CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441
Showing posts with label Ni Marufuku. Show all posts
Showing posts with label Ni Marufuku. Show all posts

NI MARUFUKU....KUVAA NGUO KIPUMBAVU!!!!

#....NI MARUFUKU!#
*Kwa kijana yeyote wa kiume kuvaa suruali chini ya makalio eti kata kei ama mlegezo....maana hiyo ilianzishwa na wafungwa wa marekani na ilikuwa dalili ya kiburi na Afrika kusini walikuwa wanavaa hivyo wafanyakazi wa Boers ili kurahisisha zoezi la kupigwa mihuri hapa juu ya matako baada ya kazi,na kwa sasa wanaume wasio riziki wa mashariki ya kati na ulaya wanavaa ili kuwavutia wateja wao kabla hawajaolewa....sasa wewe unavaa sasa hivi unamaanisha nini? Tena wengine unakuta boxer chafu kama nini....ukimuona kijana wa namna hiyo hata awe nani ama maarufu kiasi gani,ujue HAJITAMBUI!


 
 *Kwa kijana yeyote wa kike kuvaa nguo za kulalia,nguo za ndani ama nguo zinazomdharilisha yeye na wasichana wengine wote....yaani mtu anatembea mjini na skintight tu,mwingine anatembea ameyaacha maziwa nje,tena makusudi...acheni ujinga ninyi,kama nguo ni ya ndani vaa ndani,thamani yako haiongezeki kwa kujichoresha na kuacha maziwa nje,kila mmoja anajua kilichopo ndani so kifiche tu,by the way chenye thamani hufichwa.....hizo ni tabia za makahaba na night stripers sasa wewe unayevaa hivyo una malengo gani? Wengine maumbo mabaya na wengine miili imejaa makovu,jamani ficha tu.

 
 Sasa haijalishi ni nani wala nani,nimesema marufuku! Kama una akili timamu utazingatia hili lakini kama wewe ni mpumbavu basi unaweza kuendelea na nakuhakikishia usipobadilika mwisho wako utakuwa wa majuto...na kama utakuwa na watoto basi ndio utakuwa umeshawaharibu hata kabla hawajazaliwa!
SALAM HIZI NAZILETA BAADA YA MFUNGO KUISHA MAANA NAJUA KUNA WENGINE NDIO KAMA VILE WALIKUWA KIFUNGONI KUFANYA MEMA SASA WAMEACHILIWA KURUDI KULEKULE!
Na hata kanisani tusikuone na huo ujinga wako unless kama wewe ni agent na umetumwa kuharibu kanisa,potelea mbali ukinikasirikia lakini najua jambo moja tu.....MAMBO YOTE YATAPITA LAKINI NENO LA MUNGU HALITAPITA KAMWE!!


Na King Chavala MC
+255 713 883 797

Ujumbe huu unakujia kwa Udhamini mkubwa wa; 
http://chavalamedia.blogspot.com
(c)2013

#...NI MARUFUKU!!#(04)......KUFANYA MAREKEBISO JUU YA JAMBO LA KUAZIMA BILA RUHUSA!!!!

#.....NI MARUFUKU KABISAAAA#
Ni marufuku kabisaa kufanya mambo au marekebisho au matengenezo usiyoruhusiwa juu ya kitu au jambo la kuazima bila ruhusa ya mwenyewe!
Kwa kawaida kitu cha kuazima hakina uhuru wa kutosha,kwani umepewa kwa kipimo....waswahili wanasema...."Nguo ya kuazima haisitiri Matako"
Kuna mambo mengi tunajiamulia wenyewe juu ya vitu vya kuazima na kwa kweli huwa inakuwa sio sawa,kwa mfano;

