CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha!!


John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha.
John Shabani

JOHN Shabani si jina geni masikioni mwa watu hasa wapenzi wa muziki wa injili na wanafunzi wa muziki huo.

John mzaliwa wa kijiji cha Kirando katika kitongoji cha Nyankima, kata ya sunuka, Wilaya ya Kigoma Vijijini, anatokea katika ukoo wa waumini wazuri wa dini ya kiislam.

Muimbaji huyo ambaye umaarufu wake uliwika baada ya kushiriki tamasha la pasaka ambalo anasem akuwa liliinua uimbaji wake na anatamani kama atapewa nafasi ya kushiriki tena kwa miaka ijao ikiwemo mwaka huu.

Anasema kuwa historia yake baada ya kumaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi kirando, alijiunga na elimu ya sekondari, lakini kutokana na itikadi za kidini, alijikuta akiwa katika wakati mgumu wa kupigwa vita na wazazi, kwasababu ya uamuzi wake wa kujiunga na Dini ya kikristo hali iliyomsababishia muimbaji huyo kuishi miaka mingi akiwa mbali na wazazi wake.

Mwaka 1992, John akiwa kijana mdogo, alipata ufadhili wa kwenda nchini Kongo ambako huko alijifunza muziki na kusoma Chuo cha Biblia na ndipo kipaji chake cha kutunga nyimbo na kuimba kilijitokeza kwa kasi.

Muimbaji huyo anasema kuwa hakutaka kuona mtu yeyote akiwa katika hali ya kukata tamaa, maana alifahamu madhara yake kwasababu hiyo, alianzisha vikundi mbalimbali vya vijana akiwa na lengo la kuwaelimisha ili kujikwamua katika hali ya kukata tamaa na kutokujihusisha na vitendo viovu kama vile madawa ya kulevya, Ukahaba na anasa za kila aina mambo ambayo aliyapiga vita.

Shabani anasema kuwa ameishi miaka mingi kama yatima, lakini hali hiyo imemsaidia kujifunza mengi na kuwa na tabia njema, kumheshimu na kumthamini kila mtu, hali hiyo ilimfanya kupata kibali machoni pa wengi.

Anasema kuwa amekuwa msaada kwa vijana wengi ndani na nje ya nchi na kuwakwamua waliokuwa wamekata tamaa na kujihusisha na vitendo viovu.Pia kutokana na ujuzi wa muziki alioupata na kipaji alichonacho cha kutunga, kuandika nyimbo na kuimba, anasema kuwa amekuwa msaada kwa waimbaji mbalimbali binafsi na vikundi , hasa nyimbo za Injili.

Mwaka 2001 John alifunga pingu za maisha na Debora Shabani na mwaka 2002 walifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwae Joyce, akiwa na maana ya kuyasahau maisha ya huzuni na shida na kujitabiria maisha ya furaha.

Mwaka 2004, John aliajiriwa katika kampuni ya Msama promotions ya jijini Dare es salaam, kampuni inayojihusisha na kuinua vipaji na pia kuwainua vijana na watu wa rika na jinsia zote waliokata tamaa ya maisha na hasa wale walioko vijiweni wakijihusisha na madawa ya kulevya, ukahabaa

Albamu yake ya kwanza Marufuku kukata tama anasema kuwa imewasaidia wengi waliokata tamaa na kuwapa matumaini mapya albamu hiyo na nyingine alioirekodi mwaka 2009 zilizoitwa huu ni wakati wangu na Moyo wangu.

John ametembelea nchi mbalimbali, akijifunza maisha ya watu ikiwemo kugundua kwamba karibu asilimia kubwa ya wanadamu, awe maskini, tajiri, msomi au asiye na elimu, wenye vyeo au waajiriwa, watoto kwa wakubwa, wanaume kwa wanawake, awe mzungu au mweusi n.k, wote kwa njia moja au nyingine wamepitia katika hali ya kukata tamaa au kukatishwa tamaa na jambo fulani, mtu, watu, hali au mazingira fulani.

