEE KUPOKEA MISAADA YAO BASI WAACHANE NA HAYO MAMBO YA YESU YESU....NA KWA KUWA HAKUNA BABA MWINGINE ZAIDI YA MBINGUNI NA HAKUNA  NAMNA BINADAMU ANAWEZA KUISHI KWA MISAADA YA BINADAMU MWINGINE BAADA YA KUMKANA MUNGU WA KWELI.
 
SASA WATOTO HAO WAKO KWENYE ENEO LAO LA SHULE WANASOMA NA WANAYO MIRADI AMBAYO BADO HAIJAANZA KULETA FAIDA ILI WAWEZE KUJIENDESHA WENYEWE, NAHIYO ITAKUWA HIVYO TU BAADA YA MIEZI MITATU AU MINNE KUANZAIA SASA.
WATOTO HAWA KWA SASA HAWANA CHAKULA KABISA, NA HATA LEO WAMEKULA KWA MSAADA WA KIJANA MMOJA ALIJITOLEA YEYE BINAFSI NA FAMILIA YAKE....MBALI NA GHARAMA NYINGINE ZA UENDESHAJI KAMA MISHAHARA/POSHO ZA WALIMU;
************************************************************************************************
KITUO HIKI KINATUMIA UNGA KILO 30, MAHARAGE KILO 14 NA SUKARI KILO 5....NA IKIWA NI WALI,BASI HUHITAJIKA KILO 30 ZA MCHELE KWA MLO MMOJA....NA PIA UNAWEZA KUCHANGIA MAFUTA NA FEDHA KWA AJILI YA VITU VINGINE VINAVYOWEZA KUHITAJIKA.
************************************************************************************************

NINAAMINI KWA MSAADA WA WATANZANIA WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA WATOTO WA KITANZANIA, WATOTO HAWA HAWATAKOSA CHAKULA KWA SIKU HIZI 120 ZA MPITO KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA WENYEWE, SIO LAZIMA ULETE MSAADA MKUBWA SANA, LAKINI NAAMINI UNAWEZA UKAJITOLEA CHAKULA KIASI JAPO KWA SIKU MOJA TU KAMA SIO TATU, YAWEZA KUWA WEWE BINAFSI AU KAMPUNI AU FAMILIA AU KANISA, LAKINI NINACHOKIAMINI NI KUWA KAMA KWELI TUNAAMINISHA KUMPENDA MUNGU NA KUWAPENDA WATOTO WATANZANIA TENA WANAOLELEWA KATIKA MALEZI YA KIMUNGU BASI LAZIMA WATOTO HAWA WATAISHI BILA HOFU YA CHAKULA KWA SIMU HIZI 120, NA KWA HAKIKA BWANA ATAKUBARIKI SAWASAWA NA IMANI YAKO KWAKE
YAK 1:27 "....DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGUBABA NI HII, KUWATAZAMA WAJANE NA YATIMA KATIKA DHIKI YAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO NA MAWAA"
 
MSAADA HUO UNAHITAJIKA SANA SANA, NAAM KWA NAMNA YOYOTE ILE UNAYOWEZA KUCHANGIA BASI USISITE,FANYA HIVYO...SADAKA YAKO YA KUWALISHA WATOTO HAWA HAITASAHAULIKA HATA KIDOGO, UNAWEZA KULETA MCHANGO WAKO WA CHAKULA PALE OFISI ZA NIIM COMPUTERS, MOROCO HOTEL AU UKATUMA MCHANGO WAKO WA FEDHA KWA NJIA YA SIMU, NAAM KWA MAULIZO ZAIDI 
TAFADHALI WASILIANA NA WASIMAMIZI NA WARATIBU WA ZOEZI HILI KWA NO.
0713 26 1425 na 0754 527955, pia 0783 757051
KWA NIABA YA WASIMAMIZI WA KITUO HIKI NINAWASHUKURU HATA KABLA HAMJAFANYA JAMBO LOLOTE MAANA NAAMINI UMEGUSWA NA UKO TAYARI SASA KUWASAIDIA WATOTO HAWA...KAMA TUNAWEZA KUCHANGIA SHEREHE ZA HARUSI, NAFIKIRI HATMA YA WATOTO HAWA NI ZAIDI,MUNGU AKUBARIKI UNAPOMSHIRIKISHA NA MWENZAKO!!
 
