CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Papaa On Tuesday.....Kwanini Hatujifunzi Kutokana na Makosa?


Wakati Wamarekani na watu wengine mwaka 2011 walisheherekea kuuwawa kwa Osama Bin Laden, ni vema tukakumbuka kujifunza kutokana na makosa hasa tukajifunza kutoka kwenye makosa tunayofanya wenyewe. Kuna msemo unaotumika kuwa “Experience is a good teacher” lakini ninahisi bado Experience hajawa mwalimu mzuri kwenye maisha ya watu wengi sana. Hujawahi kuona swali liliwahi toka mwaka Fulani na watu wakapeana ‘Past Papers” na swali lile lile mtu akakosa?ama swali hilo hilo mtu amelifanya kwenye assignment amekosa na baadae akaelewa wapi alikosea lakini baadae akakosa tena, au mtu anaingia kufanya biashara moja na katika kufanya anagundua kuna kitu alikuwa anakosea akapata hasara akianza biashara ya pili anarudia makosa yale yale. Au hujawahi ona mtu anacheza upatu kama ule wa siku zileeee “Faida Investment” ana akapata hasara kutokana na hasara akajiapiza hatacheza tena upatu, ajabu ilipokuja “DECI” akarudia makosa yale yale na ikala kwake, kuna mwingine amewahi kuwa na relationship zaidi ya 2 lakini makosa aliyokuwa anafanya awali ndo hayo hayo yanamtesa mpaka leo, umewahi jiuliza kwanini?Hujawao ona kuna mtu ameumizwa moyo zaidi ya mara 800 na kila siku anaapa, mie siwezi mpa mtu moyo wangu, anaongea utadhani amejifunza baada ya miezi 6 yale yale yaliyotokea kwenye uhusiano uliopota ndo hayo hayo yanatokea hata sasa.
Kuna mwingine anasahau mpaka unahisi “anaugonjwa wa kusahau” wakati mwingine kusahau kwake kumemsababishia kuingia katika gharama za ziada ambazo pengine hawakuwa amepanga kuingia, wengine kutoka na kusahau wamepoteza trust hata kwa waajiri wao makosa yale yale waliyokuwa wakifanya awali ndiyo wanayorudia. Unakuta mwezi huu umeelekezwa labda kazi hii inafanyika hivi ajabu kosa la mwezi uliopita unalirudia vile vile wengi wetu tunadhani kujisikia vibaya ni dalili ya kubadilika. Utasikia mtu anasema "ninajisikia vibaya sana kukosea", Kujisikia vibaya haitoshi ila kujifunza katika yale tunayoyakosea katika maisha.

Unakuta makosa ya matumizi mabaya ya Mshahara wako yanajirudia kila mwezi hakuna siku ambayo mshahara ukakutana, mshahara wa mwezi huu haujawahi kusalimiana na mashahara wa mwezi ujao wanapishana siku wiki nzima, makosa hayo yamekupelekea kwenye madeni ya kila mwezi unajikuta wewe ukishika mshahara huna chako umewashikia wengine hela zao unabaki kujisikia vibaya kujisikia vibaya hakukusaidii mwezi ujao usirudie makosa, kujifunza katika tatizo na kuamua kubadilika ndiko kutakusababisha kubadilika kutoka katika hali uliyonayo.
Kuna watu wamewahi jichukia nafsi zao na tabia zao, na kuna wengine waliwahi jiapiza kuwa hawata rudia tena lakini ndo utadhani wamejiapiza kufanya zaidi ya alivyokuwa anafanya mwanzo. Kujifunza ni mfumo wa kila siku lakini kujifunza kutokana na Makosa hata Serikali yetu imekuwa ni tatizo. Makosa yale yale yanayotokea kwenye Serikali na kupelekea upotevu wa fedha nyingi za Serikali, ndio huo huo pia utatokea mwakani na mwakakeshokutwa pia. Makosa yale yale yanayoitesa CCM ndiyo makosa hay ohayo yatatesa NCCR-Mageuzi ndo hay ohayo yataitesa CHADEMA na ndo hay ohayo yataitesa TLP. Sababu zile zile za kufeli kwa wadogo zetu kwenye shule za Sekondari mwaka huu ndo hizo hizo pia zitasababisha mwakani watu wafeli. Makosa yale yale tuliyofanya kwenye Uchaguzi wa mwaka 2010 ndo yale yale 2015 kwani kuna jipya??


