CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Papaa on Tuesday(PAPAA ON HONEYMOON)....Wewe ni sehemu ya maisha yangu (You're the part of ma life)

.....WARAKA TOKA HONEYMOON!!


Nikiwa bado niko honeymoon naomba leo nizungumze na wewe kuutambua Moyo wa Mwanamke.Ni wazi kua moyo wa mwanamke ni wa utofauti sana kuliko sisi tunavyomtazama napenda kuchukua nafasi hii kukufahamisha au kukutambulisha mwanamke aliyebeba kusudi lako,hatima yako,mwanamke aliyesababisha Mungu ashike damu kwa mara ya kwanza maana kuna sababu kubwa sana ya Mungu kumtoa mwanamke katika ubavu wa mwanaume kuna sababu kubwa sana ya Mungu kuruhusu damu kumwagika,Mungu sio katiri na wala hakufanya jambo la kinyama na wala hakutaka kumuumiza Adamu ila alikuwa na kusudi na malengo maalumu sana na jambo zuri sana kwa Adamu ndio maana alifanya yeye mwenyewe kazi hiyo ya upasuaji,maeneo mengine yote Mungu aliamuru watu wachinje wanyama na damu ifanye kazifulani na hata kwa Yesu aliruhusu apigwe na kuchomwa mkuki ili damu ifanye kazi lakini kwa Adamu aliingia mwenyewe hakuitaji mikono ya mtu ndio maana maandiko yanasema mke mwenye busara hutoka kwa Bwana'
 Hapa inatubidi kuliangalia kiundani sana kusudi la Mungu kumtoa mwanamke kwa mwanaume kwa kuusoma moyo wa mwanamke aliyebeba kusudi lako.Kwa nini mimi Samuel Sasali nili mpenda mke wangu kipenzi Milembe John Madaa,hakuna anayependa bila sababu na hakuna anayependwa bila sababu zinzomfanya,mtu kupenda au kutopenda hata Mungu alikuwa sababu za kuupenda ulimwengu hata kumtoa mwana wa pekeee ulimwenguni.Kupenda sio dhambi na kutopenda sio dhambi upendo ni sehemu ya maisha na ni Mungu ambaye ameweka kwa mwanadamu hivyo.
 LOVE imetoka kwa mungu sio mtu ameamua kupenda jua kuwa love ni sehemu ya maisha hata wanyama wanapenda na wana wivu wao kwa wao lakini love ya mwanadamu ni kubwa na inanguvu kuliko wanyama sababu nilizo nazo kwanini ninapenda na kwanini natakiwa kumpenda?
(a)Kwa sababu naitaji kufalijiwa (nafsi)
(b)Kwa sababu naitaji kukamilishwa (mwanz 2:18)
(c)Kwa sababu Upendo ni Asili
(d)Kwa sababu ni mpango wa Mungu
(e)Kwa sababu nahitaji kupendwa

 Love haijengwi kwa mali,pesa,watoto,uzuri,elimu,wadhifa wako,Uaskofu,Uchungaji,Utume,Udaktari.Upendo unajengwa kwa maneno matamu (palatable word) (sweet word) maneno yenye uwezo wa kukamata hisia ya mtu na kumfanya achilie maisha yake kwako yanatakiwa maneno yenye nguvu ya ushawishi na hata sex haijengi ndoa bali sex ni (thanksgiving) ni sadaka ya shukurani baada ya mambo muhimu kufanyika watu wengi wamedanganyika kuwa sex ndio upendo kitu ambacho sicho na ni afundisho potofu,vitu vinavyotengeneza upendo ni vidogo sana na vinadharauliwa sana kama busu,kukumbatia,mawasiliano na muda wa kutosha na mwenzi wako.
 Upendo unafanya mtu kujua kusudi la kuumbwa fulani kwa ajili ya mtu fulani,mwanadamu amegawanyika katika sehemu kuu tatu 1)Nafsi 2)Roho 3)Mwili kumbuka moyo unahitaji kufarijiwa,unahitaji kupendwa na unahitaji kuheshimiwa.

Papaa