CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Papaa on Tuesday(PAPAA ON HONEYMOON)....Wewe ni sehemu ya maisha yangu (You're the part of ma life)

.....WARAKA TOKA HONEYMOON!!


Nikiwa bado niko honeymoon naomba leo nizungumze na wewe kuutambua Moyo wa Mwanamke.Ni wazi kua moyo wa mwanamke ni wa utofauti sana kuliko sisi tunavyomtazama napenda kuchukua nafasi hii kukufahamisha au kukutambulisha mwanamke aliyebeba kusudi lako,hatima yako,mwanamke aliyesababisha Mungu ashike damu kwa mara ya kwanza maana kuna sababu kubwa sana ya Mungu kumtoa mwanamke katika ubavu wa mwanaume kuna sababu kubwa sana ya Mungu kuruhusu damu kumwagika,Mungu sio katiri na wala hakufanya jambo la kinyama na wala hakutaka kumuumiza Adamu ila alikuwa na kusudi na malengo maalumu sana na jambo zuri sana kwa Adamu ndio maana alifanya yeye mwenyewe kazi hiyo ya upasuaji,maeneo mengine yote Mungu aliamuru watu wachinje wanyama na damu ifanye kazifulani na hata kwa Yesu aliruhusu apigwe na kuchomwa mkuki ili damu ifanye kazi lakini kwa Adamu aliingia mwenyewe hakuitaji mikono ya mtu ndio maana maandiko yanasema mke mwenye busara hutoka kwa Bwana'
 Hapa inatubidi kuliangalia kiundani sana kusudi la Mungu kumtoa mwanamke kwa mwanaume kwa kuusoma moyo wa mwanamke aliyebeba kusudi lako.Kwa nini mimi Samuel Sasali nili mpenda mke wangu kipenzi Milembe John Madaa,hakuna anayependa bila sababu na hakuna anayependwa bila sababu zinzomfanya,mtu kupenda au kutopenda hata Mungu alikuwa sababu za kuupenda ulimwengu hata kumtoa mwana wa pekeee ulimwenguni.Kupenda sio dhambi na kutopenda sio dhambi upendo ni sehemu ya maisha na ni Mungu ambaye ameweka kwa mwanadamu hivyo.
 LOVE imetoka kwa mungu sio mtu ameamua kupenda jua kuwa love ni sehemu ya maisha hata wanyama wanapenda na wana wivu wao kwa wao lakini love ya mwanadamu ni kubwa na inanguvu kuliko wanyama sababu nilizo nazo kwanini ninapenda na kwanini natakiwa kumpenda?
(a)Kwa sababu naitaji kufalijiwa (nafsi)
(b)Kwa sababu naitaji kukamilishwa (mwanz 2:18)
(c)Kwa sababu Upendo ni Asili
(d)Kwa sababu ni mpango wa Mungu
(e)Kwa sababu nahitaji kupendwa

 Love haijengwi kwa mali,pesa,watoto,uzuri,elimu,wadhifa wako,Uaskofu,Uchungaji,Utume,Udaktari.Upendo unajengwa kwa maneno matamu (palatable word) (sweet word) maneno yenye uwezo wa kukamata hisia ya mtu na kumfanya achilie maisha yake kwako yanatakiwa maneno yenye nguvu ya ushawishi na hata sex haijengi ndoa bali sex ni (thanksgiving) ni sadaka ya shukurani baada ya mambo muhimu kufanyika watu wengi wamedanganyika kuwa sex ndio upendo kitu ambacho sicho na ni afundisho potofu,vitu vinavyotengeneza upendo ni vidogo sana na vinadharauliwa sana kama busu,kukumbatia,mawasiliano na muda wa kutosha na mwenzi wako.
 Upendo unafanya mtu kujua kusudi la kuumbwa fulani kwa ajili ya mtu fulani,mwanadamu amegawanyika katika sehemu kuu tatu 1)Nafsi 2)Roho 3)Mwili kumbuka moyo unahitaji kufarijiwa,unahitaji kupendwa na unahitaji kuheshimiwa.

Papaa

SASA SAMUEL SASALI AMEKAMILISHWA NA MILEMBE MADAHA NA TANGU LEO ATAITWA MR.!!!

