CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

JOHN LISU KUREKODI DVD YAKE LIVE TAR 06/10/2013 PALE CCC-UPANGA,DAR ES SALAAM!!



UKO HAPA DVD LIVE RECORDING
 NA JOHN LISSU,
06/10/2013,CCC-UPANGA, DAR ES SALAAM, TANZANIA.

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE;



SALAM Tanzania!
Shalom Dar es salaam, Shalom Tanzania!
Ndugu wanahabari na watanzania wote kwa ujumla!
Naamini tuko salama na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku alizotupatia Mungu wa mbinguni, tumshukuru Mungu sana kwa Amani na utulivu aliotupa na tuendelee kumuomba ili atuepushe na kila aina ya dhahama na uharibifu wa Yule adui!
Kama tulivyosikia hivi karibuni, yale yaliyotokea nchi jirani ya Kenya, kwa hakika tunawapa pole sana kwa mkasa huo, pole kwa wale waliowapoteza wapendwa wao na wale waliojeruhika tunawaombea wapone haraka, tunaamini hekima ya Mungu itakuwa juu ya serikali yao kushughulikia jambo hilo kikamilifu.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, hata sasa tunapoende kumalizia robo ya tatu ya mwaka 2013, tumeshuhudia mambo mengi sana mwaka huu ya kila aina, yapo yale yalionza kwa mara ya kwanza na mengine yamekuwa ni mwendelezo tu wa yale yadumuyo au yalioyaanza hapo kale, tumeshuhudia michezo mbalimbali na vipaji lukuki vikiinuka na kuimarika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, na kwa yote mema na mazuri tunampa Mungu Utukufu kwa hakika!

UTANGULIZI;
John Lisu ni mmoja wa waimbaji/Waabudishaji wanaoheshimika katika Tasnia ya muziki wa Injili kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza muziki wa Injili nchini Tanzania na nje ya Nchi. Nyimbo nyingi alizozitunga na kuziimba zimekuwa zikitumika katika makanisa mbalimbali kama nyimbo za kusifu na kuabudu; pia waimbaji wengine waliokua wakiimba naye wameweza kukua na kufikia uwezo wa kuwa waimbaji wa kujitegemea. John Lisu pia ametia hamasa kubwa miongoni wa wanamuziki wa Injili kuanza kufanya muziki wa live. John Lisu ameweza kufanya tours za ndani ya Tanzania, Africa na Bara la Ulaya kwa ajili ya huduma.
John Lisu anategemea kufanya Project II ya Live recoding inayojulikana kama "UKO HAPA" baada ya project ya kwanza ya Jehova yu hai kufanya vizuri sana. Tamasha litafanyika ndani ya ukumbi wa City Christian Centre (CCC) Upanga tarehe 6 Octoba 2013, kuanzia saa 8. mpaka saa 2 usiku. Tamasha litasindikizwa na waimbaji nguli kama Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Pastor Safari Paul, Bomby Johnson Waimbaji wote wamethibitisha kuwepo. 

VENUE:
City Christian Centre (CCC) mkabala na chuo kikuu cha mzumbe
Si mbali saana kutoka Diamond Jubilee
USAFIRI (basi zilizobandikwa matangazo ya tamasha) utakuwepo kutoka posta mpya kwenda ukumbini kuanzia saa saba na nusu mchana kwa bei ya kawaida.
HABARI NJEMA-MUHTSARI!!!!!

Sasa kwa mara pili nchini Tanzania, mwimbaji WA NYIMBO ZA INJILI na mwabuduji JOHN LISSU wa jijini Dar Es Salaam, atakuwa anafanya Ibaada kubwa ama Tamasha la kusifu la Kuabudu(LIVE PERFORMANCE), litakalorekodiwa moja kwa moja (DVD LIVE RECORDING) lenye jina “UKO HAPA” (Yaani Mungu na Uwepo wake).
Tamasha hilo litafanyika jumapili ya Tarehe 6, Octoba 2013  katika Ukumbi mkubwa wa kisasa wa Kanisa la City Christian Centre (CCC)- Upanga, mkabala na Chuo Kikuu Mzumbe – tawi la Dar es salaam, kuanzia saa nane mchana.
Tunataraji watu 5000 kuwa sehemu ya tamasha hili la kipekee,Utakuwa sehemu ya tamasha hilo kwa tiketi ya 10,000/= (kawaida), 20,000/= (VIP) na 3000/= (Watoto);
na Kwale watakaohitaji tisheti maalum za tukio hilo, basi zinapatikana kwa kati ya 12,000-15,000/=, wewe wasiliana tu na (0713905118)

