CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

MWISHO WA SEPTEMBER NDIO MWISHO WA KUTOA MICHANGO KWA SAMUEL SASALI!!!

Hello habari zenu!
Natumai nyote mko vizuri mnaposoma habari hii!!
Naamini habari ya habari za Useja wa Papaa ziliwasikitisha sana na mlitamani mseme ila hamkuweza, naam maombi yenu Mungu akajibu na akampata Mchumba, ndio ni mchumba mkubwa tu wa kutosha Kitanda ,dressing table na kabati na bado sehemu ya kutembea inabaki.
Mlipozidisha maombi macho yake yakafungukia paleeeeee HKMU Mikocheni, naamini wengi habari ziliwafikia na hata kwasababu ya ufukunyuku wengine mkajua hata kabla yeye mwenyewe hajajua.

Alifuata taratibu zote za kijamii na kifamilia,Mali akalipa (Kama anadaiwa atamalizia mwenyewe) na shughuli za kuthibitisha kuwa yuko serious zilifanyika nyumbani kwa binti na baadae kanisani kwa kumvisha pete ya thamani sana, ndio kwasababu anampenda sana.

Ahsante kwa kushiriki hayo yoooote yaliyopita kwa maneno na simulizi......sasa ni wakati wako wa kushiriki kikamilifu tena kwa hali na mali.
 
Tarehe ya Harusi imeshatangazwa, 26th October 2013 pale Victory Christian Centre Tabernacle (VCCT) pale Mbezi beach A kwa Dr.Huruma Nkone na baadae taafrija kufanyika katika bustani kubwa ya pale Lamada Hotel,Ilala-boma saa moja mpaka tano usiku.

Yawezekana wewe ni rafiki,jirani,shabiki,msomaji wa blog, ndugu, mwanahabari mwenzie, labda mnoni mwenzie au mtoto wa mchungaji mwenzie au unasali pamoja nae,au mmewahi kupiga picha pamoja au umewahi kumwona na kumfurahia hata mara moja tu au basi ni rafiki yako katika mitandao ya kijamii au humjui kabisa ndio unamjua leo....ni sawa tu anaitwa Samwel Sasali,Papaa,The Blogger....basi hii ni nafasi yako kushiriki shangwe hii sambamba na marafiki wote wa muhimu hapa mjini kama vile Wachungaji,Wafanyabiashara,Wanasiasa,waimbaji,wanafunzi na wengine kadha wa kadha bila kumsahau Askofu Mkuu wa TAG,Dr Barnabas Mtokambali na burudani live itaendeshwa na John Lissu na bendi yake.

Nafasi ni chache sana ukilinganisha na Uwingi wa matafiki wa kijana huyu, hivyo nakushauri uchukue kadi yako mapema na uchangie kabla ya Septemba 30, maana baada ya hapo hata kama utakuwa na hela nyingi mkononi utakosa kadi.

Naomba kusisitiza tena na tena kama rafiki, kama pacha wake na kama mwanakamati kuwa NI MUHIMU KUSHIRIKIANA NA MWENZETU, NI MUHIMU KUCHANGIA LAKINI KWA SABABU YA UWINGI WA MARAFIKI UKILINGANISHA NA IDADI TUNAYOITAKA,NAAMINI UTAZINGATIA KUCHANGIA MAPEMA NA KUPATA KADI YAKO.

Kadi zinapatikana kwa Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi,Bwana Noell Tenga, Bwana Harusi Mtarajiwa, Samuel Sasali, Renee Lyatuu,James Temu(Uncle jimmy) na Kwa King Chavala.

Hata kama siku hiyo haufikiri kuwepo harusini,haitakuwa vibaya kama ukichangia japo 50,000/=na kuendelea kwa kadri Mungu alivyokubariki.
Kwa Bloggers na wanahabari msiache kunitafuta maana nina kadi zenu!!

KUMBUKA;
Ni hao tu niliowataja ndio watakupa kadi na sio mwingeyo, Tunatamani chango wako usiwe chini ya 50,000 ili tuweze kufanikisha shughuli ya mwenzetu!!

Kwa Mawasiliano zaidi;
Samuel Sasali 0713 494110/0686 255 269
Happy Lwendo; 0717 149085
Noell Tanga; 0713 261425

IMETOLEWA NA KING CHAVALA KWA NIABA YA KAMATI NA CHINI YA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.

ZOOMING ZONE 0004.......Na PROSPER A. MWAKITALIMA, The T-shirt Printer tycoon!!!



HELLO HABARI!
NAAMINI MKO POA NA MNAENDELEA VIZURI, NILIKUWA KIMYA KWA MUDA NA HII NI KWASABABU ZOOMING ZONE SIO MAKALA YA KILA SIKU AMA KILA MTU, HIVYO LEO LENZI IMEMULIKA KIJANA MMOJA HAPA MJINI NA HUYU NDIO ATAKUWA……Zooming Zone 004
************************************************************************************               
Zooming Zone 0004....Na Prosper A.Mwakitalima
Huyu sio mwingine basi ni kijana mjasiriamali “SWAHIBA” anayetamba na kujulikana sana kwa KUCHAPISHA T-SHRTS vizuri, nzuri na zenye maneno mazuri hapa Mjini, Tanzania.
Naam pia ndio huyu ambaye habari zake zilivuma sana hapa mjini kwa kupona“kufufuka” toka katika ajali mbaya sana sana pale maeneo ya River side Ubungo  23/11/2011 iliyohusisha lori la mafuta na gari yake ndogo,ajali ambayo ilichukua maisha ya watu kadhaa akiwemo mama mmoja mjamzito ambaye alikatika kichwa(ilitisha sana kwa kweli)….lakini Jambo la kushangaza ni kuwa kijana huyu alipona kabisa maana hakuvunjika mfupa wala mshipa Zaidi ya michubuko kadhaa tu,hakuna aliyeamini hata leo lakini huo ndio ukweli!
Huwezi kuamini lakini huu ndio ukweli!

Huyu pia ni mmoja wa washika dau na wawezeshaji wa Mtoko wa marafiki Mjini uitwao “FRIENDS ON FRIDAY (FoF)”, na ndio mbeba maono na mkurugenzi wa “SIFA TANZANIA”Mfululizo wa matamasha ya kumwinua Yesu hapa nchini Tanzania.
Huyu ni PROSPER ALFRED MWAKITALIMA a.k.a SWAHIBA a.k.a “The Next Billionaire” (King Chavala tu anaruhusiwa kumwita “MY PS”)
 
Prosper,Wambura na Chavala Singida
NILIBAHATIKA KUFANYA NAE MAHOJIANO HIVI KARIBUNI KWA KINA NA NIKAPATA MENGI SANA NA HAYA NI MACHACHE KATIKA MENGI, AMBAYO NAAMINI YANAWEZA KUKUSAIDIA KUMFAHAMU VIZURI NA YAMKINI KUJIFUNZA MENGI KUTOKA KWAKE, HUYU NI KIJANA WA KIPEKEE AMBAYE NI MFANO WA KUIGWA NA VIJANA WA KITANZANIA…..FUATANA NAMI KATIKA MAELEZO YANGU KUHUSU