Imeandikwa na
KING CHAVALA MC
KWA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.

Friends On Friday Twende Kazi



Friends On Friday Event Number Moko ya Vijana wa madhehebu yote ilifanyika Ijumaa ya Wiki Iliyopita na safari Hii Friends On Friday Inakujua tarehe 6 Sept, 2013 ikiwa na Jina "FOF Maridadi"

Blogger Ambwene Mwamwaja Afafanua Gospel Kitaa Blog Inavyokusanya Habari



Mtangazaji wa WAPO Radio na Mmiliki wa Blog Ya Gospel Kitaa, amefunguka na kueleza kuwa ana network Kubwa ya watu wanaompa habari karibu nchi nzima na Kuweza kuziratibu akiwa Nchini Uingereza. Blogger huyo maarufu Ambwene Michael Mwamwaja alieleza kuwa mbali na kupata taarifa hizo pia huzifanyia uthibitisho wa habari kabla hajazituma katika Blog.

Blogger huyo maarufu ambaye kwa sasa anaishi Nchini Uingereza yuko nchini kwa mapumziko mafupi ambapo alieleza kwa kina namna ambavyos aliweza iwakilisha Tanzania katika Tuzo za Africa Gospel Music Awards ambapo Mwanamuziki wa Injili Kutoka Tanzania Christina Shusho aliwakilisha Vema nchi ya Tanzania.

Mwamwaja ni Mmiliki wa blog ya www.gospelkitaa.blogspot.com aliyasema hayo alipokuwa akihojiwa na Kipindi nambari one cha Gospel Tanzania "Chomoza".


KUNA VITA NDIO, LAKINI PIA KUNA SHEREHE JESHINI....HONGERA LUTENI FRANK MNDEME!!!

Habari zenu!
Kwa namna ya kipekee, natamani uone ni jinsi gani Shughuli ya Kuoa inavyoheshimiwa hata na Jeshi....wanaamini mwanajeshi pia anahitaji msaidizi na mwenza, na ndio maana ukianza mafunzo ya jeshi,ama kujiunga na jeshi na kuwa mwanajeshi....unatakiwa kulitumikia jeshi ukiwa single kwa miaka 6 (Sijui kama katazo hili lina nguvu hata sasa) na ndio unaruhusiwa kuoa kiheshima!!

Luteni Frank Mndeme na mkewe
Unaweza kuona jinsi heshima ilivyo...
Yaani hii ni Official Hongera!

HUU NI MFANO WA HARUSI ZA KIJESHI, NIMEPATA PICHA CHACHE ZA NAMNA ILIVYOKUWA WAKATI LUTENI FRANK MNDEME ALIPOOA  SIKU CHACHE ZILIZOPITA!!

Huyu ni mdogo wa Mathew Mndeme, mmoja wa waandishi wa Blog hii....Simple Man with always a story to tell!

CHAVALA IDEAS PLATFORM Inawatakia kila lakheri na fanaka ya maisha mema wanandoa hawa...furaha ya ndoa na upendo wa kweli udumu na kukua kila leo,Amen!

Hotline; +255 713 883 797

Papaa On Tuesday.....Kwanini Hatujifunzi Kutokana na Makosa?