a)Mtu anakuazima simu yako aongee na mtu mara moja maana yake imeisha airtime ambayo nayo alikopa na hapo mlipo hamna access ya kununua....sasa unakuta mtu baada ya kupiga kwanza anaanza *102#....hivi hicho ndio umeomba au? na haishii hapo unakuta ameongea na simu zaidi ya hata alivyoomba yaani unakuta mtu kajiachia kama yake vile na bado credit ikiisha na kwako eti anakopa na anapiga tena mpaka na hiyo inaisha na hapo hajakwambia kitu...sasa wewe unashangaa ukitaka kupiga yule mrembo anakwambia....hauna salio la kutosha kupiga simu...basi unanunua vocha faster....unashangaa message.....Ahsante kwa kulipa deni.....na bado unadaiwa ......ahhhh dah sasa ndio nini hivi?
Hapo ulipokuwa umemuachia basi kapiga picha,kafungua na picha zako na mpaka bundle yako ya internet imeisha eti kisa anadownload miziki...Sasa wenye tabia hiyo nawaambia Marufuku,acheni kuwakwaza wenzenu,mimi tabia ya hata tu kuazimana simu wala sioni kama ina mashiko sana kipindi hiki ambako simu ziko tele na mawasiliano ni rahisi kwa yeyote!!!.....Umewezaje kununua simu na unashundwa kununua vocha??

b)Mtu anakuazima gari na unampa kwa roho safi tu,halafu anakwaruzana huko na kikimbiza gari gereji mchwara huko wanaanza kukuharibia gari hali angekwambia wewe una fundi wako unayemwamini,sasa anafanya hayo yote na hasemi,wewe ukija kushtuka siku moja unakuta some spears kwenye gari hazipo....ama mtu anakwenda huko halafu anakutana na stickers basi ananunua na kubandika kwa gari yako....hivi umeazima gari yangu ukanipambie au utumie na kuirudisha,tena mbaya zaidi eti mtu anakuwekea masticker ya kipepo kabisa na yeye anafurahia...sijui Majani,Kappa au Monster Power...jamani Ni Marufuku kabisaaa,ukiazima kitu kirudishe hivyo hivyo na usijifanye wewe ndio mwenyejiiiiiiiii

c)Mtu amekuja kwako kukutembelea may be anakaa wiki moja au siku kadhaa,kwa kuwa ni mgeni hapa ni nyumbani pa kuazima...sasa unakuta mtu anaanza kupanga na kupangalua mara kochi hili ageuzie kule,pambo hili aweke kule yaani wewe ukitoka kwa mishe mishe unakuta everything has changed,jamani hapa kwako? hata kama umetamani kunisaidia kwanini usiniulize? unajua kuna saa mnavuruga mahusiano ya watu hivi hivi,yaani mwenyewe mlimbwende amepanga na kupamba na umekubali for sake of love halafu huyu mfukunyuku anakuja na kuharibu kisha anaondoka,unafikiri akija huyo mlimbwende siku moja unamwambiaje kama sio dharau hiyo!!!!

Ipo mifano mingi sana,lakini nimesema marufuku tena marufuku kabisa!!
HESHIMU MIPAKA YA CHOCHOTE UNACHOPEWA,SIO UNAKARIBISHWA SEBULENI WEWE UNAENDA MPAKA CHUMBANI AAAAH!!
......Sema neno na wewe kama tumeelewana!!!

N.B;Hii ni kwa faida ya mahusiano na urafiki wa ko na watu,na hii inawahusu watu wenye akili timamu tu na wanaojielewa na kujitambua!!

@Kwa hisani kubwa ya Chavala Ideas Platform <http://chavalamedia.blogspot.com/>
(c)2013

#....NI MARUFUKU!!!#(03).....Kuvaa nguo zenye maandishi ya AJABU AJABU!!!