HONGERENI SANA SAMUEL SASALI NA MILEMBE MADAHA KWA KUFIKIA HATUA HIYO YA KUWA MUME NA MKE......"SAMILEMBE"

CERTIFIED MR SAMUEL AND MRS MILEMBE SASALI
SASA HAWA NI MUME NA MKE RASMI NA HIVYO NDIO VYETI VYAO VYA NDOA!!
NA HIYO HATUA HAPO JUU ILIFIKA BAADA TU YA KIAPO CHA KILA MMOJA KWA MWENZAKE PAMOJA NA PETE YA AHADI YA NDOA NA KUTUNZA KIAPO HICHO
 VAA PETE HII,IWE ISHARA YA AGANO LANGU KWAKO.....
 VAA PETE HII.....
GROOM'S MEN PAMOJA NA SAMUEL SASALI

MAIDS KUMPAMBA MILEMBE
KULIKUWEPO GROOM'S MEN NA MAIDS 30 KUIPAMBA HARUSI HII YA PAPAA SEBENE!
WALIINGIA KWA FURAHA SANA NA KILA MMOJA ALIFURAHIA UCHANGAMFU WAO

MR SAMUEL AKIONGEA NA KUMSIFIA MKEWE
MRS MILEMBE MADAHA WA SAMUEL AKIONGEA
TUKAPATA KUSIKIA SAUTI ZAO,WAKASEMA NA HATIMAYE WAKAPUMZIKA KIDOGO KABLA YA KUANZA ZOEZI LA KEKI!
MR & MRS SAMUEL AND MILEMBE SASALI
HATIMAYE WALIKATA KEKI NA KULA NA

KIPEKEE WALITOA ZAWADI YA KEKI KWA WATU WAO KADHAA MUHIMU SANA, AMBAO WAMEKUWA MSAADA KWA KILA MMOJA WAO NA KWA MAHUSIANO YAO.....BAADHI YA WALIOPEWA ZAWADI YA KEKI NI PAMOJA NA WAZAZI WA PANDE ZOTE MBILI,
 MILEMBE ALIPELEKA UKWENI...
NA HUKU PIA VIVYO HIVYO!

KAMATI YA MAANDALIZI,MARAFIKI HURU,AFLEWO TEAM,DK PARVINA,PROSPER MWAKITALIMA,APOSTLE ONESMO NDEGI, LINDA TEMBA NA DK.HURUMA NKONE, MCHUNGAJI ALIYEFUNGISHA NDOA HIYO!!
KEKI KWA MCHUNGAJI NA MKE WAKE

KEKI KWA PROSPER MWAKITALIMA

KEKI KWA DK PARVINA
HATIMAYE WATU WALIKUJA KUMPONGEZA KWA KUCHEZA NA KUMRUSHA JUU SANA...
NA BAADA YA HAPO MENGI YALIENDELEA,KAMA VILE KUONA SHORT DOCUMENTARY NA HATIMAYE CHAKULA,NA HAPO WALITUMBUIZA THE VOICE,SAMWEL YONAH, AMANI KAPAMA, BOMBY JOHNSON PAMOJA NA KING CHAVALA-MC NA KIBAO MAALUM KABISA KWA MAHARUSI "SAMILEMBE"
KING CHAVALA-MC
WATU WALIKUWA WAKITOA ZAWADI MLANGONI,LAKINI KUNA BAADHI YA WATU AU MAKUNDI MAALUM YALILAZIMIKA KUPELEKA MBELE ZAWADI ZAO.
KAMATI YA MAANDALIZI ILIENDA MBELE KWA KUCHEZA KAMA HIVI
CHRISTIAN BLOGGERS NAO HAWAKUBAKI NYUMA KATIKA KUMPONGEZA MWENZAO!
"SAMILEMBE"

HATIMAYE BAADA YA YOTE WALIPIGA PICHA NA KUONDOKA KUELEKEA HUKO AMBAKO HAKUNA AJUAYE NA WAO HUJUA TU WAKISHARUDI!!

SHUKRANI NYINGI SANA KWA KAMATI YA MAANDALIZI  NA KILA ALIYEHUSIKA KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE KUFANIKISHA JAMBO HILI,AHSANTE SANA MWENYEKITI NOEL TENGA KWA KUKUBALI KUTUMIKA KUBEBA JUKUMU HILI!