VITUO VYA KUUZIA TIKETI;
1.   MWENGE – Tarakea duka la Kanda
2.   KINONDONI – DPC
3.   MLIMANICITY – Silverspoon Restaurant
4.   KARIAKOO – Mbogo Shop
5.   UKONGA BANANA – KWA GIDO
6.   POSTA - DUKA LA MSAMA

T-SHIRTS
-T-shirts maalumu kwa wanaume na wanawake zinapatikana katika vituo vya kuuzia tiketi kwa bei ya elfu kumi, mpaka elfu 15(kutegmeana na aina).

N.B; Kwa tiketi ya VIP, mnunuzi atajipatia na Audio CD ya John Lissu ya “Uko Hapa”

USAFIRI UTAKUWEPO!!
Siku ya tamasha kutakuwepo usafiri kutoka Posta Mpya mpaka CCC-Upanga,eneo la tukio, hivyo kama wewe ni mgeni na hupafahamu mahali hapo, basi utakachotakiwa kufanya ni kupanda magari toka ulipo mpaka posta mpya kabla ya saa nane,na hapo utayakuta mabasi yenye mabango ya Tamasha, basi utajongea humo na hapo utawezeshwa kufika eneo la tukio, muhimu ni kuzingatia muda!

MUHIMU SANA!!

Tamasha hili ni muhimu sana kwa Tanzania, hasa ukizingatia JOHN LISSU ni mmoja wa waimbaji wa kwanza kuimba live kila mahali anapoalikwa na ni mwimbaji wa kwanza binafsi kufanya LIVE DVD RECORDING pale Ubungo plaza, na ile ya kwanza iliitwa “JEHOVA YU HAI” na sasa anafanya LIVE RECORDING kwa viwango vingine bora zaidi, maana Mungu hutupa hatua moja zaidi kila siku.
Ni muhimu kwa kila mtanzania kujivunia kipaji na tukio hili muhimu katika historia, njoo umwabudu na kumsifu Mungu pamoja, Njoo ujifunze, Njoo umuunge mkono mtanzania mwenzako na njoo uje ufanyike sehemu ya Historia hii kwa Utukufu wa Jehova.

MWALIKO MAALUM;
Kipekee Ninapenda kuwakaribisha wachungaji, mitume, manabii, wainjilisti, waalimu na viongozi wote wa makanisa na huduma mbalimbali, ninawakaribisha viongozi wote wa kisiasa na kijamii kutoka serikalini na vyama vya siasa vyote, ninapenda kuwakaribisha wanaharakati na wanataaluma wote, ninapenda kuwakaribisha waimbaji wote wa nyimbo za injili na wanasanaa wote, ninapenda kuwakaribisa wanafamilia wote, asiwepo wa kubaki nyuma, ninapenda sasa kukukaribisha wewe unaesoma hapa, naam nisaidie kumkaribisha na mwenzako na yeye aje na mwenzake, kimsingi tukio hili ni letu wote bila kujali kitu chochote, njooni tumsifu na kumwabudu Bwana na Mungu hataacha kuibariki Tanzania!

SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Hakneel Production (Wadhamini wakuu), na Jonn Lissu na timu nzima ya maandalizi; Kanisa la CCC-Upanga; vyombo vya habari hususani Praise Power na WAPO Radio; Clouds TV kupitia CHOMOZA na Clouds Radio kupitia GT; Sibuka Tv kupita Gospel Hits; Bloggers hususani Christian Bloggers, magazeti na vyombo vingine vyote vya habari! Shukrani hizi zimfikie kila mtu mmoja mmoja aliyetoa mchango wa mawazo, fedha, ushauri, maombi, ubunifu, yaani mchango wowote wa hali na mali na Mungu awabariki nyote!