Wakati Wamarekani na watu wengine mwaka 2011 walisheherekea kuuwawa kwa Osama Bin Laden, ni vema tukakumbuka kujifunza kutokana na makosa hasa tukajifunza kutoka kwenye makosa tunayofanya wenyewe. Kuna msemo unaotumika kuwa “Experience is a good teacher” lakini ninahisi bado Experience hajawa mwalimu mzuri kwenye maisha ya watu wengi sana. Hujawahi kuona swali liliwahi toka mwaka Fulani na watu wakapeana ‘Past Papers” na swali lile lile mtu akakosa?ama swali hilo hilo mtu amelifanya kwenye assignment amekosa na baadae akaelewa wapi alikosea lakini baadae akakosa tena, au mtu anaingia kufanya biashara moja na katika kufanya anagundua kuna kitu alikuwa anakosea akapata hasara akianza biashara ya pili anarudia makosa yale yale. Au hujawahi ona mtu anacheza upatu kama ule wa siku zileeee “Faida Investment” ana akapata hasara kutokana na hasara akajiapiza hatacheza tena upatu, ajabu ilipokuja “DECI” akarudia makosa yale yale na ikala kwake, kuna mwingine amewahi kuwa na relationship zaidi ya 2 lakini makosa aliyokuwa anafanya awali ndo hayo hayo yanamtesa mpaka leo, umewahi jiuliza kwanini?Hujawao ona kuna mtu ameumizwa moyo zaidi ya mara 800 na kila siku anaapa, mie siwezi mpa mtu moyo wangu, anaongea utadhani amejifunza baada ya miezi 6 yale yale yaliyotokea kwenye uhusiano uliopota ndo hayo hayo yanatokea hata sasa.
Kuna mwingine anasahau mpaka unahisi “anaugonjwa wa kusahau” wakati mwingine kusahau kwake kumemsababishia kuingia katika gharama za ziada ambazo pengine hawakuwa amepanga kuingia, wengine kutoka na kusahau wamepoteza trust hata kwa waajiri wao makosa yale yale waliyokuwa wakifanya awali ndiyo wanayorudia. Unakuta mwezi huu umeelekezwa labda kazi hii inafanyika hivi ajabu kosa la mwezi uliopita unalirudia vile vile wengi wetu tunadhani kujisikia vibaya ni dalili ya kubadilika. Utasikia mtu anasema "ninajisikia vibaya sana kukosea", Kujisikia vibaya haitoshi ila kujifunza katika yale tunayoyakosea katika maisha.

Unakuta makosa ya matumizi mabaya ya Mshahara wako yanajirudia kila mwezi hakuna siku ambayo mshahara ukakutana, mshahara wa mwezi huu haujawahi kusalimiana na mashahara wa mwezi ujao wanapishana siku wiki nzima, makosa hayo yamekupelekea kwenye madeni ya kila mwezi unajikuta wewe ukishika mshahara huna chako umewashikia wengine hela zao unabaki kujisikia vibaya kujisikia vibaya hakukusaidii mwezi ujao usirudie makosa, kujifunza katika tatizo na kuamua kubadilika ndiko kutakusababisha kubadilika kutoka katika hali uliyonayo.
Kuna watu wamewahi jichukia nafsi zao na tabia zao, na kuna wengine waliwahi jiapiza kuwa hawata rudia tena lakini ndo utadhani wamejiapiza kufanya zaidi ya alivyokuwa anafanya mwanzo. Kujifunza ni mfumo wa kila siku lakini kujifunza kutokana na Makosa hata Serikali yetu imekuwa ni tatizo. Makosa yale yale yanayotokea kwenye Serikali na kupelekea upotevu wa fedha nyingi za Serikali, ndio huo huo pia utatokea mwakani na mwakakeshokutwa pia. Makosa yale yale yanayoitesa CCM ndiyo makosa hay ohayo yatatesa NCCR-Mageuzi ndo hay ohayo yataitesa CHADEMA na ndo hay ohayo yataitesa TLP. Sababu zile zile za kufeli kwa wadogo zetu kwenye shule za Sekondari mwaka huu ndo hizo hizo pia zitasababisha mwakani watu wafeli. Makosa yale yale tuliyofanya kwenye Uchaguzi wa mwaka 2010 ndo yale yale 2015 kwani kuna jipya??


Changamoto kubwa sana ambayo inainyemelea Tanzania yetu ni watu kupenda kuambiwa, yaani akiwa anaumwa yeye mwenyewe hawezi kujitesa kunywa maji, ila Daktari akimwambia asipokunywa maji atakufa basi atakunywa maji mpaka atawaboa, wengi wanaenda Gym siku hizi si kwa sababu wanapenda mazoezi aaah wanaenda “kujikinga na magonjwa” wakisha pungua unene wanarudia yale yale. Kama hauna “mood” ya mazoezi yatakushinda utafanya siku mbili tatu unaacha why?hatujifunzi kupitia makosa yetu.


Kila mtu anapaswa kujifunza kutokana na makosa, usiogope kukosea sababu ni sehemu ya kujifunza ukiogopa kukosea hautakuja kuweza ila ukikosea unajua kwanini ulikosea na nini au wapi urekebishe. Kabla ya kujua kuendesha baiskeli wengi walidondoka, kabla ya kuweza kuendesha gari wengi waligonga kwenye Reverse ila walipogonga ndivyo walivyozidi kujifunza. Kujifunza ni gharama,gharama ya kujifunza ni ndogo ukilinganisha na gharama ya kurudia kosa lile lile, kuna mambo ambayo pengine yana gharimu maisha yako kwa sasa kwa sababu tu kukosea kuchagua kitu Fulani, pengine gari ulilonunua linakugharimu sababu tu ya kukosea kuchagua, wengine wenzi wao wa maisha, wengine ni taaluma zao kila mtu ana “makovu yasiyokuwa na hisia” ambayo yanatesa watu wengi.