KWA NIABA YA TIMU NZIMA CHA YA CHAVALA MEDIA, TUNAWATAKIA KILA LAKHERI NA MAISHA MAREFU SANA YENYE FURAHA NA AMANI NA UPENDO WA KWELI WATU HAWA MUHIMU SANA KWETU,AMEN!!

IMEANDIKWA NA 
King Chavala MC
+255 713 883 797

JOHN LISU KUREKODI DVD YAKE LIVE TAR 06/10/2013 PALE CCC-UPANGA,DAR ES SALAAM!!



UKO HAPA DVD LIVE RECORDING
 NA JOHN LISSU,
06/10/2013,CCC-UPANGA, DAR ES SALAAM, TANZANIA.

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE;



SALAM Tanzania!
Shalom Dar es salaam, Shalom Tanzania!
Ndugu wanahabari na watanzania wote kwa ujumla!
Naamini tuko salama na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku alizotupatia Mungu wa mbinguni, tumshukuru Mungu sana kwa Amani na utulivu aliotupa na tuendelee kumuomba ili atuepushe na kila aina ya dhahama na uharibifu wa Yule adui!
Kama tulivyosikia hivi karibuni, yale yaliyotokea nchi jirani ya Kenya, kwa hakika tunawapa pole sana kwa mkasa huo, pole kwa wale waliowapoteza wapendwa wao na wale waliojeruhika tunawaombea wapone haraka, tunaamini hekima ya Mungu itakuwa juu ya serikali yao kushughulikia jambo hilo kikamilifu.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, hata sasa tunapoende kumalizia robo ya tatu ya mwaka 2013, tumeshuhudia mambo mengi sana mwaka huu ya kila aina, yapo yale yalionza kwa mara ya kwanza na mengine yamekuwa ni mwendelezo tu wa yale yadumuyo au yalioyaanza hapo kale, tumeshuhudia michezo mbalimbali na vipaji lukuki vikiinuka na kuimarika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, na kwa yote mema na mazuri tunampa Mungu Utukufu kwa hakika!

UTANGULIZI;
John Lisu ni mmoja wa waimbaji/Waabudishaji wanaoheshimika katika Tasnia ya muziki wa Injili kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza muziki wa Injili nchini Tanzania na nje ya Nchi. Nyimbo nyingi alizozitunga na kuziimba zimekuwa zikitumika katika makanisa mbalimbali kama nyimbo za kusifu na kuabudu; pia waimbaji wengine waliokua wakiimba naye wameweza kukua na kufikia uwezo wa kuwa waimbaji wa kujitegemea. John Lisu pia ametia hamasa kubwa miongoni wa wanamuziki wa Injili kuanza kufanya muziki wa live. John Lisu ameweza kufanya tours za ndani ya Tanzania, Africa na Bara la Ulaya kwa ajili ya huduma.
John Lisu anategemea kufanya Project II ya Live recoding inayojulikana kama "UKO HAPA" baada ya project ya kwanza ya Jehova yu hai kufanya vizuri sana. Tamasha litafanyika ndani ya ukumbi wa City Christian Centre (CCC) Upanga tarehe 6 Octoba 2013, kuanzia saa 8. mpaka saa 2 usiku. Tamasha litasindikizwa na waimbaji nguli kama Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Pastor Safari Paul, Bomby Johnson Waimbaji wote wamethibitisha kuwepo. 

VENUE:
City Christian Centre (CCC) mkabala na chuo kikuu cha mzumbe
Si mbali saana kutoka Diamond Jubilee
USAFIRI (basi zilizobandikwa matangazo ya tamasha) utakuwepo kutoka posta mpya kwenda ukumbini kuanzia saa saba na nusu mchana kwa bei ya kawaida.
HABARI NJEMA-MUHTSARI!!!!!

Sasa kwa mara pili nchini Tanzania, mwimbaji WA NYIMBO ZA INJILI na mwabuduji JOHN LISSU wa jijini Dar Es Salaam, atakuwa anafanya Ibaada kubwa ama Tamasha la kusifu la Kuabudu(LIVE PERFORMANCE), litakalorekodiwa moja kwa moja (DVD LIVE RECORDING) lenye jina “UKO HAPA” (Yaani Mungu na Uwepo wake).
Tamasha hilo litafanyika jumapili ya Tarehe 6, Octoba 2013  katika Ukumbi mkubwa wa kisasa wa Kanisa la City Christian Centre (CCC)- Upanga, mkabala na Chuo Kikuu Mzumbe – tawi la Dar es salaam, kuanzia saa nane mchana.
Tunataraji watu 5000 kuwa sehemu ya tamasha hili la kipekee,Utakuwa sehemu ya tamasha hilo kwa tiketi ya 10,000/= (kawaida), 20,000/= (VIP) na 3000/= (Watoto);
na Kwale watakaohitaji tisheti maalum za tukio hilo, basi zinapatikana kwa kati ya 12,000-15,000/=, wewe wasiliana tu na (0713905118)