MUHTASARI MKUU;
Tukio; TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU, LITAKALOREKODIWA
(DVD LIVE RECORDING CONCERT)
Mhusika; JOHN LISSU
Jina: “UKO HAPA”
Mahali; UKUMBI WA KANISA LA CITY CHRISTIAN CENTRE (CCC)- UPANGA
Lini; 06TH OCTOBA, 2013
Muda; KUANZIA SAA NANE MCHANA
Kiingilio; Tsh 10,000/= (kawaida); 20,000/= (VIP) na 5000/= (Watoto)

Wasindikizaji; CHRISTINA SHUSHO, MIRIUM LUKINDO, PASTOR SAFARI, BOMBY JOHNSON, NEEMA GOSPEL CHOIR-AIC Chang’ombe na PAUL CLEMENT.

Mengineyo; USAFIRI UTAKUWEPO TOKA POSTA MPAKA CCC-UPANGA na Unaweza kujipatia Tisheti pia.
Wahusika; WATU WOTE MNAKARIBISHWA!


UKIPATA HABARI HII USIACHE KUMSHIRIKISHA NA MWENZAKO, NAAMINI HAUTAKOSA TUKIO HILI MUHIMU LA KIHISTORIA KATIKA NCHI YA TANZANIA KWA UTUKUFU WA MUNGU!!


PICHA NA TAARIFA


MAWASILIANO:
O713 240 397 – JOHN LISU
0713 905 118 –PROSPER MWAKITALIMA – EVENT MANAGER
0713 883 797 - FREDY CHAVALA - PUBLICITY


Imetolewa na;
Fredy E. Chavala <King Chavala (MC)>
Publicity Manager
+255 713 883 797
On Behalf of The Organizing Committee

John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha!!


John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha.
John Shabani

JOHN Shabani si jina geni masikioni mwa watu hasa wapenzi wa muziki wa injili na wanafunzi wa muziki huo.

John mzaliwa wa kijiji cha Kirando katika kitongoji cha Nyankima, kata ya sunuka, Wilaya ya Kigoma Vijijini, anatokea katika ukoo wa waumini wazuri wa dini ya kiislam.

Muimbaji huyo ambaye umaarufu wake uliwika baada ya kushiriki tamasha la pasaka ambalo anasem akuwa liliinua uimbaji wake na anatamani kama atapewa nafasi ya kushiriki tena kwa miaka ijao ikiwemo mwaka huu.

Anasema kuwa historia yake baada ya kumaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi kirando, alijiunga na elimu ya sekondari, lakini kutokana na itikadi za kidini, alijikuta akiwa katika wakati mgumu wa kupigwa vita na wazazi, kwasababu ya uamuzi wake wa kujiunga na Dini ya kikristo hali iliyomsababishia muimbaji huyo kuishi miaka mingi akiwa mbali na wazazi wake.

Mwaka 1992, John akiwa kijana mdogo, alipata ufadhili wa kwenda nchini Kongo ambako huko alijifunza muziki na kusoma Chuo cha Biblia na ndipo kipaji chake cha kutunga nyimbo na kuimba kilijitokeza kwa kasi.

Muimbaji huyo anasema kuwa hakutaka kuona mtu yeyote akiwa katika hali ya kukata tamaa, maana alifahamu madhara yake kwasababu hiyo, alianzisha vikundi mbalimbali vya vijana akiwa na lengo la kuwaelimisha ili kujikwamua katika hali ya kukata tamaa na kutokujihusisha na vitendo viovu kama vile madawa ya kulevya, Ukahaba na anasa za kila aina mambo ambayo aliyapiga vita.

Shabani anasema kuwa ameishi miaka mingi kama yatima, lakini hali hiyo imemsaidia kujifunza mengi na kuwa na tabia njema, kumheshimu na kumthamini kila mtu, hali hiyo ilimfanya kupata kibali machoni pa wengi.

Anasema kuwa amekuwa msaada kwa vijana wengi ndani na nje ya nchi na kuwakwamua waliokuwa wamekata tamaa na kujihusisha na vitendo viovu.Pia kutokana na ujuzi wa muziki alioupata na kipaji alichonacho cha kutunga, kuandika nyimbo na kuimba, anasema kuwa amekuwa msaada kwa waimbaji mbalimbali binafsi na vikundi , hasa nyimbo za Injili.

