CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Papaa On Tuesday....Kuku anayetaga Huwa Hachinjwi!!!!


Kwenye kiswahili kuna methali, nahau na Misemo ambayo huwa inatupa tafakari ya kina kuhusu maisha. Na hii misemo yote ni kwa ajili ya kutufunza kile wahenga wanachodhani ni busara kwenye kizazi chao, Chetu na kinachokuja kujifunza kutoka kwao katika yale waliyoyapitia. Kwenye mila za Kiafrika kuku huliwa wakati wa sikukuu ama anapokuwa anakuja mgeni. Ukiacha siku hizi kwenye huu ujio wa Kuku wa Kizungu enzi hizo wakati Nahau zinatungwa kulikuwa hakuna wazo kama kuna Kuku aina nyingine watakuwepo duniani kila nyumba ilikuwa na utamaduni wa kufuga kuku hasa kwenye jamii za wafugaji, inapotokea kuna ugeni katika nyumba fulani basi ndio wakati muafaka sana wa kuku kuchinjwa. Katika banda kulikuwa kuna jogoo na wale wanaotaga kwa ajili ya kutotoa kuongeza uzao. Kuku wanaotaga walikuwa wanahifadhiwa kwa ajili ya manufaa ya baadae ndipo wahenga wakasema "Kuku anayetaga huwa hachinjwi".


Kuna mambo kadha wa kadha ya kujifunza kupitia kuku wa kutaga na suala zima la kuchinja kuku. Kuchinja ni kuondoa uhai wa kuku na kupoteza faida ambazo mfugaji angeendelea kuzipata iwapo angeendelea kufuga yule kuku. Tunachangamoto kubwa sana ya kujua kwenye maisha yetu nini ni kuku anayetaga na lini pia achinjwe. Wengi tumekuwa tukichinja kuku anayetaga na kupoteza kabisa dira za kwenye maisha. Fursa ambazo huwa zinakuja kwenye maisha yetu ni nadra sana kuzirudia kwa sababu mbalimbali tumekuwa tukizipoteza ama kuziharibu kwa kutokujua kuwa yamkini fursa hizo zingetusaidia kwa mambo mengine kwenye maisha.


Mara kadhaa nimeongea kwenye hadhara ambazo nimekuwa na fursa ya kuzungumza kuhusu Kizazi tulichonacho kisivyoweza kuziona na kuzithamini fursa tulizonazo. Wengi wetu ni ngumu kuzikabiri changamoto tunazokutana nazo kwenye maisha iwe ajira, iwe mahusiano, iwe kitaaluma iwe chochote kile kizazi hiki tumejifunza kuchukua maamuzi ya hasira kuliko busara, wengi tunaamini tunaweza ishi bila yeyote,na tunaweza fanya chochote pasipo msaada wa yeyote mwisho wa siku tunakwama kwenye mambo mengi kwa sababu tulidhani sisi ndio kila kitu. Ndio maana leo mtu akiwa na hasira anaweza ukashangaa alikuwa anafanya kazi kutokana na namna moja ama nyingine anakasirishwa na mazingira ya kazi anaamua kuongea yote, anafunguka kupita maelezo utamsikia "kazi itakuwa hii bana, kazi zipo za maana, kaofisi gani haka" anaongea mwisho wa siku anaamua kuacha anarudi nyumbani hasira zikiisha anagundua kuwa alitukana Wakunga wakati uzazi ungalipo alimchinja kuku anayetaga tena kwa kisu butu.

Maamuzi ambayo tunayafanya kwenye maisha hutugharimu iwapo hatutajua matokeo ya maamuzi hayo maana tunao uwezo wa kuchagua nini cha kufanya hila hatuna uwezo wa kuamua namna ya matokeo iwapo tu matokeo yanajulikana na unapaswa ukubaliane nayo. Unao uwezo wa kuchinja kuku anayetaga ama asiyetaga. Asilimia kubwa ya watanzania tunaishi katika nyumba za kupanga unaishije na majirani zako, unaishije na watu wanaokuzunguka. Mkorofi hana dini wala kabila dini yake na kabila lake ni Ukorofi. Ukiona majirani hawakushirikishi katika mambo yao mengi ujiulize unaishije na walimwengu. Ukitaka kujua kipimo kidogo cha wewe unavyoishi na walimwengu subiri ikifika jambo lako uone walimwengu watalipokeaje na kulichangamkia kiasi gani. Kama wewe kila msiba uko busy ama kila mambo ya wenzio uko busy basi subiri ya kwako yakifika na ukagundua unawahitaji watu wawe na wewe. Biblia inasema unavyotaka watu wakufanyie wafanyie wewe kwanza. Jirani na nilipokuwa nikiishi Block 41 enzi hizo kulikuwa na mdada ambaye alikuwa na gari yake full tinted, anaweza akapita kijiweni wala asisalimie ingawa salamu haipotezi chochote, anaweza akakukuta barazani atataka wewe ndiwe umuanze alikuwa anajua hawahitaji wale watu wa mtaa ule yeye level nyingine siku ya siku gari lake likaingia kwenye mtaro, dada wa watu akashindwa kushuka kwenye gari akahangaika mwisho akashuka watu wamekaa kwenye vibaraza vyao wanamtazama, akaenda kuomba vijana wa kijiweni wamsaidie wakamuuliza "hivi leo ndo unajua sisi ni watu"??pamoja na kutangaza angetoa fedha watu wakamkatalia, akadhani atashinda vita ya wema kwa nyodo akachukua simu akampigia boyfriend wake aje nae alipofika hakuwa na msaada ikabidi apige kaka wa watu aombe radhi kwa niaba ya mpenzi wake ili kupata msaada wa kusukuma gari lile, ajabu wale vijana wakasukuma gari na wakakataa kuchukua hela, tangu siku ile maisha ya mdada yalibadirika salamu mbele kama skafu ya Chama Cha Maskauti.