VITUO VYA KUUZIA TIKETI;
1.   MWENGE – Tarakea duka la Kanda
2.   KINONDONI – DPC
3.   MLIMANICITY – Silverspoon Restaurant
4.   KARIAKOO – Mbogo Shop
5.   UKONGA BANANA – KWA GIDO
6.   POSTA - DUKA LA MSAMA

T-SHIRTS
-T-shirts maalumu kwa wanaume na wanawake zinapatikana katika vituo vya kuuzia tiketi kwa bei ya elfu kumi, mpaka elfu 15(kutegmeana na aina).

N.B; Kwa tiketi ya VIP, mnunuzi atajipatia na Audio CD ya John Lissu ya “Uko Hapa”

USAFIRI UTAKUWEPO!!
Siku ya tamasha kutakuwepo usafiri kutoka Posta Mpya mpaka CCC-Upanga,eneo la tukio, hivyo kama wewe ni mgeni na hupafahamu mahali hapo, basi utakachotakiwa kufanya ni kupanda magari toka ulipo mpaka posta mpya kabla ya saa nane,na hapo utayakuta mabasi yenye mabango ya Tamasha, basi utajongea humo na hapo utawezeshwa kufika eneo la tukio, muhimu ni kuzingatia muda!

MUHIMU SANA!!

Tamasha hili ni muhimu sana kwa Tanzania, hasa ukizingatia JOHN LISSU ni mmoja wa waimbaji wa kwanza kuimba live kila mahali anapoalikwa na ni mwimbaji wa kwanza binafsi kufanya LIVE DVD RECORDING pale Ubungo plaza, na ile ya kwanza iliitwa “JEHOVA YU HAI” na sasa anafanya LIVE RECORDING kwa viwango vingine bora zaidi, maana Mungu hutupa hatua moja zaidi kila siku.
Ni muhimu kwa kila mtanzania kujivunia kipaji na tukio hili muhimu katika historia, njoo umwabudu na kumsifu Mungu pamoja, Njoo ujifunze, Njoo umuunge mkono mtanzania mwenzako na njoo uje ufanyike sehemu ya Historia hii kwa Utukufu wa Jehova.

MWALIKO MAALUM;
Kipekee Ninapenda kuwakaribisha wachungaji, mitume, manabii, wainjilisti, waalimu na viongozi wote wa makanisa na huduma mbalimbali, ninawakaribisha viongozi wote wa kisiasa na kijamii kutoka serikalini na vyama vya siasa vyote, ninapenda kuwakaribisha wanaharakati na wanataaluma wote, ninapenda kuwakaribisha waimbaji wote wa nyimbo za injili na wanasanaa wote, ninapenda kuwakaribisa wanafamilia wote, asiwepo wa kubaki nyuma, ninapenda sasa kukukaribisha wewe unaesoma hapa, naam nisaidie kumkaribisha na mwenzako na yeye aje na mwenzake, kimsingi tukio hili ni letu wote bila kujali kitu chochote, njooni tumsifu na kumwabudu Bwana na Mungu hataacha kuibariki Tanzania!

SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Hakneel Production (Wadhamini wakuu), na Jonn Lissu na timu nzima ya maandalizi; Kanisa la CCC-Upanga; vyombo vya habari hususani Praise Power na WAPO Radio; Clouds TV kupitia CHOMOZA na Clouds Radio kupitia GT; Sibuka Tv kupita Gospel Hits; Bloggers hususani Christian Bloggers, magazeti na vyombo vingine vyote vya habari! Shukrani hizi zimfikie kila mtu mmoja mmoja aliyetoa mchango wa mawazo, fedha, ushauri, maombi, ubunifu, yaani mchango wowote wa hali na mali na Mungu awabariki nyote!