Ndipo mwaka 2006, alipata maono na msukumo mkubwa wa kuandika Kitabu ambacho kitakuwa msaada kwa njia moja au nyingine kwa kila atakayekipata. Kitabu hicho kinaitwa Marufuku kukata tama. Kitabu hicho pamoja na kile kiitwacho “Mafanikio yatokanayo na kusifu na kumwabudu Mungu” vinategemea kukamilika baada ya miezi miwili.

Mwaka 208 sitausahau  ilikuwa ni siku ya huzuni na majonzi, siku ya kilio na kuomboleza. ni siku alipofariki mke wake mpendwa na mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili, Debora Shabani, mwimbaji aliyegusa mioyo ya watu wengi ndani na nje ya nchi, niliumia sana lakini sikukata tamaa”anasema.

Shabani alitunukiwa tuzo ya heshima pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake kwa ajili ya kuinua vipaji na pia kuchangia kuinua muziki wa Injili Afrika mashariki na kati. Pamoja na hayo amekua akianzisha vikundi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu Tuzo anayosema kuwa ilitolewa na kampuni ya Christian promoters Ltd, Pia ni miongoni mwa waanzilishi na kiongozi wa Chama cha muziki wa injili Tanzania (Chamuita).

Mwaka 2011, John alipata heshima kubwa kama mwalimu, kuongoza kundi la waimbaji (Tanzania gospel all stars) kuimba wimbo maalum wa miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.

Anasema kuwa pamoja na mzigo mkubwa aliokuwa nao kwa kidogo anachopata,amehakikisha kuwa anaisaidia jamii, hasa watu wenye ulemavu, wajane na yatima Vijana waishio katika mazingira magumu, pamoja na wakimbizi. Tayari ameanza mikakati ya kusajili Taasisi Hope Foundation kwa ajili ya maono hayo.

Pamoja na malengo mbalimbali aliyonbayo Shabani, lakini pia ni kuwa na kituo cha watoto na vijana, lengo ni kuandaa kizazi chenye maadili mema, kuibua, kutambua na kuinua vipaji vya watoto na vijana, mbinu na mikakati ya kuwakwamua watoto

Pia anasema kuwa mpango huo unalenga kutafuta ufadhili kwa ajili ya kuaendeleza vijana kielimu pamoja na kuwawezesha pale inapobidi, kuandaa matamasha ya watoto na vijana, kuunganisha watoto na vijana wengine duniani, kuwapa kipaumbele watoto na vijana wenye elemavu, kuwa na kiwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali ya watoto na vijan.

Kwa sasa anajishughulisha na kufundisha bendi,vikundi na waimbaji binafsi na kusema kuwa lengo ni Kufundisha kuimba au kunyoosha,Jinsi ya kuitumia sauti kuitunza na kuitawala,  Historia ya muziki na maadhi ya muziki, Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora, Matumizi ya kipaza sauti,Kuwatungia nyimbo au kurekebisha nyimbo zilizotungwa tayari, Kutoa ushauri kwa wanaotatarajia kuingia studio, mbinu za kuitangaza albamu au nyimbo zikubalike na Kutengeneza muziki wenye viwango.


Papaa On Tuesday...Hata Ukizima Mshumaa Wa Mwenzio Haufanyi Wako Uwake Zaidi

Ninakila Sababu Ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya siku ya Leo kwa Kuweza Kutupa tena Uzima katika Maisha haya tuliyo nayo. Kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu,kuna rafiki yangu Zulfa alitoka kwenda Matembezi ya Weekend amepata ajali wamekata Mguu sasa ni Kilema. Hata kama hakuna aliyekufa ama kuwa kilema kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu kwamba tunaishi.