Mwaka 2001 John alifunga pingu za maisha na Debora Shabani na mwaka 2002 walifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwae Joyce, akiwa na maana ya kuyasahau maisha ya huzuni na shida na kujitabiria maisha ya furaha.

Mwaka 2004, John aliajiriwa katika kampuni ya Msama promotions ya jijini Dare es salaam, kampuni inayojihusisha na kuinua vipaji na pia kuwainua vijana na watu wa rika na jinsia zote waliokata tamaa ya maisha na hasa wale walioko vijiweni wakijihusisha na madawa ya kulevya, ukahabaa

Albamu yake ya kwanza Marufuku kukata tama anasema kuwa imewasaidia wengi waliokata tamaa na kuwapa matumaini mapya albamu hiyo na nyingine alioirekodi mwaka 2009 zilizoitwa huu ni wakati wangu na Moyo wangu.

John ametembelea nchi mbalimbali, akijifunza maisha ya watu ikiwemo kugundua kwamba karibu asilimia kubwa ya wanadamu, awe maskini, tajiri, msomi au asiye na elimu, wenye vyeo au waajiriwa, watoto kwa wakubwa, wanaume kwa wanawake, awe mzungu au mweusi n.k, wote kwa njia moja au nyingine wamepitia katika hali ya kukata tamaa au kukatishwa tamaa na jambo fulani, mtu, watu, hali au mazingira fulani.

Ndipo mwaka 2006, alipata maono na msukumo mkubwa wa kuandika Kitabu ambacho kitakuwa msaada kwa njia moja au nyingine kwa kila atakayekipata. Kitabu hicho kinaitwa Marufuku kukata tama. Kitabu hicho pamoja na kile kiitwacho “Mafanikio yatokanayo na kusifu na kumwabudu Mungu” vinategemea kukamilika baada ya miezi miwili.

Mwaka 208 sitausahau  ilikuwa ni siku ya huzuni na majonzi, siku ya kilio na kuomboleza. ni siku alipofariki mke wake mpendwa na mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili, Debora Shabani, mwimbaji aliyegusa mioyo ya watu wengi ndani na nje ya nchi, niliumia sana lakini sikukata tamaa”anasema.

Shabani alitunukiwa tuzo ya heshima pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake kwa ajili ya kuinua vipaji na pia kuchangia kuinua muziki wa Injili Afrika mashariki na kati. Pamoja na hayo amekua akianzisha vikundi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu Tuzo anayosema kuwa ilitolewa na kampuni ya Christian promoters Ltd, Pia ni miongoni mwa waanzilishi na kiongozi wa Chama cha muziki wa injili Tanzania (Chamuita).

Mwaka 2011, John alipata heshima kubwa kama mwalimu, kuongoza kundi la waimbaji (Tanzania gospel all stars) kuimba wimbo maalum wa miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.

Anasema kuwa pamoja na mzigo mkubwa aliokuwa nao kwa kidogo anachopata,amehakikisha kuwa anaisaidia jamii, hasa watu wenye ulemavu, wajane na yatima Vijana waishio katika mazingira magumu, pamoja na wakimbizi. Tayari ameanza mikakati ya kusajili Taasisi Hope Foundation kwa ajili ya maono hayo.

Pamoja na malengo mbalimbali aliyonbayo Shabani, lakini pia ni kuwa na kituo cha watoto na vijana, lengo ni kuandaa kizazi chenye maadili mema, kuibua, kutambua na kuinua vipaji vya watoto na vijana, mbinu na mikakati ya kuwakwamua watoto

Pia anasema kuwa mpango huo unalenga kutafuta ufadhili kwa ajili ya kuaendeleza vijana kielimu pamoja na kuwawezesha pale inapobidi, kuandaa matamasha ya watoto na vijana, kuunganisha watoto na vijana wengine duniani, kuwapa kipaumbele watoto na vijana wenye elemavu, kuwa na kiwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali ya watoto na vijan.