MUHTASARI MKUU;
Tukio; TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU, LITAKALOREKODIWA
(DVD LIVE RECORDING CONCERT)
Mhusika; JOHN LISSU
Jina: “UKO HAPA”
Mahali; UKUMBI WA KANISA LA CITY CHRISTIAN CENTRE (CCC)- UPANGA
Lini; 06TH OCTOBA, 2013
Muda; KUANZIA SAA NANE MCHANA
Kiingilio; Tsh 10,000/= (kawaida); 20,000/= (VIP) na 5000/= (Watoto)

Wasindikizaji; CHRISTINA SHUSHO, MIRIUM LUKINDO, PASTOR SAFARI, BOMBY JOHNSON, NEEMA GOSPEL CHOIR-AIC Chang’ombe na PAUL CLEMENT.

Mengineyo; USAFIRI UTAKUWEPO TOKA POSTA MPAKA CCC-UPANGA na Unaweza kujipatia Tisheti pia.
Wahusika; WATU WOTE MNAKARIBISHWA!


UKIPATA HABARI HII USIACHE KUMSHIRIKISHA NA MWENZAKO, NAAMINI HAUTAKOSA TUKIO HILI MUHIMU LA KIHISTORIA KATIKA NCHI YA TANZANIA KWA UTUKUFU WA MUNGU!!


PICHA NA TAARIFA


MAWASILIANO:
O713 240 397 – JOHN LISU
0713 905 118 –PROSPER MWAKITALIMA – EVENT MANAGER
0713 883 797 - FREDY CHAVALA - PUBLICITY


Imetolewa na;
Fredy E. Chavala <King Chavala (MC)>
Publicity Manager
+255 713 883 797
On Behalf of The Organizing Committee

John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha!!


John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha.
John Shabani

JOHN Shabani si jina geni masikioni mwa watu hasa wapenzi wa muziki wa injili na wanafunzi wa muziki huo.

John mzaliwa wa kijiji cha Kirando katika kitongoji cha Nyankima, kata ya sunuka, Wilaya ya Kigoma Vijijini, anatokea katika ukoo wa waumini wazuri wa dini ya kiislam.

Muimbaji huyo ambaye umaarufu wake uliwika baada ya kushiriki tamasha la pasaka ambalo anasem akuwa liliinua uimbaji wake na anatamani kama atapewa nafasi ya kushiriki tena kwa miaka ijao ikiwemo mwaka huu.

Anasema kuwa historia yake baada ya kumaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi kirando, alijiunga na elimu ya sekondari, lakini kutokana na itikadi za kidini, alijikuta akiwa katika wakati mgumu wa kupigwa vita na wazazi, kwasababu ya uamuzi wake wa kujiunga na Dini ya kikristo hali iliyomsababishia muimbaji huyo kuishi miaka mingi akiwa mbali na wazazi wake.

Mwaka 1992, John akiwa kijana mdogo, alipata ufadhili wa kwenda nchini Kongo ambako huko alijifunza muziki na kusoma Chuo cha Biblia na ndipo kipaji chake cha kutunga nyimbo na kuimba kilijitokeza kwa kasi.

Muimbaji huyo anasema kuwa hakutaka kuona mtu yeyote akiwa katika hali ya kukata tamaa, maana alifahamu madhara yake kwasababu hiyo, alianzisha vikundi mbalimbali vya vijana akiwa na lengo la kuwaelimisha ili kujikwamua katika hali ya kukata tamaa na kutokujihusisha na vitendo viovu kama vile madawa ya kulevya, Ukahaba na anasa za kila aina mambo ambayo aliyapiga vita.

Shabani anasema kuwa ameishi miaka mingi kama yatima, lakini hali hiyo imemsaidia kujifunza mengi na kuwa na tabia njema, kumheshimu na kumthamini kila mtu, hali hiyo ilimfanya kupata kibali machoni pa wengi.

Anasema kuwa amekuwa msaada kwa vijana wengi ndani na nje ya nchi na kuwakwamua waliokuwa wamekata tamaa na kujihusisha na vitendo viovu.Pia kutokana na ujuzi wa muziki alioupata na kipaji alichonacho cha kutunga, kuandika nyimbo na kuimba, anasema kuwa amekuwa msaada kwa waimbaji mbalimbali binafsi na vikundi , hasa nyimbo za Injili.