#....NI MARUFUKU!!!#
Ni marufuku kwa mtu yeyote mwenye akili timamu,mstaarabu na mwenye future na anayejiheshimu kuvaa fulana/nguo au niseme T-shirts ambazo zina maneno asiyofahamu maana yake au hata kama ana fahamu maneno yasiyo faa....yaani wewe unanua tu bora ni Tshrt,zingine zina matusi aitha kujitusi mvaaji,au wengine wanaosoma au hata kuaibisha jamii yako.....Nimekutana na mtu amevaa tshrt imeandikwa..."I am proud of My Virgin Grandma" na mtu yuko happy tu dah! inawezekanaje Bibi yako mama yake na mama yako awe bikra hata sasa kama sio matusi hayo? 

MAMA YAKO ALIZALIWAJE NA BADO BIBI YAKO AKABAKI BIKRA KAMA SIO USHIRIKINA HUO????

 Unajua maana ya haya maandishi kwa tshrt hii?
Au mtu unavaa tu?

Kwanini basi usiulize kwanza kabla au mara tu unaponunua?\

Na watu wengine wala hawatakwambia utashangaa wanakucheka tu,kila ukivaa na wewe unaweza kudhani wanakufurahia kumbe kejeli!

JE UNAJUA KAMA NGUO KAMA HIZI ZIMEBEBA MAANA NA KUPIGIA DEBE MASHOGA NA WASAGAJI?

Nimeona nyingi sana lakini masikini wengine huwa hawajui maana yake hivyo wanavaa tu, na sehemu nyingine wazazi wengine huwanunulia watoto wao dah! haiwezekani mtu mzima akavaa Tshrt inayomtambulisha kama "kahaba mpole" mbona zipo nguo kibao zenye maneno mazuri tena ya lugha yetu ya kiswahili kwanini kuvaa kitu unachokielewa....najua unanielewa na yamkini umewahikuona na wewe mtu akiwa amevaa kituko....kama unakumbuka basi tupia mfano wa uliyowahi kuiona na useme ...HATA HII MARUFUKU KABISA!!!
ANGALIZO:Kwa wale wanaopenda kuvaa hivyo hivyo makusudi kabisa basi yamkini wana maana zao ambazo wangependa watu wajue bila wao kuongea kwa mdomo....hao ni issue nyingine,lakini wewe sio mmoja wa WASIOJITAMBUA NA KUJIKUBALI SAWASAWA NA UUMBAJI WAO,basi nimesema marufuku kabisa!!!

>>>Hii ni kwa ajili ya watu wenye akili timamu tu wanaojitambua na kujiheshimu tu.....vigezo na masharti kuzingatiwa!!

@Kwa hisani kubwa ya Chavala Ideas Platform <chavalamedia.blogspot.com>

#.....NI MARUFUKU!!!#(02)....Kwa Mwanaume Kufungua au Kupekua Mkoba wa Kike!!!


HABARI ZENU!!!!
Ni marufuku kwa kijana yeyote yule wa kiume au mwanaume kufungua au kupekua pochi au mkoba wa kike kwasababu yeyote ile hata kama ni rasmi,kama sio chini ya usimamizi na ruhusa maalum sana ya mwenye mkoba au pochi hiyo!!



Ni tabia mbaya sana kupekua pekua either kutafuta pesa kwenye pochi ya dada yako au mama yako au kutafuta ushaidi wowote ule kwa pochi ya mpenzi au mkeo....Je unajua pochi au mkoba wa kike unabebaga vitu gani? Je unafikiri pochi ya kike ni kapu la sokoni au? Vipi kama vilivyomo humo vikikupandisha presha ama kukupofusha,nani atakusaidia? na utajiteteaje?...Vipi kama ukivunja vya kuvunjika au kumwaga vya kumwagika? Vipi kama ukikuta picha ya ndugu yako either mjomba au mzazi utafanyaje?
Kama vile ambavyo sio rahisi wewe kumruhusu binti kupekua wallet yako vivyohivyo na wewe heshimu yao...nimewahi kuona baadhi ya vijana na wanaume wakinyang'anya na kupekua kwa lazima mikoba ya wadada au pochi za wamama na kisha kuwatupia chini,nilikuwa safarini na niliumia sana....na siku moja nilikutana na rafiki yangu mmoja na nikataka kumpokea mkoba na akakataa kabisa na kunieleza mengi na hapo ndio nikakumbuka maonyo ya mama kuwa ni marufuku kubeba mkoba wa kike isipokuwa kwa kibali maalum tena mkoba wa mtu maalum kama vile mkeo au mpenzi rasmi!!
Yamkini unafanyaga haya lakini hujui kama ni tabia mbaya,na wakati mwingine huwa unadhani ndio kujali,basi nikwambie wazi kabisa....Ni marufuku,tena marufuku tena marufuku kabisaaaaa!!
ukome ukomae kabisa...na hii ni kwa faida yako kijana,carrying someone's handberg might be an attitude of a gentleman but "pekuling" and "tafutaing" is a habit of Wamataifa...sasa nimesema marufuku,kama unabisha unaweza kuendelea tu!
Hii ni marufuku maalumu kwa watu wenye akili timamu tu!!

