CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Christina Shusho Atwaa Tuzo Ya Mwanamuziki Bora Kutoka Africa Mashariki Katika "Africa Gospel Music Awards"


Hatmaye Kampeni Zilizokuwa Zikiongozwa na Media Mbalimbali Za Kikristo na Kipindi Chako Bora Kabisa Cha Chomoza Ya Clouds Tv zimezaa matunda baada ya Mwanamuziki wa Injili Kutoka Tanzania, Christina Shusho kufanikiwa Kutwaa Tuzo ya Inayowahusu Wanamuziki wa Injili Africa almaarufu Africa Gospel Music Awards.

Christina Shusho anatwaa Tuzo ya Pili kubwa baada ya Mwanzoni mwa Mwezi July Kutwaa Tuzo nchini Kenya kwenye Tuzo za Groove Awards zinazofanyika nchini humo, na katika Tuzo za Africa Gospel Music Awards Shusho alikuwa akishindanishwa na Wanamuziki 6 Kutoka Kenya, Wawili Kutoka Uganda na Mmoja Kutoka Tanzania yaani Martha Mwaipaja.


Katika Usiku wa tarehe 7 July, 2013 wakati Shusho akitangazwa kwenda Kuchukua Tuzo hiyo hakuwepo nchini Uingereza bali Blogger Maarufu Tanzania mwenye Kumiliki Blog ya Gospel Kitaa Ambene Michael aliyeko nchini Uingereza aliwakilisha vema upokeaji wa Tuzo hiyo ya Shusho

Kushoto  ni Blogger Ambene Michael aliyepokea Tuzo Kwa Niaba ya Shusho Nchini Uingereza


Viva Shusho Viva Tanzania.