Mwaka 2001 John alifunga pingu za maisha na Debora Shabani na mwaka 2002 walifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwae Joyce, akiwa na maana ya kuyasahau maisha ya huzuni na shida na kujitabiria maisha ya furaha.

Mwaka 2004, John aliajiriwa katika kampuni ya Msama promotions ya jijini Dare es salaam, kampuni inayojihusisha na kuinua vipaji na pia kuwainua vijana na watu wa rika na jinsia zote waliokata tamaa ya maisha na hasa wale walioko vijiweni wakijihusisha na madawa ya kulevya, ukahabaa

Albamu yake ya kwanza Marufuku kukata tama anasema kuwa imewasaidia wengi waliokata tamaa na kuwapa matumaini mapya albamu hiyo na nyingine alioirekodi mwaka 2009 zilizoitwa huu ni wakati wangu na Moyo wangu.

John ametembelea nchi mbalimbali, akijifunza maisha ya watu ikiwemo kugundua kwamba karibu asilimia kubwa ya wanadamu, awe maskini, tajiri, msomi au asiye na elimu, wenye vyeo au waajiriwa, watoto kwa wakubwa, wanaume kwa wanawake, awe mzungu au mweusi n.k, wote kwa njia moja au nyingine wamepitia katika hali ya kukata tamaa au kukatishwa tamaa na jambo fulani, mtu, watu, hali au mazingira fulani.

Ndipo mwaka 2006, alipata maono na msukumo mkubwa wa kuandika Kitabu ambacho kitakuwa msaada kwa njia moja au nyingine kwa kila atakayekipata. Kitabu hicho kinaitwa Marufuku kukata tama. Kitabu hicho pamoja na kile kiitwacho “Mafanikio yatokanayo na kusifu na kumwabudu Mungu” vinategemea kukamilika baada ya miezi miwili.

Mwaka 208 sitausahau  ilikuwa ni siku ya huzuni na majonzi, siku ya kilio na kuomboleza. ni siku alipofariki mke wake mpendwa na mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili, Debora Shabani, mwimbaji aliyegusa mioyo ya watu wengi ndani na nje ya nchi, niliumia sana lakini sikukata tamaa”anasema.

Shabani alitunukiwa tuzo ya heshima pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake kwa ajili ya kuinua vipaji na pia kuchangia kuinua muziki wa Injili Afrika mashariki na kati. Pamoja na hayo amekua akianzisha vikundi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu Tuzo anayosema kuwa ilitolewa na kampuni ya Christian promoters Ltd, Pia ni miongoni mwa waanzilishi na kiongozi wa Chama cha muziki wa injili Tanzania (Chamuita).

Mwaka 2011, John alipata heshima kubwa kama mwalimu, kuongoza kundi la waimbaji (Tanzania gospel all stars) kuimba wimbo maalum wa miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.

Anasema kuwa pamoja na mzigo mkubwa aliokuwa nao kwa kidogo anachopata,amehakikisha kuwa anaisaidia jamii, hasa watu wenye ulemavu, wajane na yatima Vijana waishio katika mazingira magumu, pamoja na wakimbizi. Tayari ameanza mikakati ya kusajili Taasisi Hope Foundation kwa ajili ya maono hayo.

Pamoja na malengo mbalimbali aliyonbayo Shabani, lakini pia ni kuwa na kituo cha watoto na vijana, lengo ni kuandaa kizazi chenye maadili mema, kuibua, kutambua na kuinua vipaji vya watoto na vijana, mbinu na mikakati ya kuwakwamua watoto

Pia anasema kuwa mpango huo unalenga kutafuta ufadhili kwa ajili ya kuaendeleza vijana kielimu pamoja na kuwawezesha pale inapobidi, kuandaa matamasha ya watoto na vijana, kuunganisha watoto na vijana wengine duniani, kuwapa kipaumbele watoto na vijana wenye elemavu, kuwa na kiwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali ya watoto na vijan.

Kwa sasa anajishughulisha na kufundisha bendi,vikundi na waimbaji binafsi na kusema kuwa lengo ni Kufundisha kuimba au kunyoosha,Jinsi ya kuitumia sauti kuitunza na kuitawala,  Historia ya muziki na maadhi ya muziki, Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora, Matumizi ya kipaza sauti,Kuwatungia nyimbo au kurekebisha nyimbo zilizotungwa tayari, Kutoa ushauri kwa wanaotatarajia kuingia studio, mbinu za kuitangaza albamu au nyimbo zikubalike na Kutengeneza muziki wenye viwango.