Kwanini tufanya maamuzi ambayo hata kama yatatugharimu baadae lakini tuchague kwa busara. Kwanini kuvunja simu ya mumeo au mpenzio kwa sababu eti umekuta sms usizozielewa. Kwani tatizo ni simu ama ni mtu wengi tunapambana na matokeo ya tabia tukidhani tunadhibiti chanzo cha tabia. Juzi kati nimesikia kuna mtu amechoma gari la mumewe baada ya kukuta kwenye gari la mumewe kuna Condom. Sasa ukichoma gari ndio unakuwa umemaliza tatizo la usaliti??Usiharibu leo wakati unajua kesho utahitaji ama utawahitaji hao watu ama mtu. Kizazi chetu ni kizazi cha Maamuzi ya hasira wapenzi wakikosana solution ya kwanza ni Kuchuniana, baada ya masaa 600 ndio wanakuja kuanza kuongelea mgogoro wao wa mapenzi. Kiwango cha kukabiriana na changamoto kinadhoofishwa na maamuzi wa haraka haraka tunayoyachukua huku tukiwa bado tunauhitaji wa kile ambacho tunataka kukipoteza leo. Tumechinja kuku anayetaga wa kazi zetu, tumechinja mahusiano yetu, tumechinja biashara zetu wenyewe wakati bado tunavihitaji.


Idadi ya watu wanaoweza kuamini inazidi kupungua, kila mtu anajihami na mwenzake kisaikolojia ama kivitendo kabisa, kwenye ajira mabosi wa kikaburu na wafanyakazi wa kibongo full stress, wanandoa wanawake walishaamini hakuna mwanaume ambaye ha-chit wote wanachit sema hatujui tu, wanachit kwa sms, wanachit kingono, wanachit ki fedha, marafiki wanaoaminiana wako wachache wengi wetu wanaishi bila na kuwa best friend, wengi wanaishi maisha ya wenyewe wenyewe wakidhani wakikaa wenyewe ndio watakuwa salama zaidi. Nani anamwamini nani kiasi cha kwamba akafunguka asilimia 500 hata wachungaji hawaaminiwi itakuwa waumini. Ukimkopesha mtu fedha leo unaweka na asilimia za kuamini kuwa utazungushwa kuipata hela yako. Kuna wengine kwa ajili ya kukopa kopa wanashindwa kabisa kuaminiwa hata kama wanashida kubwa na ya ukweli. Kuna siku walichinja kuku wa kutaga matokeo yake hana tena msaada kutoka kaw watu. Ukifika saa ya wewe kukopa basi kila mtu atatoa sababu utasikia "yaani sasa hivi hapa nimelipa ada".

Kila maamuzi unayoyachukua leo yatakugharimu either kwa heri ama kwa shari. Ukiamua kuchinja kuku wa kutaga basi jua unapoteza kuku na mayai, na vifaranga. Busara katika kuamua ndio msingi wa maendeleo. Inawezekana leo ukaamua jambo ambalo wengi wasijue maana yake. Inawezekana una kuku mmoja ndo huyo huyo ambaye anataga hata angekuja mgeni gani huwezi mchinja huyo kuku sababu una hakika kabisa nikimuacha leo baada ya siku chache nitakuja kuwa na kuku wengi. Maamuzi ya kutokuchinja ni maamuzi yako na sio maamuzi mepesi lakini maamuzi ya kutokufanya sasa yana faida zaidi kuliko ukaamua kuchinja leo. Kuna mambo mengi sana kwa sababu ya marafiki, sababu za tamaa zetu, sababu za Kutafuta sifa kwenye maisha tumejikuta tumechinja Kuku anayetaga na kusahau kuwa yamkini huyu kuku angetufaa baadae. Majuto ni Mjukuu wa Baba anayeitwa maamuzi na mama anayeitwa wakati sahihi. Ukiamua jambo sahihi wakati sahihi unaitwa una hekima kama sio busara, ukikosea hapo utakutana na majuto mtaa wa mbele.

Kukua wa Kutaga Huwa Hachinjwi.
Ze Blogger

0798020110.

Papaa On Tuesday Kwa Hisani Ya Friends On Friday.