Kwa sasa anajishughulisha na kufundisha bendi,vikundi na waimbaji binafsi na kusema kuwa lengo ni Kufundisha kuimba au kunyoosha,Jinsi ya kuitumia sauti kuitunza na kuitawala,  Historia ya muziki na maadhi ya muziki, Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora, Matumizi ya kipaza sauti,Kuwatungia nyimbo au kurekebisha nyimbo zilizotungwa tayari, Kutoa ushauri kwa wanaotatarajia kuingia studio, mbinu za kuitangaza albamu au nyimbo zikubalike na Kutengeneza muziki wenye viwango.


Papaa On Tuesday...Hata Ukizima Mshumaa Wa Mwenzio Haufanyi Wako Uwake Zaidi

Ninakila Sababu Ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya siku ya Leo kwa Kuweza Kutupa tena Uzima katika Maisha haya tuliyo nayo. Kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu,kuna rafiki yangu Zulfa alitoka kwenda Matembezi ya Weekend amepata ajali wamekata Mguu sasa ni Kilema. Hata kama hakuna aliyekufa ama kuwa kilema kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu kwamba tunaishi.

Mwanamuziki Elton John akiwa na Bernie Taupin Mwaka 1973 waliuandika wimbo "Candle In The Wind" ukiwa maalum kwa ajili ya heshima ya Marehemu Marilyn Monroe. Maisha 


yetu ya kila siku kwenye dunia hii ni kama Mshumaa, Ka nafasi ulikonako hapo ofisini 
kwako ni kama ka mshumaa, sehemu ya biashara uliyopo ni kama ka mshumaa, maisha yetu

 ya kila siku ni kama Mshumaa ambapo mishumaa hii inatufanya kuwa nuru, Mishumaa hii 

inatufanya kufahamika na kukubalika kutokana na mwanga tunaoutoa, njia tunayoionesha

yenye kuleta mafanikio.

Ingawa Kila mtu ana mshumaa wake kuna wengine wamekuwa na jitihada mwamwi 

(Mwanzo Mwisho) kuhakikisha mishumaa ya wengine inazima ili ibaki peke yao kutoa 

mwangaza na kuonekana wao ni bora kuliko wengine. Kumulika kwako wewe na kutoa

mwangaza na kung'aa kwenye maisha kuna wanyima usingizi wengine, kuna wakosesha raha

 wengine, ukiuliza hasa kama kuna sababu ya msingi wala hakuna sababu ila tu yeye 

hafurahii mafanikio wengine wanayopata hata kama nae ana mafanikio lakini unakuta

 anahitaji zaidi. Maisha yenyewe haya yetu ya kila siku Unafukuzana na hela ya Unga, 

Ukipata hela ya unga unagundua Chumvi imeisha, unakimbiza hela ya chumvi ukipata 

umegundua pampass zimeisha kila siku ni mbio mwamwi lakini ajabu from no where kuna

 mtu hapendi mafanikio yako.


Kwa kadri ambavyo tumekuwa tukiwaponda wengine kwa kile wanachokifanya basi vivyo


 hivyo na sisi tumekuwa tupondwa mahala pengine kwa kile tunachokifanya. Kuna watu 

hawapendi mafanikio yako live live ama kuna wale wa Silent Killers ukipata tatizo ama 

baya likikufika wanakutana wanagongeana mikono wanasema "Tulijua hafiki mbali" wewe 

ni Mkristo au Muislam wa wapi unayefurahia kushindwa kwa Mwanadamu Mwenzio. Wewe 

umekuwa Mtu wa Kushangilia kwa matatizo ama kukwama kwa wengine??maisha ni 

Mzunguko zamu yako itafika tu.




Kwenye maisha nimekutana na Watu ambao bila sababu wananichukia, inawezekana hata 


wewe umekutana na watu ambao wanachukia mafanikio yako bila sababu. Akipatikana mtu

 akamuuliza pengine hata pasipo kufahamu akamuuliza "Inaonekena Stella biashara

 zinamuendea pouwa sana ndo maana ameweza nunua gari", basi huyu anayekuchikia bila

 sababu utadhani ndo ana majibu yako yote atasema "aaah wapi unadhani hela yake,

 kahongwa lile gari, umalaya tu hakuna kitu anafanya mjini.." huyu mtu anaongea sana

 negatives kuhusu wengine. Kila anachoulizwa cha kwako yeye anaponda mbaya anaongea 

negatives mwanzo mwisho, kama ni kazi ofisini anakuongelea vibaya mpaka wengine 

wanashangaa, anatamani kuzima mshumaa wako ili wake ubaki unawaka raha yake wewe

 ufukuzwe kazi abaki yeye ndo aonekane bora,ukiwa na tabia hiyo kwisha habari yako.