Mwanamuziki Elton John akiwa na Bernie Taupin Mwaka 1973 waliuandika wimbo "Candle In The Wind" ukiwa maalum kwa ajili ya heshima ya Marehemu Marilyn Monroe. Maisha 


yetu ya kila siku kwenye dunia hii ni kama Mshumaa, Ka nafasi ulikonako hapo ofisini 
kwako ni kama ka mshumaa, sehemu ya biashara uliyopo ni kama ka mshumaa, maisha yetu

 ya kila siku ni kama Mshumaa ambapo mishumaa hii inatufanya kuwa nuru, Mishumaa hii 

inatufanya kufahamika na kukubalika kutokana na mwanga tunaoutoa, njia tunayoionesha

yenye kuleta mafanikio.

Ingawa Kila mtu ana mshumaa wake kuna wengine wamekuwa na jitihada mwamwi 

(Mwanzo Mwisho) kuhakikisha mishumaa ya wengine inazima ili ibaki peke yao kutoa 

mwangaza na kuonekana wao ni bora kuliko wengine. Kumulika kwako wewe na kutoa

mwangaza na kung'aa kwenye maisha kuna wanyima usingizi wengine, kuna wakosesha raha

 wengine, ukiuliza hasa kama kuna sababu ya msingi wala hakuna sababu ila tu yeye 

hafurahii mafanikio wengine wanayopata hata kama nae ana mafanikio lakini unakuta

 anahitaji zaidi. Maisha yenyewe haya yetu ya kila siku Unafukuzana na hela ya Unga, 

Ukipata hela ya unga unagundua Chumvi imeisha, unakimbiza hela ya chumvi ukipata 

umegundua pampass zimeisha kila siku ni mbio mwamwi lakini ajabu from no where kuna

 mtu hapendi mafanikio yako.


Kwa kadri ambavyo tumekuwa tukiwaponda wengine kwa kile wanachokifanya basi vivyo


 hivyo na sisi tumekuwa tupondwa mahala pengine kwa kile tunachokifanya. Kuna watu 

hawapendi mafanikio yako live live ama kuna wale wa Silent Killers ukipata tatizo ama 

baya likikufika wanakutana wanagongeana mikono wanasema "Tulijua hafiki mbali" wewe 

ni Mkristo au Muislam wa wapi unayefurahia kushindwa kwa Mwanadamu Mwenzio. Wewe 

umekuwa Mtu wa Kushangilia kwa matatizo ama kukwama kwa wengine??maisha ni 

Mzunguko zamu yako itafika tu.




Kwenye maisha nimekutana na Watu ambao bila sababu wananichukia, inawezekana hata 


wewe umekutana na watu ambao wanachukia mafanikio yako bila sababu. Akipatikana mtu

 akamuuliza pengine hata pasipo kufahamu akamuuliza "Inaonekena Stella biashara

 zinamuendea pouwa sana ndo maana ameweza nunua gari", basi huyu anayekuchikia bila

 sababu utadhani ndo ana majibu yako yote atasema "aaah wapi unadhani hela yake,

 kahongwa lile gari, umalaya tu hakuna kitu anafanya mjini.." huyu mtu anaongea sana

 negatives kuhusu wengine. Kila anachoulizwa cha kwako yeye anaponda mbaya anaongea 

negatives mwanzo mwisho, kama ni kazi ofisini anakuongelea vibaya mpaka wengine 

wanashangaa, anatamani kuzima mshumaa wako ili wake ubaki unawaka raha yake wewe

 ufukuzwe kazi abaki yeye ndo aonekane bora,ukiwa na tabia hiyo kwisha habari yako.


Kuna watu wanachukia mafanikio ya wenzao bila hata sababu, furaha yao wao ni kuona


 wenzao wana huzuni siku zote, ukikutana nao wanakupa pole mpaka machozi yanawatoka

 kumbe mioyo yao ina kung'ong'a, anachukia kila hatua ya maendeleo yako. Kwanini kuzima

 Mshumaa wa mwenzio ili uonekane wako ndo unawaka??maisha hayako hivyo, unaweza

 ukamfanyi mtu leo ubaya ili uonekane wewe ndo boss, unataka uonekane wewe ndo Alfa

 and Omega, jua kitu Kimoja wewe sio Mungu wa Kumpangia Mtu maisha yake inawezekana

 hujui kuwa unatumika kumuandaa hiyo unayomfanyia huyo mtu kuwa na future nzuri. 

