CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

.....ACCEPT TO START ORDINARILY, BUT REMAIN FOCUSED TO YOUR FUTURE!!!!


OPT TO START FROM ZERO THEN ONE DAY YOU GONNA BE A HERO!!!

Hello friends,what's up?

I do hope you are doing well!

I have felt in my heart to share with you this very important IDEA!! And this is very important to all youth, young professionals and fresh from school experts and workers!!

If you get an employment post far from the city( i mean country side) with the company or organization that is operating almost the whole country and above...with a good title/starting profile even if with low salary, just take it rather than simple job with high salary in the city!

I say this because in remote areas/regions, you shall work there without pressure or stiff competition for many people never opt to go there; perhaps if you a Branch Assistant Manager obvious you can work as a manager when a manager is away....You can build experience which you wouldn't dare to have if you would have remained in Town as just a simple worker,you can buy assets and perhaps try to invest in agriculture, simply because life in regions is not that high as in towns..with such experience, working profile and good environment of learning the work, you can possibly and easily apply for the bigger post in city branches and may be headquarter whenever they air out opportunities....and actually you must be considered because you deserve it!! But in Town you work for more than 5 years without any promotion other than fearing to be fired any time!

It is very possible after two or five years to be the boss of your fellow professionals whom chooses to remain in Town after collage, when you opted to go in regions!

When you apply for job be very careful with the title no matter how much they want to pay you...for instance You start a job with a title Assistant Office Clerk be sure that it will take time for you to get accepted in any Managerial position in an organization...this is because you last experience hinder the trust of people over you...So you better start with big profile in a small enterprise/organization because with that CV you can work anywhere very accessibly.

N.B;
It is not my Idea that, you go to work in remote areas, so that you can be back in town, that is to say that, if environment allow you to invest and live where you are then that is great too...LIFE IS WHEREVER!!

So the choice is always yours...to start ordinarily in a place where no one have hope with you, but building base for future fame OR starting executive and remaining in that position for years!

WHEN YOU START WORKING, THE MOST IMPORTANT THING IS NOT SALARY, BUT WORKING EXPERIENCE AND BUILDING PROFILE; SO NEVER CHOOSE THE WORK BASING ON PACKAGE CRITERIA BUT A JOB WITH AMPLE ENVIRONMENT OF NATURING YOUR POTENTIAL!!!

......THIS IS JUST MY IDEA, YOU CAN APPLY IT OR COMPLY WITH IT!!!!
(C)Chavala


ZOOMING ZONE 0001....NA SAMWEL SASALI,THE BLOGGER!!!!


Salaam!!


Leo katika kipengele hiki natamani nimzungumzie kijana mmoja aitwaye



SAMWEL SASALI a.k.a PAPAA SEBENE,THE BLOGGER


(Natural African Activist Tanzanian patriot short funny loving caring brother, very God loving servant!!!)


Huyu ni lango katika nyumba ya Mzee Sasali na kwa ushuhuda na ukiri wake mwenyewe,yeye ni zawadi ya Mungu kwa familia hiyo na sadaka ya mama yake kwa Mungu!


Amebahatika kusoma Tanzania,sifa ya pekee ya kusoma kwake ni kusoma huku akifanya vitempo wakati wa likizo au wakati akisubiri kwenda hatua nyingine na Shahada yake ya kwanza ameipatia Chuo kikuu cha Mzumbe-Morogoro na hii ni Shahada ya Usimamizi wa Rasilimali watu(Bachelor Degree of Human Resource Management)



Amewahi kufanya kazi na halmashauri ya wilaya ya Ilala, Huwaei na sasa yuko na Benson Informatics Ltd kama HRM.


Samweli ni MC maarufu na anajimudu katika kazi yake, Preacher(Muhubiri/Mwalimu) wa neno la Mungu tangu kale, Thinker and Idea Developer

.........anafanya vitu vingi sana hapa mjini, na kilichofanya nimfahamu ni correllation ya mengi tunayofanya pamoja...nilikuwa namsikia tu but nilikutana nae face to face na kuzungumza nae mara ya kwanza mwaka 2007 pale MUFES kulikuwa na ibaada ya fundrising ya kununua vyombo vya muziki na yeye ndio alikuwa MC na mimi nilikuwa mgeni mualikwa tu.
...................................then urafiki na ukaribu ukaanza hapo hata leo na mpaka baadae sana!!


