CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

***NILIYOJIFUNZA KUHUSU USAFIRI WA NDEGE NA MAISHA YETU***


Mambo kadhaa niliyotafakari na kujifunza katika kusafiri kwangu hata kama sio sana(Maana najua wapo wapimaji),hususani usafiri wa anga nimeona kabisa mchakato mzima unafanana kabisaaaa na Maisha yetu ya kila siku!!
i. Kwanza mtu unakuwa na destiny,yaani mahali unakwenda na hapo unaamua muda na namna ya kwenda huko uendako na yamkini hata saa au siku ya kwenda!
*Hii ni sawa kabisa na maisha maana mtu huwa na ndoto au mipango fulani au destiny kisha unaamua mwenyewe ni lini uanze safari kuelekea ndoto yako!

ii. Hili ni basi kwa maana ya "basi"kama mabasi mengine Ila sema hili linapita angani(Airbus), kwahivyo unakuwa na tiketi kisha boarding pass na unapanda na kukaa kama basi la kawaida tu!
*Katika maisha kuna mambo mbalimbali mengine sio tofauti na wengine Ila tu hufanyika tofauti na wengine!

iii.Ukiwa ndani ya ndege kwa kuwa sio sebuleni kwako yako maelezo na maelekezo muhimu za kuzingatia ili safari yako Iwe murua...mfano urefu wa safari,umbali toka usawa wa bahari na usalama ndani ya ndege...ni muhimu kuzingatia ingawa wengi hupuuzia wakidhani wao ni wenyeji sana!
*Katika maisha ni muhimu sana kuzingatia maelekezo, mafunzo na hekima kabla ya kuanza safari kwenda kwa ndoto yako,hata kama una kipaji ni muhimu sana kujifunza namna ya kufanya na kipaji chako ili wewe na wote wanaofaidika na kipaji hicho wafurahi.... So ni muhimu kuwa na washauri,waelekezaji na mentors kwa Kizungu!!

iv.Ndege ikitaka kuondoka,huanza kwanza kuondoka ilipopaki na kwenda kuanzia mwanzo kabisa wa barabara ya kukimbilia (running track) na na hapo huanza kukimbia kwa nguvu lakini hupita usawa uleule ambao ilikuwepo kisha kuondoka....
*Kama ambavyo ndege huenda kuanzia mbali na kisha kupitia pale pale kabla ya kuondoka basi hata katika maisha ni vivyo hivyo...kabla ya kuanza ndoto zako ni kama huwa unaenda kujianza mahali kisha unapita pale pale kwa watu wako au katika mazingira yako na kusema sasa ndio naenda eeh!! Na huku chini watu wanasema Oooh jamani yuleeee!!
(Zaidi ya hapo Nataka kusisitiza kuwa hata uweje hauendi kuishi mbinguni jamii yako ni hiyo so wewe ni jamii tu)

v.Ndege hukimbia sana kwa barabara ya kukimbilia kabla ya kupaa na wewe Ukiwa ndani utasikia mtetemeko zaidi hapo na mara ikianza tu kuiacha ardhi ni kama vile husikii saaana na angani huwezi Ona spidi yake maana ni kama imesimama tu!!...Iko maana kubwa sana ndege kukimbia chini kabla ya kuruka!!
*Ukianza safari kwenda kwa ndoto yako usikurupuke, unahitaji kujipasha na kujihakiki kuwa sasa uko tayari kwa matumizi ya wafaidikaji na ndoto au maono au vipaji vyako!!
(Usijaribu kukimbiakimbia haraka haraka eti upae haraka basi una hatari ya kurudi chini kwa kuanguka au kuanza upya... Unaweza ukaexperience misukosuko lakini ndio sawa lazima mtetemeko kwanza before ung'ae!

vi. Na Ukiwa chini unaweza ukadhani kuwa huku juu ndio kuna Network kubwa ya mitandao ya simu kwasababu huwa tunapanda miti zamani kuitafuta lakini ukweli ni kuwa huku juu hakuna network kabisa labda kama kwa simu maalum!! Kwahiyo ni muhimu kutumia network ya huko chini vema na sio kutaraji ya huko juu utachemka!!
*Ni rahisi sana kuona utaruka muda sio mrefu na hivyo kuanza kudharau watu au kupuuzia network zako za kitambo eti kisa utakutana au unatazamia kukutana na watu wengine wakubwa huko juu...Nakwambia kabisa usije ukaharibu uhusiano wako na Mtangazaji au Mwalimu aliyekufundisha mpaka ukafika hapo eti kisa unafahamiana na mwenye Chombo cha habari au mwenye shule...utafeli haraka sana

vii.Jambo la saba la mwisho kwa tafakari ya leo ni kuwa ukiwa chini huwa unaona mawingu na unajua yako mbali sana na mara ukiwa ndani ya ndege unayakuta mawingu moshi, hapo unaweza ukajisemea aah kumbe mawingu yako hapa tu,lakini ukweli ni kuwa mawingu yale ya Blue (sky) yako mbali sana sana na hata ndege haiwezi sogelea hatA.... Sasa ni muhimu kujua tofauti ya Clouds na Sky ili usije ukaoverexpect kisha ukapata frustration!
*Ni rahisi sana kuelezea possibility ukiwa hujaanza safari kuelekea huko,yawezekana ni rahisi kusema kuhusu jinsi ilivyo rahisi kufanya biashara fulani na ukachambua faida hapo au jinsi ya kufahamika au jinsi yeyote ya kwenda utazamiapo... Na labda tu ndio umejaribu kidogo tu na ukapata appreciation au umaarufu au kafaida kidogo tu basi unadhani safari imeisha.... Kuwa makini aisee Oooh!!

Nimetumia muda wangu wa angani vema kuandika hii mpaka natua naamini kuna Mtu itamsaidia somewhere, kama sio wewe basi ndugu waweza endelea tu na mambo yako na Amani iwepo!!

....Labda kuna wakati nitasema ya huko angani na kutua but I don't promise, hiyo ilinijia tu basi nikaona si vema nikapuuzia!!

NAAMINI WALE WOTE WENYE AKILI TIMAMU NA WENYE NDOTO ZAO ITAWAFAA HII NA WALE WANENAJI AU WASHAURI MWAWEZA TUMIA HII KUKAZIA MSEMAYO HUKO!!

Ubarikiwe sana na uwe na wakati Mzuri!!!

(c)King Chavvah, 2014
#LearnToLearnLearning!!!