Zahma ambayo mtu ameipata kutafuta nyumba ya kupanga na kujikusanyia kodi ya nyumba ndo makosa hay ohayo yatatokea katika kutafuta nyumba na kukusanya kodi, kwanini?sababu hatuna utamaduni wa kujifunza kutokana na makosa. Makosa yale yale waliyofanya wazazi wetu katika umri wao wa kufanya maamuzi mazito ndiyo hayo hayo pia yatatokea na kwetu na kwenye vizazi vyetu. Usipojijengea utamaduni wa kujifunza hakuna wa kukufunza kwa kizazi chetu. Kwani wewe unafunzwa na nani makosa yale ambayo wewe uliyafanya ukaharibikiwa mapema si ajabu watoto wako pia yakawatokea kwa mwamvuli wa "uzungu" watoto wako katika umri wako ule wa kujua mema na mabaya watadondokea katika shimo lile lile. Tarehe ya mtoto kuzaliwa iko mbele kuliko anniversary ya Harusi yenu.
Uamuzi wa kujifunza ni wako usisubiri mtu wa kuja kukufunza, hata wanaokufunza walijifunza kwa kukosea, na kama unaweza kujifunza kabla ya kukosea kwanini usubiri kukosea ndo ujifunze?jifunze kupitia makosa yaw engine, walipokanyaga wao na kukosea wewe usikanyage.Usipochafuka utajifunzaje?

Kuna watu huwa wanasema usijifunze kwa walioshindwa maana na wewe utashindwa, kuna mtu aliwahi sema if you have never done any mistake,you have never tried something new. Kwanini uogope kujifunza kwa walioshindwa, kujifunza kwao kwenye mapungufu yao inasababisha mwerevu kujua njia gani aspite, kujifunza kwa waliofanikiwa peke yake ni mfumo ambao tumetengenezewa ili kutujengea ujasiri wa kuogopa. ndio maana kwenye interviews hata za ndoa utakuta wanaitwa watu ambao wamefanikiwa wanaonesha namna ambavyo wamefanikiwa mbona hatujawahi waita watu ambao wamechemsha tukawahoji kwanini walichemsha?kisa na mkasa eti hatuna jipya la kujifunza kwa walioshindwa ni kweli hatuna la kujifunza, katika kushindwa kwako mambo mengi ni kweli huwezi mfunza mtu?labda kama hatujajua makosa yetu ni yepi ndio maana hatuwezi wafunza wengine kile tulichokosea. Wote tunapenda story ya Petro aliyemkana Yesu mara tatu kisha akatengeneza, lakini hakuna mtu anayejifunza kwa Yuda aliyemkana Yesu kisha akajitundika kitanzi.


…//Papaa
0713 494110



UNAFIKI ULIOJIFICHA NYUMA NA MANENO YA MARAFIKI... "TUKO PAMOJA SANA"!!!





SALAM KWA WOTE!
Na amini watu wote tuko vizuri na bado tunakazana kuzifikia ndoto za maisha yetu!
Leo nimesukumwa kuzungumzia jambo moja hapa ambalo naona likiachwa hivyo litakuwa tatizo,tena tatizo kubwa.

UTANGULIZI;
Katika haya maisha hakuna mtu anaweza kuishi peke yake, sio tu kwa maana ya mwenza wa maisha ila namaanisha bila mtu mwingine yeyete, maana huwezi kuwa kila kitu na huwezi kufanya kila kitu mwenyewe kihusuyo maisha yako...una ndoto yako ya kumiliki Chuo kikuu ni sawa, lakini kuliweka hilo wazo kwenye maandishi ya kusomeka unahitaji watalaamu wa kuandika, kabla hujaanza kufanya lolote, unatakiwa upate mwongozo kwa wale waliotangulia na hapo unahitaji watu wengine.....kwa ufupi kila hatua utakayopiga utawahitaji watu,aitha kwa kuwaomba au kuwaajiri kwa maana ya kuwapa kazi na kuwalipa. hata ukitaka tu kutoka kwenda mjini lazima uhitaji dereva na konda na hata kama una gari binafsi kuna saa utamuhitaji muuzaji wa mafuta....KIMSINGI "KUISHI" NI KURAHISISHIANA MAJUKUMU KWA KILA MMOJA WETU KWA FAIDA YA KILA MMOJA WETU!.
Kwa msingi huo nataka utambue kuwa UNAHITAJIKA KUWASAIDIA WENGINE kama vile ambavyo na wewe UTAWAHITAJI WENGINE KUKUSAIDIA kufikia ndoto za maisha yako!