Samwel ni Blogger na anamiliki blog yake iitwayo
“samsasali.blogspot.com”
ambayo inafanya vema sana katika tasnia hii ya social medias, anapatikana pia facebook kwa saana na pia BBM 



Papaa ndio muanzilishi wa Mtandao wa marafiki uitwao MARAFIKI HURU....na mtandao huo baadae ukazaa maono mengine nayo ni mtoko wa marafiki wapendwa kila mwezi uitwao FRIENDS ON FRIDAY(FOF), ambao kwa sasa umeenea mpaka Mbeya,Arusha na kuna kila jitihada za kuanzisha Zanzibar


PAPAA amekuwa na experience nzuri sana ya publicity ya matukio mbalimbali hapa mjini,hivyo mafanikio ya matamasha au matukio kama LAUGH AGAIN CONCERTS; AFLEWO; CAMPUS NIGHTS; RIOTS; NA MENGINE MENGI yana mchango mkubwa sana wa huyu mkaka!.

Huyu kijana ni mzungumzaji mzuri(Motivational Speaker) na mwingi wa Idea kila kukicha, ana moyo wa kujitoa na kumsaidia kila afaaye kusaidiwa... zaidi ya yote huyu jamaa ni mwanaharakati wa kweli, maana akiamua kukomaa na issue huwa anajitosa tu hata kama inaonekana hatari mbeleni...alianza kufanya vibarua ili kujisomesha kabla haujaja huu mfumo wa mikopo ya serikali na amewahi kufanya utangazaji pale Praise Power na hivi sasa anajiandaa kuwa mbunge wa Mbinga!!




Namkubali sana,namuheshimu na najifunza vingi kutoka kwake!

Kila tukionana lazima nijichangamotishe kwa harakati zake, natamani sana vijana wa kitanzania tuuige mifano ya vijana wenzetu na hawa ndio wanapaswa kuwa Roll Model na sio hao wazungu na watu gani!!!


Ni bora niseme ukweli kwa yale yanipasayo kusema sasa,maana siku akifa haitafaa kitu kwake wala kwangu,itakuwa kama vile unatafuta kumfahamu!!


Siwezi kuandika hapa kila kitu but in summary, THE GUY IS MY HERO!!


“THINK DIFFERENTLY MAKE A DIFFERENCE”.....na huu ndio msemo wake wa moyo!!!


SISI NI MARAFIKI KWA HIYO TUNASAIDIANA, UKITAKA KUTHIBITISHA NJOO UMSEME VIBAYA KWANGU UONE KAMA UTAONDOKA MACHONI KWANGU SALAMA!!





NEVER HATE....APPRECIATE!!!!


+255-713-883 797(Andika kama una swali au maoni....unaweza tu ku-comment post hii kama ukiwa member wa blog hii,karibu sana)

(c)Zooming Zone'2012  
Haki zote zimehifadhiwa na Chavala,The King!!


....MPAKA IDEA HII ITAKAPOELEWEKA....


HARAKATI ZA KUKUZA VIPAJI HALISI HUSUSANI

VICHEKESHO VYA KIKRISTO ZINAENDELEA KUZAA

MATUNDA PAMOJA NA CHANGAMOTO ZILIZOPO!!!!

Salaam!

Ni muda sasa umepita tangu harakati za kutambulisha Christian comedy Tanzania zianze,matunda na matokeo mazuri yanaonekana japo bado hakijafikia kile kiwango ambacho kinapendeza mbele ya macho ya dunia. Ingawa bado ninaamini kuwa mwisho mwa mwaka huu 2012 tutakuwa tumepiga hatua ya maana.

Nimeweza kufikia mikoa mingi ya Tanzania japo kufanya kidogo utambulisho na kuangalia mazingira ya vipaji vya huko,mpaka leo ninaandika hapa imebaki mikoa minne tu ya Tanzania Bara,ambayo ni Ruvuma,Rukwa,Mara na Kagera na Pemba kwa Zanzibar ambapo bado sijafika, lakini naamini kabla Ya June 2013 nitakuwa nimefika kila sehemu ya Tanzania na kurudia tena kwingine!
Shauku yangu ni kuona watu hususani vijana wanaishi maisha yao mazuri,wakila matunda ya vipaji vyao,lakini pia jamii ikielimika na kuburudika kwa vipaji hivyo na si kukereka tu!

Kanisa linalo jukumu kubwa sana kuhakikisha vipaji na vipawa vinavyoibuliwa na kukuzwa kanisani haviendi kupata umaarufu duniani kwa mwavuli wa ulimwengu bali vibaki kuwa utukufu kwa Mungu kila vinapoonekana na kutambuliwa.....sio sifa kwa kanisa kumsikia msanii wa ulimwengu akisema mimi nilianzia kanisani kuimba kwaya au Sunday skuli,sasa unajiuliza kilichomkimbiza ni nini? Kwanini ameacha kuimba kwaya? Majibu yake yatakuwa rahisi tu.....HUKU NDIO KUNALIPA!!!!