@Kwa Hisani kuwa ya Chavala Ideas Platform <chavalamedia.blogspot.com> (c)2013

#.....NI MARUFUKU KABISAAAAAA!!#(01).....Kufanya Maamuzi kwasababu ya kumhurumia mwingine!!!!

HELLO GUYS!!
Ni marufuku kwa mtu yeyote yule mwenye akili timamu kufanya maamuzi yeyote yale muhimu yanayobeba mstakhabali wa maisha yake kwa kigezo cha "KUWAONEA HURUMA WENGINE KATIKA MAAMUZI YAO"


Kwa mfano;
Eti mtu anakubali kuingia katika mahusiano kwasababu tu mtu huyo amekufuatilia kwa muda mrefu,kwa hiyo unamuonea huruma mdada au mkaka wa watu.....hivi wewe una huruma kuliko hata neno huruma lenyewe,aliyekwambia huruma ni kiunganishi nani?
AU
Eti mtu amepata kazi nzuri ambayo mahali pengine ambapo atalipwa zaidi ya mara mbili ya alipo sasa na kazi ni uhakika,lakini mtu huyo anasita na kubaki hapo,kwa madai ya kuwa mwajiri wake wa sasa atajisikia vibaya,sasa wewe unaishi kumfanya ajisikie vizuri hali unateseka na maisha yako?
AU
Mtu anakuomba umsaidie kitu,na wewe unajua kwa hakika kitaharibu muda wako na labda na hadhi yako,lakini kwasababu unamuonea huruma huyo anayekuomba basi unakubali,angalia usije ukajitafutia laana,kuna mama mmoja aliwahi kumuokoa mwanae wa kiume ili asife kwa kutembea nae baada ya kijana huyo kunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume huku akimngojea mpenzi wake na bahati(sijui mbaya au nzuri) huyo mpenzi hakuja,na dawa hizo ukinywa usipotumika unaweza kuondoka(hivi ndivyo ilivyo),na mama huyo aliwasihi dada zake wamsaidie wakagoma ila yeye akaona ni bora amuokoe mwanae,sasa yaliyomkuta mama yule ni kupata mimba ya mwanae na ili kuficha aibu alitaka kutoa na katika kutoa sijui ilitokea defects gani mwilini basi akapalalaizi na kazi akaacha na maisha yote yakasimama na kubaki majonzi,sasa sijui huyu mama tunamsemeaje lakini hata sasa kijana alishakimbia kuficha aibu na mama ndio huyo anateseka kitandani!
SASA SIO KWA MIFANO HIYO TU BALI NA MINGINE MINGI,TAFADHALI USIFANYE MAAMUZI YA MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO KWA KUJIONEA AU KUWAONEA HURUMA WATU WENGINE...BE REAL AND BE YOURSELF!!!
Ni marufuku kujaribu kufanya ujinga huu......kama na wewe umenielewa sema kwa nguvu.......NI MARUFUKU KABISA!!!!