Papaa On Tuesday...Hata Ukizima Mshumaa Wa Mwenzio Haufanyi Wako Uwake Zaidi

Ninakila Sababu Ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya siku ya Leo kwa Kuweza Kutupa tena Uzima katika Maisha haya tuliyo nayo. Kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu,kuna rafiki yangu Zulfa alitoka kwenda Matembezi ya Weekend amepata ajali wamekata Mguu sasa ni Kilema. Hata kama hakuna aliyekufa ama kuwa kilema kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu kwamba tunaishi.

Mwanamuziki Elton John akiwa na Bernie Taupin Mwaka 1973 waliuandika wimbo "Candle In The Wind" ukiwa maalum kwa ajili ya heshima ya Marehemu Marilyn Monroe. Maisha 


yetu ya kila siku kwenye dunia hii ni kama Mshumaa, Ka nafasi ulikonako hapo ofisini 
kwako ni kama ka mshumaa, sehemu ya biashara uliyopo ni kama ka mshumaa, maisha yetu

 ya kila siku ni kama Mshumaa ambapo mishumaa hii inatufanya kuwa nuru, Mishumaa hii 

inatufanya kufahamika na kukubalika kutokana na mwanga tunaoutoa, njia tunayoionesha

yenye kuleta mafanikio.

Ingawa Kila mtu ana mshumaa wake kuna wengine wamekuwa na jitihada mwamwi 

(Mwanzo Mwisho) kuhakikisha mishumaa ya wengine inazima ili ibaki peke yao kutoa 

mwangaza na kuonekana wao ni bora kuliko wengine. Kumulika kwako wewe na kutoa

mwangaza na kung'aa kwenye maisha kuna wanyima usingizi wengine, kuna wakosesha raha

 wengine, ukiuliza hasa kama kuna sababu ya msingi wala hakuna sababu ila tu yeye 

hafurahii mafanikio wengine wanayopata hata kama nae ana mafanikio lakini unakuta

 anahitaji zaidi. Maisha yenyewe haya yetu ya kila siku Unafukuzana na hela ya Unga, 

Ukipata hela ya unga unagundua Chumvi imeisha, unakimbiza hela ya chumvi ukipata 

umegundua pampass zimeisha kila siku ni mbio mwamwi lakini ajabu from no where kuna

 mtu hapendi mafanikio yako.


Kwa kadri ambavyo tumekuwa tukiwaponda wengine kwa kile wanachokifanya basi vivyo


 hivyo na sisi tumekuwa tupondwa mahala pengine kwa kile tunachokifanya. Kuna watu 

hawapendi mafanikio yako live live ama kuna wale wa Silent Killers ukipata tatizo ama 

baya likikufika wanakutana wanagongeana mikono wanasema "Tulijua hafiki mbali" wewe 

ni Mkristo au Muislam wa wapi unayefurahia kushindwa kwa Mwanadamu Mwenzio. Wewe 

umekuwa Mtu wa Kushangilia kwa matatizo ama kukwama kwa wengine??maisha ni 

Mzunguko zamu yako itafika tu.




Kwenye maisha nimekutana na Watu ambao bila sababu wananichukia, inawezekana hata 


wewe umekutana na watu ambao wanachukia mafanikio yako bila sababu. Akipatikana mtu

 akamuuliza pengine hata pasipo kufahamu akamuuliza "Inaonekena Stella biashara

 zinamuendea pouwa sana ndo maana ameweza nunua gari", basi huyu anayekuchikia bila

 sababu utadhani ndo ana majibu yako yote atasema "aaah wapi unadhani hela yake,

 kahongwa lile gari, umalaya tu hakuna kitu anafanya mjini.." huyu mtu anaongea sana

 negatives kuhusu wengine. Kila anachoulizwa cha kwako yeye anaponda mbaya anaongea 

negatives mwanzo mwisho, kama ni kazi ofisini anakuongelea vibaya mpaka wengine 

wanashangaa, anatamani kuzima mshumaa wako ili wake ubaki unawaka raha yake wewe

 ufukuzwe kazi abaki yeye ndo aonekane bora,ukiwa na tabia hiyo kwisha habari yako.