Katika harakati zangu nimegundua mambo ambayo ni muhimu kusema wazi wazi kabisa, kanisa lina shida,tena shida kubwa na shida yenyewe inatokana na mambo kama haya;

a.    Vijana wengi hawajitambui wala kujielewa,sasa usipojielewa vema hauwezi kuwa na utulivu mzuri,utakuwa unatangatanga huku na kule ili mradi tu ubahatishe njia ya kutokea na ndio unajikuta watumishi wa Mungu wanahaha mpaka wanavamia pesa chafu!

b.    Viongozi wengi wa makanisa hawana dira na visomeo vya alama za nyakati,wengi wako na mitindo ya kizamani na hawawezi kukubali haraka,kulea wala kukuza vipaji vya vijana wa kisasa...na ukweli ni kwamba vijana wa leo wana namna yao ya kuwakilisha vipaji vyao.

c.    Kanisa halipendi kuwatia moyo kwa kulipia sawasawa thamani ya vipaji hivyo ili viendelee kukua kanisani, wengi huwabana vijana na kuwapa majukumu mengi,hata wakaacha mambo yao mengine lakini mwisho wa siku wanaambiwa ni huduma na hivyo wanaambulia hamna kitu....hivi uliwahi kuona wapi watu wanalipia kodi za nyumba zao na kula huduma?

d.  Wakristo wengi hawana uzalendo na vipaji vya nyumbani kwao,yaani vipaji vya makanisani; wengi wanapenda kazi za duniani zaidi na hata kama ni za dini basi ni zile za kutoka nje. Na wakristo ndio  wanaongoza kwa kudurufu au kuburn kazi za wasanii, hivi kama sisi wenyewe tusipowaunga mkono kwa kununua kazi halisi, ni nani atakayefanya hivyo?

e.    Na jambo lingine ni wale wasanii wenye majina makubwa kutowapa support ya kutosha wale wasanii wanaochipukia, wasanii wakubwa wamekuwa wakiwatisha makanisa machanga kwa kudai malipo makubwa kila wanapoitwa au kualikwa na wengine wamekuwa wakisemwa kwa tabia mbaya wanayoionyesha mbele ya jamii kama vile kiburi,majivuno,majigambo na uasherati/uzinzi.

NI MPAKA MATATIZO HAYA YATAKAPOPATIWA UFUMBUZI WA KUDUMU NDIPO FURAHA YA VIPAJI HALISI KANISANI INAKAPOKUZWA MARADUFU NA HII INAANZA NA KILA ALIYE MKRISTO...YAANI INAANZA NA WEWE!!!

Lakini bado nina imani kubwa kuwa tukiweka nguvu zetu za kutosha huko mambo yatakuwa mazuri tu! Kanisa lazima liiongoze nchi kwa kila kitu yaani kijamii,kisiasa,kiserikali,kiuchumi na kiroho.

Harakati bado zinaendelea na hazitakoma mpaka hapo nitakapoona Vipaji halisi vya Kikristo,hususani Ucheshi wa Kikristo unatambulika vilivyo.

Ninamshukuru Mungu sana kwani harakati hizi zimeibua vipaji vya maana na bado vingi vinakuja zaidi....yaani ninapoona kazi za Richard Chidundo; Gerald Mrema; Emmanuel Mathias Manu(MC pilipili); 1st Q dancers na wengine wengi hata wale ambao walikuwa kwenye secular na sasa wako huku kama vile Masanja Mkandamizaji,basi nafarijika sana na kutiwa moyo kuwa saa inakuja ambayo kila mkoa utajivunia vijana wenye vipaji katika maeneo yao huko.

Rai yangu ni moja tu....kila aliyeamua kumtumikia mungu kwa kipaji chake,basi na afanye hivyo kwa kumaanisha na kwa lengo la kuujenga ufalme wa Mungu na si vinginevyo....ubaya wala uchafu wowote usitajwe juu yako na ushirikiano na wenzako uzidi zaidi na zaidi,juu ya yote ujitahidi kujifunza kila siku ili ubunifu wako usipungue wala kuzoeleka.

Mungu wangu na awabariki,pamoja sana katika harakati hizi!!!

King Chavala
The great MC and Founder of Christian Standard and Stand Up Comedy in Tanzania

FRIENDS ON FRIDAY KUANZA MWAKA MPYA KWA EPISODE YA NYAMA CHOMA


BAADA YA KUFANYA VIZURI SANA KWA MWAKA MZIMA ULIOPITA, FRIENDS ON FRIDAY INAZIDI KUJA NA UBUNIFU MPYA KILA MARA NA SASA MTOKO WA IJUMAA HII NI WA NYAMA CHOMA, NATUMAI HUWEZI KUKOSA HII KAMA WEWE NI RAFIKI WA KWELI!!!

NJOO BASI MAHALI MARAFIKI WANAPOKUTANA NA KUBADILISHANA MAWAZO!!!