Kuna watu wanachukia mafanikio ya wenzao bila hata sababu, furaha yao wao ni kuona


 wenzao wana huzuni siku zote, ukikutana nao wanakupa pole mpaka machozi yanawatoka

 kumbe mioyo yao ina kung'ong'a, anachukia kila hatua ya maendeleo yako. Kwanini kuzima

 Mshumaa wa mwenzio ili uonekane wako ndo unawaka??maisha hayako hivyo, unaweza

 ukamfanyi mtu leo ubaya ili uonekane wewe ndo boss, unataka uonekane wewe ndo Alfa

 and Omega, jua kitu Kimoja wewe sio Mungu wa Kumpangia Mtu maisha yake inawezekana

 hujui kuwa unatumika kumuandaa hiyo unayomfanyia huyo mtu kuwa na future nzuri. 

Kumpiga teke Chura ni Kumsaidia Kuruka. Kama tunajisikia raha kuumiza mioyo ya watu ili

sisi tuonekane bora kuliko wengine. Kuna Wakristo kabisa lakini ni wanafiki wakubwa 

kutwa kucha kutamani wenzao wakwame ili wao waonekane bora zaidi.


Kwenye maisha tunayoishi nasema tena kumpiga teke chura ni kumsaidia kuruka kuna 

wengine wala hawajui kuwa wanatumika kuwaimarisha wengine kwa maneno yao, leo

 ukinisema pembeni kwa watu inakusaidia nini, kama kuna mtu unajua hafanyi vizuri kuhusu

 kitu fulani kwanini usimwambie??Kuna watu wao ni Ma-Master of everything kama redio

 moja maarufu hapa nchini wao wanajua kila kitu kwenye vipindi vyao. Tunatamani

 wengine wachemshe ili unachokifanya wewe kionekane kuwa bora. Huu sio Ukristo wala

 sio Uislam hata ma Ma-Budha hawafanyi hivyo ni Upagani wa hali ya Juu. Inakusaidia nini

 kumsema mtu kuzima mshumaa wa mtu wakati unajua Mshumaa wako hautafika mbali.

 Usilewe Sifa kwa sifa unazozipata leo, leo watu wanakushangilia sababu una hela ama una

 kipawa kila sifa iko kwako, kuna siku vitaisha kuna siku atakuja bora kuliko wewe kama 

wenzako walivyoachwa ndivyo ambavyp utaachwa, niliwahi kuandika Usitukane Wakunga

 wakati Uzazi Ungalipo. Usijione bora kwa Mshahara unaoupata kwa kazi ya sasa maisha ni

 kupokezana ndugu yangu. Mungu sio Filikunjombe mwenzako itafika zamu yake. Wewe 

wadharau watu sababu wewe unajiona bora kuliko wao, roho mbaya haojawai kupanda bei

 tangu imeanza kutumika zaidi ya kushuka bei, tafuta wenye roho mbaya kama wewe 

ambao kwenye maisha wamekuwa wakitamani wengine wasitokelezee wabaki wao kama

 miungu watu kama waliwahi kufika mbali, ukizima mishumaa ya wengine jua tu na wako

 utazimwa tena ghafla mno saa usiyodhani, maana kabla ya wewe alikuwepo mwengine

kama wewe.