Kuna watu wanachukia mafanikio ya wenzao bila hata sababu, furaha yao wao ni kuona


 wenzao wana huzuni siku zote, ukikutana nao wanakupa pole mpaka machozi yanawatoka

 kumbe mioyo yao ina kung'ong'a, anachukia kila hatua ya maendeleo yako. Kwanini kuzima

 Mshumaa wa mwenzio ili uonekane wako ndo unawaka??maisha hayako hivyo, unaweza

 ukamfanyi mtu leo ubaya ili uonekane wewe ndo boss, unataka uonekane wewe ndo Alfa

 and Omega, jua kitu Kimoja wewe sio Mungu wa Kumpangia Mtu maisha yake inawezekana

 hujui kuwa unatumika kumuandaa hiyo unayomfanyia huyo mtu kuwa na future nzuri. 

Kumpiga teke Chura ni Kumsaidia Kuruka. Kama tunajisikia raha kuumiza mioyo ya watu ili

sisi tuonekane bora kuliko wengine. Kuna Wakristo kabisa lakini ni wanafiki wakubwa 

kutwa kucha kutamani wenzao wakwame ili wao waonekane bora zaidi.


Kwenye maisha tunayoishi nasema tena kumpiga teke chura ni kumsaidia kuruka kuna 

wengine wala hawajui kuwa wanatumika kuwaimarisha wengine kwa maneno yao, leo

 ukinisema pembeni kwa watu inakusaidia nini, kama kuna mtu unajua hafanyi vizuri kuhusu

 kitu fulani kwanini usimwambie??Kuna watu wao ni Ma-Master of everything kama redio

 moja maarufu hapa nchini wao wanajua kila kitu kwenye vipindi vyao. Tunatamani

 wengine wachemshe ili unachokifanya wewe kionekane kuwa bora. Huu sio Ukristo wala

 sio Uislam hata ma Ma-Budha hawafanyi hivyo ni Upagani wa hali ya Juu. Inakusaidia nini

 kumsema mtu kuzima mshumaa wa mtu wakati unajua Mshumaa wako hautafika mbali.

 Usilewe Sifa kwa sifa unazozipata leo, leo watu wanakushangilia sababu una hela ama una

 kipawa kila sifa iko kwako, kuna siku vitaisha kuna siku atakuja bora kuliko wewe kama 

wenzako walivyoachwa ndivyo ambavyp utaachwa, niliwahi kuandika Usitukane Wakunga

 wakati Uzazi Ungalipo. Usijione bora kwa Mshahara unaoupata kwa kazi ya sasa maisha ni

 kupokezana ndugu yangu. Mungu sio Filikunjombe mwenzako itafika zamu yake. Wewe 

wadharau watu sababu wewe unajiona bora kuliko wao, roho mbaya haojawai kupanda bei

 tangu imeanza kutumika zaidi ya kushuka bei, tafuta wenye roho mbaya kama wewe 

ambao kwenye maisha wamekuwa wakitamani wengine wasitokelezee wabaki wao kama

 miungu watu kama waliwahi kufika mbali, ukizima mishumaa ya wengine jua tu na wako

 utazimwa tena ghafla mno saa usiyodhani, maana kabla ya wewe alikuwepo mwengine

kama wewe.



Ipo haja ya sisi kama Vijana, Watanzania na Wakristo Kusaidiana, kuna watu wana mawazo

 ya ajabu sana wanaonaga eti ukimpa "deal" fulani eti atatoka, unaogopa kumtoa mtu??

unataka utoke peke yako basi wewe sio Mungu ukigoma kutoa watu utashangaa wanakupita

 wewe bado umesimama pale pale. Biblia inasema wazi ni heri Kutoa kuliko Kupokea,

 haijakataza kupokea ila heri ipo kwenye kutoa, Unavyotaka watu Wakufanyie kwenye

 Maisha Wafanyie wewe wengine, kama unataka Kutolewa kwenye maisha ukatoka, basi

 kwanza anza kusaidia wengine kutoka leo. FM Academia wana Chorus inasema "Aliyekupa

 wewe ndiye kawanyima wao, dunia mafungu saba" kuwa makini.


Think differently and Make a Difference, kumbuka Muosha huoshwa, Kila aliye mwalimu leo

 aliwahi kuwa Mwanafunzi.



Papaa Ze Blogger.

0713 494110.