DHANA YA MAISHA;
Katika maisha yetu hakuna hata mmoja wetu ambaye yuko sawa na mwengine kwa maana ya makusudi ya kuishi kwake, kila mmoja alizaliwa peke yake (hata mapacha kila mmoja alitoka kwa wakati wake); kwa staili yake na hata sasa kila mmoja ana ndoto zake na anaishi maisha yake. Ukilitambua hili hutamuonea wivu mwenzako katika moja ya ndoto zake,ila na wewe utatia bidii katika za kwako ila ikifika saa ya kusema ama kuonyesha ni kwa kiasi gani amesonga na ndoto zake na wewe utakuwa na ya kwako ya kusema. Ubaya ni kwamba watu wengi hawajitambui, kwa hiyo wanafanya maisha yanakuwa magumu sana huku duniani,maana mtu mmoja anataka kufanya kila kitu na kwasababu anabahatisha katika kila, basi atakuwa anajitahidi kumkwamisha kila anayejaribu au kufanya kama yeye!


UNAFIKI NISIOUPENDA.....
Kama umejitambua na unajiheshimu ni wazi kuwa na watu wanatambua hilo na sawasawa na kujiheshimu kwako ndio na watu wanavyokuheshimu. Ukiona mtu amekufuata na kukuuliza jambo lolote lile aitha anataka kulifahamu ama anataka ushauri wako au zaidi anaomba ushiriki wako....basi imekupasa kwanza kumshukuru sana Mungu kwa nafasi hiyo, hata kama hutafanya lolote katika haya anayoweza kuwa anayahitaji....nasemma hivyo ili ujue yafuatayo;

KWANZA UMETAMBULIWA KUWA UNAWEZA KUWA MSAADA KATIKA HILO.
PILI UMEHESHIMIWA SANA, MAANA WAKO WENGI LAKINI UMEONEKANA WEWE
TATU ULICHONACHO NDIO KAZI YAKE HASWA,MAANA TUMEPEWA ILI KUFAIDIANA.

Sasa kama ni hivyo basi ukipata nafasi hiyo mshukuru Mungu na baada ya hapo Omba hekima ya namna ya kujihusisha na jambo hilo na kama unaona huwezi kuhusika kabisa unaweza kumjibu kwa hekima SAMAHANI MIMI SITAWEZA, na yamkini ni vizuri hata ukimwelekeza kwa mtu mwingine unayeona anaweza kuwa na msaada!

Sasa usije ukadhani kwasababu una elimu ya juu sana au una umaarufu mkubwa au una kipaji sana au ni kiongozi maarufu au pesa kuliko wengine, ndio maana ukafuatwa wewe HAPANA!!
jIFUNZE Kuwaheshimu na kuwakubali wengine katika yote wanayofanya yanayostahili heshima....na mara zote HEKIMA NA MAWAZO MAZURI hutokana na watu tusiowadhania!

SASA SIKU HIZI KUNA NAMNA WATU HUKWEPA MAJUKUMU NA KUDANGANYA KWA NJIA YA MZUNGUKO, MTU ANAOMBWA JAMBO AU ANASHIRIKISHWA AU ANAALIKWA SEHEMU FULANI....HALI AKIJUA HANA NIA WALA MPANGO MOYONI AU NAFSINI MWAKE KWA KUSHIRIKI AU KUSHIRIKIANA....ANAISHIA KUTOA MATUMAINI FEKI ATI....."TUKO PAMOJA" AU "HAMNA NENO MTU WANGU" na hapo unamuaacha huyo ndugu akiwa na matumaini makubwa na ikifika saa ya jambo lenyewe usitokee kabisaaaa!!