Ipo haja ya sisi kama Vijana, Watanzania na Wakristo Kusaidiana, kuna watu wana mawazo

 ya ajabu sana wanaonaga eti ukimpa "deal" fulani eti atatoka, unaogopa kumtoa mtu??

unataka utoke peke yako basi wewe sio Mungu ukigoma kutoa watu utashangaa wanakupita

 wewe bado umesimama pale pale. Biblia inasema wazi ni heri Kutoa kuliko Kupokea,

 haijakataza kupokea ila heri ipo kwenye kutoa, Unavyotaka watu Wakufanyie kwenye

 Maisha Wafanyie wewe wengine, kama unataka Kutolewa kwenye maisha ukatoka, basi

 kwanza anza kusaidia wengine kutoka leo. FM Academia wana Chorus inasema "Aliyekupa

 wewe ndiye kawanyima wao, dunia mafungu saba" kuwa makini.


Think differently and Make a Difference, kumbuka Muosha huoshwa, Kila aliye mwalimu leo

 aliwahi kuwa Mwanafunzi.



Papaa Ze Blogger.

0713 494110.

SHUJAA WA KIDATOORGA ALIYEUA SIMBA!!!

 UKIMUONA UNAWEZA USIAMINI, LAKINI HUO NDIO UKWELI NA NILIMKUTA HUKO HYDOM, NILIVYOENDA SOME WEEKS BACK!
 NA HAWA NI WALIMBWENDE WANAOMPAMBA NA KUMHUDUMIA KWA HESHIMA HIYO!
YAANI MPAKA RAHA, NYUMBA NI YA ASILI, KILA KITU HUMO NI ASILI NA HATA HAWA WALIMBWENDE WAMEVALIA KIASILI!

HII SIO MOVIE NI MAISHA HALISI....NITARUDI KUONGEA KWA KINA KUHUSU UTAMADUNI HUO WA KIPEKEE AFRIKA!!

Le African Adventures!

Papaa On Tuesday......Mwanga Wa Mbalamwezi Haukaushi Muhogo!!


Nimatumaini yangu ya kuwa wote tu wazima na tunaendelea vema na shughuli zetu za kile siku.

Katika kabila letu la Wanyasa, chakula cha asili cha kikabila ni ugali wa muhogo pamoja na dagaa kutoka Ziwa Nyasa. Kwa mnyasa kupata chakula cha namna hii basi unakuwa umemfikisha nyumbani kabisa kuliko kumpa chipsi mayai au kitimoto na ndizi. Nilipokuwa kijijini wakai fulani niliona jinsi mihogo inavyokaushwa, akina mama wa Kinyasa watajihimu asubuhi kuimenya mihogo hiyo na kuiloweka kwa muda kisha kuwekwa juani ili iweze kufaa baadae kwa kutwangwa kisha kupatikana unga wa muhogo wenye kupikwa ugali hupatikana. Kuna familia zingine ukifika wakati wa jioni huanua mihogo hiyo kwa kuiweka ndani kuhofia isiharibiwe na wanyama ama hata kuibiwa pia maana ndo deal kwa familia zilizokuwa zinaaminika kwa uchawi walikuwa wanaacha tu anayeiba yatamkuta ya kumkuta. Siku moja nikamuuliza Marehemu Babu yangu "Kwanini Wengine wanatoa Mihogo kuingiza ndani"?akaniambia kule kijijini kuna msemo wanautumia "mwanga wa mbalamwezi haukaushi muhogo". Nilitamani kufahamu maana ya msemo huo wenye kubeba maana kubwa sana nyuma yake.

Kuna mambo ambayo kwenye maisha huwezi yabadili ni kama kutaka kulazimishia mwanga wa mbalamwezi ukaushe mihogo, mihogo yake ni jua. Kuna watu wana tabia ya kulazimishia kufanya mambo wasiyo na uwezo nayo. Yaani unataka kufanya mambo ili watu wakukubali kuwa wewe mambo safi, unataka watu wakuone na wewe uko juu una Samsang Galaxy wakati matumuzi yako ni kupiga simu na kutuma SMS, unapiga picha event moja kesho una delete picha hizo hizo kuweka event ya pili. Kwenye vikao vya harusi walizojaa marafiki zako unatoa ahadi kubwa kubwa za harusi uonekane na wewe mambo safi. Kuna mambo ya mbalamwezi kuna mambo lake jua ndo yanaenda.
Kwanini unataka uishi zaidi ya vile ya ulivyo, kwanini unaishi maisha ya kujitahidi??kwanini usiishi vile ulivyo kwani unapoteza nini unapokuwa unaishi maisha yako ya kawaida. Hii tabia ya kutembelea kwa watu kishaukakuta wenzio wana flat screens na wewe ukataka, ukakuta wana Sub Woofers za Ukweli mwisho wa siku na wewe ukataka, Ukaenda kwa watu ukakuta wana Kengere na wewe ukataka, ukakuta mtu ana BlackBerry na wewe unajinyimaaaaaaaaaaaaaa eti na wewe uonekane upo kwenye Class kama uwezo wako ni kutoa mwanga basi usitake kukausha mihogo kuna mambo hayawezekani kwa sasa wala baadaae kwanini uyalazimishie?

