CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

#...NI MARUFUKU!!#(04)......KUFANYA MAREKEBISO JUU YA JAMBO LA KUAZIMA BILA RUHUSA!!!!

#.....NI MARUFUKU KABISAAAA#
Ni marufuku kabisaa kufanya mambo au marekebisho au matengenezo usiyoruhusiwa juu ya kitu au jambo la kuazima bila ruhusa ya mwenyewe!
Kwa kawaida kitu cha kuazima hakina uhuru wa kutosha,kwani umepewa kwa kipimo....waswahili wanasema...."Nguo ya kuazima haisitiri Matako"
Kuna mambo mengi tunajiamulia wenyewe juu ya vitu vya kuazima na kwa kweli huwa inakuwa sio sawa,kwa mfano;

a)Mtu anakuazima simu yako aongee na mtu mara moja maana yake imeisha airtime ambayo nayo alikopa na hapo mlipo hamna access ya kununua....sasa unakuta mtu baada ya kupiga kwanza anaanza *102#....hivi hicho ndio umeomba au? na haishii hapo unakuta ameongea na simu zaidi ya hata alivyoomba yaani unakuta mtu kajiachia kama yake vile na bado credit ikiisha na kwako eti anakopa na anapiga tena mpaka na hiyo inaisha na hapo hajakwambia kitu...sasa wewe unashangaa ukitaka kupiga yule mrembo anakwambia....hauna salio la kutosha kupiga simu...basi unanunua vocha faster....unashangaa message.....Ahsante kwa kulipa deni.....na bado unadaiwa ......ahhhh dah sasa ndio nini hivi?
Hapo ulipokuwa umemuachia basi kapiga picha,kafungua na picha zako na mpaka bundle yako ya internet imeisha eti kisa anadownload miziki...Sasa wenye tabia hiyo nawaambia Marufuku,acheni kuwakwaza wenzenu,mimi tabia ya hata tu kuazimana simu wala sioni kama ina mashiko sana kipindi hiki ambako simu ziko tele na mawasiliano ni rahisi kwa yeyote!!!.....Umewezaje kununua simu na unashundwa kununua vocha??

b)Mtu anakuazima gari na unampa kwa roho safi tu,halafu anakwaruzana huko na kikimbiza gari gereji mchwara huko wanaanza kukuharibia gari hali angekwambia wewe una fundi wako unayemwamini,sasa anafanya hayo yote na hasemi,wewe ukija kushtuka siku moja unakuta some spears kwenye gari hazipo....ama mtu anakwenda huko halafu anakutana na stickers basi ananunua na kubandika kwa gari yako....hivi umeazima gari yangu ukanipambie au utumie na kuirudisha,tena mbaya zaidi eti mtu anakuwekea masticker ya kipepo kabisa na yeye anafurahia...sijui Majani,Kappa au Monster Power...jamani Ni Marufuku kabisaaa,ukiazima kitu kirudishe hivyo hivyo na usijifanye wewe ndio mwenyejiiiiiiiii

c)Mtu amekuja kwako kukutembelea may be anakaa wiki moja au siku kadhaa,kwa kuwa ni mgeni hapa ni nyumbani pa kuazima...sasa unakuta mtu anaanza kupanga na kupangalua mara kochi hili ageuzie kule,pambo hili aweke kule yaani wewe ukitoka kwa mishe mishe unakuta everything has changed,jamani hapa kwako? hata kama umetamani kunisaidia kwanini usiniulize? unajua kuna saa mnavuruga mahusiano ya watu hivi hivi,yaani mwenyewe mlimbwende amepanga na kupamba na umekubali for sake of love halafu huyu mfukunyuku anakuja na kuharibu kisha anaondoka,unafikiri akija huyo mlimbwende siku moja unamwambiaje kama sio dharau hiyo!!!!

Ipo mifano mingi sana,lakini nimesema marufuku tena marufuku kabisa!!
HESHIMU MIPAKA YA CHOCHOTE UNACHOPEWA,SIO UNAKARIBISHWA SEBULENI WEWE UNAENDA MPAKA CHUMBANI AAAAH!!
......Sema neno na wewe kama tumeelewana!!!

N.B;Hii ni kwa faida ya mahusiano na urafiki wa ko na watu,na hii inawahusu watu wenye akili timamu tu na wanaojielewa na kujitambua!!

@Kwa hisani kubwa ya Chavala Ideas Platform <http://chavalamedia.blogspot.com/>
(c)2013