Changamoto kubwa sana ambayo inainyemelea Tanzania yetu ni watu kupenda kuambiwa, yaani akiwa anaumwa yeye mwenyewe hawezi kujitesa kunywa maji, ila Daktari akimwambia asipokunywa maji atakufa basi atakunywa maji mpaka atawaboa, wengi wanaenda Gym siku hizi si kwa sababu wanapenda mazoezi aaah wanaenda “kujikinga na magonjwa” wakisha pungua unene wanarudia yale yale. Kama hauna “mood” ya mazoezi yatakushinda utafanya siku mbili tatu unaacha why?hatujifunzi kupitia makosa yetu.


Kila mtu anapaswa kujifunza kutokana na makosa, usiogope kukosea sababu ni sehemu ya kujifunza ukiogopa kukosea hautakuja kuweza ila ukikosea unajua kwanini ulikosea na nini au wapi urekebishe. Kabla ya kujua kuendesha baiskeli wengi walidondoka, kabla ya kuweza kuendesha gari wengi waligonga kwenye Reverse ila walipogonga ndivyo walivyozidi kujifunza. Kujifunza ni gharama,gharama ya kujifunza ni ndogo ukilinganisha na gharama ya kurudia kosa lile lile, kuna mambo ambayo pengine yana gharimu maisha yako kwa sasa kwa sababu tu kukosea kuchagua kitu Fulani, pengine gari ulilonunua linakugharimu sababu tu ya kukosea kuchagua, wengine wenzi wao wa maisha, wengine ni taaluma zao kila mtu ana “makovu yasiyokuwa na hisia” ambayo yanatesa watu wengi.

Zahma ambayo mtu ameipata kutafuta nyumba ya kupanga na kujikusanyia kodi ya nyumba ndo makosa hay ohayo yatatokea katika kutafuta nyumba na kukusanya kodi, kwanini?sababu hatuna utamaduni wa kujifunza kutokana na makosa. Makosa yale yale waliyofanya wazazi wetu katika umri wao wa kufanya maamuzi mazito ndiyo hayo hayo pia yatatokea na kwetu na kwenye vizazi vyetu. Usipojijengea utamaduni wa kujifunza hakuna wa kukufunza kwa kizazi chetu. Kwani wewe unafunzwa na nani makosa yale ambayo wewe uliyafanya ukaharibikiwa mapema si ajabu watoto wako pia yakawatokea kwa mwamvuli wa "uzungu" watoto wako katika umri wako ule wa kujua mema na mabaya watadondokea katika shimo lile lile. Tarehe ya mtoto kuzaliwa iko mbele kuliko anniversary ya Harusi yenu.
Uamuzi wa kujifunza ni wako usisubiri mtu wa kuja kukufunza, hata wanaokufunza walijifunza kwa kukosea, na kama unaweza kujifunza kabla ya kukosea kwanini usubiri kukosea ndo ujifunze?jifunze kupitia makosa yaw engine, walipokanyaga wao na kukosea wewe usikanyage.Usipochafuka utajifunzaje?

Kuna watu huwa wanasema usijifunze kwa walioshindwa maana na wewe utashindwa, kuna mtu aliwahi sema if you have never done any mistake,you have never tried something new. Kwanini uogope kujifunza kwa walioshindwa, kujifunza kwao kwenye mapungufu yao inasababisha mwerevu kujua njia gani aspite, kujifunza kwa waliofanikiwa peke yake ni mfumo ambao tumetengenezewa ili kutujengea ujasiri wa kuogopa. ndio maana kwenye interviews hata za ndoa utakuta wanaitwa watu ambao wamefanikiwa wanaonesha namna ambavyo wamefanikiwa mbona hatujawahi waita watu ambao wamechemsha tukawahoji kwanini walichemsha?kisa na mkasa eti hatuna jipya la kujifunza kwa walioshindwa ni kweli hatuna la kujifunza, katika kushindwa kwako mambo mengi ni kweli huwezi mfunza mtu?labda kama hatujajua makosa yetu ni yepi ndio maana hatuwezi wafunza wengine kile tulichokosea. Wote tunapenda story ya Petro aliyemkana Yesu mara tatu kisha akatengeneza, lakini hakuna mtu anayejifunza kwa Yuda aliyemkana Yesu kisha akajitundika kitanzi.


…//Papaa
0713 494110