Kizazi chetu kimekuwa na changamoto sana eneo mojawapo lenye kuleta changamoto ni kuoa na kuolewa. Unakuta saa nyingine kuna watu wanawafukuzia watu mpaka wanakera, na siku hizi wanawake wenye uwezo wamekuwa ni sababu ya kunyang'anya wanaume wa wanawake wasio kuwa na uwezo na wanaume wenye tamaa wamejikuta wakidondokea kwenye mikono ya wanawake mabaradhuri. Fedha ina ushawishi, fedha inatakatisha, fedha ni jawabu la mambo yote sababu ya uwezo wa mwanamke kuweza kumudu kununua mambo yanayoweza mfanya mwanaume aonekane nae katika jamii wamejikuta wakiacha mapenzi ya kweli na kuingia kwenye tamaa, kuna rafiki yangu amehongwa gari, gari kabisaaa lakini jamaa hana uhuru kabisa, kuna rafiki yangu amehongwa chain ya 1.5 Milioni na Blackberry juu lakini anafungwa kupita mbwa wa kizungu, inakufaidia nini kupata kila kitu na huku unapoteza mpaka uhuru wako wa kucheka, unayemcheka fulani unaulizwa, unapomtazama mtu mara mbili unaulizwa why?ni mara kumi kuwa na simu ya kitochi na kubaki na mapenzi ya kweli. Kuna wanawake na wanaume wako tayari kufanya chochote wanachoweza kutimiza tamaa zao za mwili, unaweza kupewa nyumba bure, unaweza kupata gari bure, unaweza kupewa investment bure lakini huwezi kupata amani ya kweli na uhuru wa kweli for free, kama unajua uwezo wako kutoa mwanga usitake kukausha mihogo.

Heshima ni kitu cha bure sana, lakini nani anataka kutunza heshima yake, rafiki yangu aliwahi niambia "Papaa tangu nimeanza kutunza heshima haijawahi nisaidia". Kwani unataka utunze heshima ili iukusaidie?kuwa na heshima ni msaada mkubwa sana kwenye maisha, kujiheshimu, kuheshimiwa, kushemiana ni jambo ambalo naona sasa linapoteza mkondo wake watu wanakuambia its a matter of time itashuka leo kesho watu wanasahau, leo unafanya jambo la kusikitisha jamii lakini kesho heshima inarudi mjini, katika kila uovu kuna mtu wa kukutia moyo. Mwenye mbili havai moja, na mwanga wa mbalamwezi hata siku moja hauwezi kausha mihogo, lina heshima yako ili uheshimiwe.

Kufikiria kutumia mwili wako kupata kazi, kufikiria kutumia mwili wako kupata gari ama nyumba basi jiandae tena kutumia mwili wako kupanda cheo, jiandae mwili wako kupata nafasi ya kwenda kusoma, jiandae kutumia mwili wako ili usipunguzwe kazini, jiandae kutumia mwili wako kupata hela ya mafuta, jiandae kutumia mwili wako kufanya service ya gari, jiandae kufanya chochote kutumia mlango ulioufungua kwenye maisha yako, kama unajua wewe ni mbalamwezi usitamani kazi za jua kila jambo lina makusudi yake hapa duniani.

Kila mtu atavuna alichopanda haijalishi unapanda hadharani ama gizani, mchana jua humulika na usiku mbala mwezi hutoa mwanga. Mwanga wa mbalamwezi haukaushi muhogo.

Think differently and make a difference 

....//Papaa
0713 494110