Sasa ninafikiri ni wakati mzuri wa kujirekebisha sasa, kama huna nafasi au huwezi kumsaidia mtu kwa namna yeyete ile wewe sema tu....SAMAHANI NDUGU KWA HILI SITAWEZA!
Naamini hii itakusaidia pia kuwa HURU na kuwa MKWELI!

HIYO TABIA YA KUMWAMBIA MTU TUKO PAMOJA NA KISHA NYUMA YAKE UNAMNG'ONGA SIO HATA KIDOGO....TUJIREKEBISHE!!!

Ukiona inakufaa unaweza kuendelea nayo lakini kuna wakati itakugharimu tena sana, maana watu huwa wanaambiana yote yanayokuhusu na kama ni mambo ya kukalaisha basi ndio habari husambaa zaidi kuliko hata nzuri!

MFANO HAI;
Kuna mtu mmoja mahali fulani alikuwa anajifanya yuko bize kuliko hata ubize wenyewe, basi hata akiletewa kadi za michango ya harusi au shughuli mbalimbali alikuwa akijibu aaah tuko pamoja aisee....basi zingine anachangia na zingine hakuchangia na hata zile alizochangia nyingi hakuwa anahudhuria....naam hata ikitokea misiba jirani alikuwa anatuma rambirambi na kusema aaah jamani tuko pamoja kisha anaondoka....basi watu walimvumilia sana na hakuna nafasi watu walipata wasaa wa kumsema zaidi ya marafiki mmoja mmoja ambao aliwachukulia poa na kusema...aaah nimewaelewa jamani....tuko pamoja sana!
Basi ilitokea siku mmoja siku moja alipata msiba wa Baba yake mzazi ambaye alikuwa anaugulia kwake, watu walipata taarifa za msiba na wengi wao wakasema hapa ndio mahali pa kumuonyesha UPAMOJA WETU....basi wengi walifika na kutoa pole na kuacha rambirambi (tena nyingi kuliko kawaida) na wao walisema tuko pamoja katika majonzi haya na kuondoka zao....basi kwa kadri muda ulivyokuwa unakwenda alikuwa akipokea rambirambi na pole za watu wanaokuja na kuondoka kama vile ile ni shule ya kutwa ama kituo cha kupigia kura....basi pale msibani palikuwa doro kabisa na hapo ndio akaanza kuona kimbembe cha "TUKO PAMOJA"....basi msiba ulikaa siku ya kwanza yote hamna kitu,basi akawachukua vijana ili awalipe na wakachimbe kaburi, na wao walichukua pesa na wakamwambia tuko pamoja na wao wakaenda makaburini na kuanza kupiga stori, mpaka siku ya pili inaisha baada ya kufoka sana ndio wakachimba tena refu kupita kawaida...naam siku ya tatu ndio ya mazishi hakuna hata mmoja anajigusa kwenda, na hapo alienda kwa kiongozi wa mtaa na kumuomba awaite watu, naam watu walikuja na wakaenda mpaka makaburini kimyakimya,hakuna mtu kulia wala kuzungumza na walipofika pale....watu walimtolea madukuduku yao yooote na wakasema ili iwe fundisho kwa wengine,kabla ya kuzika....ALALE JUU YA UDONGO ULE WA KABURI PALE JUU,NA HAPO AKACHARAZWA BAKORA ZA KUTOSHA MBELE YA MKWEWE,WATOTO NA NDUGU ZAKE NA ndipo ibaada ya maziko ikaanza na kila hatua ya kuzika alipaswa kushiriki ili ajue huwa inakuwaje....alisaidia kushusha jeneza chini na kabla mtu yeyeote hajagusa chepeo,alianza yeye kufukua mpaka alipochoka hoi ndio wakamsaidia,na hilo lokawa fundisho kwake na kwa wengine wote mtaani kuwa pesa sio kila kitu,ila unahitajika wewe!!!


ACHANA KABISA NA HUO UNAFIKI WA KUSEMA TUKO PAMOJA HALI HUNA HATA KIMOJA KINACHODHIHIRISHA UPAMOJA HUO!!!
(Watu wawili hawezi kwenda njia moja isipokuwa wamepatana.....hivyo hamna Upamoja wa maneno bila matendo na mapatano)

AHSANTE SANA, UBARIKIWE SANA KAMA UMENIELEWA!!!

Fredy Erasto Chavala
<King Chavala(MC)>
+255 713 883 797
facebook; King Chavala MC
Twitter @kingchavala