CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

HEKIMA KUTOKA KWA MY PS......"KABILA HALIRITHIWI"!!!

Habari zenu!
Najua mmemiss hekima za MY PS sana!
Nimepata bahati ya kukaa na kuongea nae mara kadhaa na nakumbuka moja ya jambo ambalo alilisema wakati ninamuhoji kuhusu asili yake ni hili;

Nilimuuliza wewe "Prosper Mwakitalima" ni mnyakusa wa wapi?(Maana ninajua kwa hakika Mwakitalima ni mnyakusa)

Lakini chakushangaza alinijibu akasema yeye ni "MNYIRAMBA WA SINGIDA" ndio hapo sasa tukaanza mjadala kuhusu makabila na kwa hakika ilikuwa ni maada tata lakini mwisho wa siku tukafika muafaka kuwa kabila halirithiwi!!

Hebu zingatia mfano huu
1st Kizazi;
A-family>>Baba Msafwa na Mama Mchanga,wanaishi Mtwara na wanapata watoto huko,
B-family>>Baba Mnyamwanga na Mama Mpare,wanaishi Kigoma nao wanapata watoto huko

Sasa huyu Mtoto wa A-family aliyekulia Mtwara kwa wamakonde anakuja kumwoa Binti wa B-family aliyekulia Kwa Waha kigoma na hawa wawili wanaamua kuishi Songea kwa Wangoni.....Sasa wakipata watoto,watoto wao watakua kabila gani??

Utagundua kuwa inabaki tu majina lakini ukweli ni kwamba asili zimeshapotea sana na sio jambo la kushikamana nalo kabisa,hiyo My ps alivyoniambia yeye ni Mnyiramba alikuwa sawa maana amezaliwa huko singida na kukulia huko kabla ya kuja Dar akiwa mkubwa tu,hivyo anafahamu zaidi unyirama kuliko Unyakusa.


VIPI KWA MFANO HUU;
Mkurya mmoja wa Mwanza  alimpa mimba Dada wa Kigogo na kumtelekeza Shinyanga(Kwa wasukuma),basi binti yule kwa mateso alipojifungua tu akamviringisha mtoto na kumwacha jararani,hapo Dada wa kindali alimwokota na kumpeleka polisi na hapo alitokea msamaria mwema akamuomba mtoto akamtunze na huyu ni Mkinga anayeishi Mtwara....sasa ikiwa huyu hajui mzazi hata mmoja wa mtoto na yeye ni mkinga anaeishi na wamakonde....JE HUYO MTOTO ATAKUWA KABILA GANI AKIKUA????

Ukipata majibu yatunze sana,lakini cha muhimu ni kuwa KABILA HALIRITHIWI.....Ila pale umekulia na kulelewa ndio palipokushape na kukufanya hivyo uko now na hakuna half cast wa kabila hata siku moja!!

Unaweza ukaendelea kutafakari na yamkini kuuliza ama kuchangia pia

By King Chavala-MC
+255 713 883797
http://kingchavala.blogspot.com

DARE NOT TO MISS.....LIVE SEMINAR WITH AZIM JAMAL IN DAR!!!!