Kumpiga teke Chura ni Kumsaidia Kuruka. Kama tunajisikia raha kuumiza mioyo ya watu ili

sisi tuonekane bora kuliko wengine. Kuna Wakristo kabisa lakini ni wanafiki wakubwa 

kutwa kucha kutamani wenzao wakwame ili wao waonekane bora zaidi.


Kwenye maisha tunayoishi nasema tena kumpiga teke chura ni kumsaidia kuruka kuna 

wengine wala hawajui kuwa wanatumika kuwaimarisha wengine kwa maneno yao, leo

 ukinisema pembeni kwa watu inakusaidia nini, kama kuna mtu unajua hafanyi vizuri kuhusu

 kitu fulani kwanini usimwambie??Kuna watu wao ni Ma-Master of everything kama redio

 moja maarufu hapa nchini wao wanajua kila kitu kwenye vipindi vyao. Tunatamani

 wengine wachemshe ili unachokifanya wewe kionekane kuwa bora. Huu sio Ukristo wala

 sio Uislam hata ma Ma-Budha hawafanyi hivyo ni Upagani wa hali ya Juu. Inakusaidia nini

 kumsema mtu kuzima mshumaa wa mtu wakati unajua Mshumaa wako hautafika mbali.

 Usilewe Sifa kwa sifa unazozipata leo, leo watu wanakushangilia sababu una hela ama una

 kipawa kila sifa iko kwako, kuna siku vitaisha kuna siku atakuja bora kuliko wewe kama 

wenzako walivyoachwa ndivyo ambavyp utaachwa, niliwahi kuandika Usitukane Wakunga

 wakati Uzazi Ungalipo. Usijione bora kwa Mshahara unaoupata kwa kazi ya sasa maisha ni

 kupokezana ndugu yangu. Mungu sio Filikunjombe mwenzako itafika zamu yake. Wewe 

wadharau watu sababu wewe unajiona bora kuliko wao, roho mbaya haojawai kupanda bei

 tangu imeanza kutumika zaidi ya kushuka bei, tafuta wenye roho mbaya kama wewe 

ambao kwenye maisha wamekuwa wakitamani wengine wasitokelezee wabaki wao kama

 miungu watu kama waliwahi kufika mbali, ukizima mishumaa ya wengine jua tu na wako

 utazimwa tena ghafla mno saa usiyodhani, maana kabla ya wewe alikuwepo mwengine

kama wewe.



Ipo haja ya sisi kama Vijana, Watanzania na Wakristo Kusaidiana, kuna watu wana mawazo

 ya ajabu sana wanaonaga eti ukimpa "deal" fulani eti atatoka, unaogopa kumtoa mtu??

unataka utoke peke yako basi wewe sio Mungu ukigoma kutoa watu utashangaa wanakupita

 wewe bado umesimama pale pale. Biblia inasema wazi ni heri Kutoa kuliko Kupokea,

 haijakataza kupokea ila heri ipo kwenye kutoa, Unavyotaka watu Wakufanyie kwenye

 Maisha Wafanyie wewe wengine, kama unataka Kutolewa kwenye maisha ukatoka, basi

 kwanza anza kusaidia wengine kutoka leo. FM Academia wana Chorus inasema "Aliyekupa

 wewe ndiye kawanyima wao, dunia mafungu saba" kuwa makini.


Think differently and Make a Difference, kumbuka Muosha huoshwa, Kila aliye mwalimu leo

 aliwahi kuwa Mwanafunzi.



Papaa Ze Blogger.

0713 494110.