CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

KULA MATUNDA SIO LAZIMA USHAURIWE NA DAKTARI!!!

Habari zenu!
Watu wengi sana hawana tabia ya kula matunda ipasavyo! wengine huona kama ni chombezo mezani,wengine ni ziada na wengine ni mpaka daktari aseme!

KULA MATUNDA KUNA FAIDA NYINGI SANA,HIZI NI BAADHI YA HIZO CHACHE;
a.Matunda mengi ni dawa, maana yana virutubisho asilia
b. Matunda yana Vitamini nyingi sana na madini, na matunda mengi yana Vitamin C
c. Matunda hususani yale yenye nyuzi nyuzi (rouphages) husaidia mmeng'enyo na uyeyushaji wa chakula mwilini.
d. Matunda huongeza damu mwilini na kusafisha pia mfano ndizi huongeza vitamini K ,ambayo inasaidia sana kwa WALE WENYE MATATIZO YA KUTOKA DAMU PUANI.
e. Matunda yenyewe ni mlo wa kutosha kabisa na kwa mujibu wa wataalamu mtu anaweza kuishi kwa matunda tu na bado akawa na afya njema kuliko mtu anayekula vyakula vingine!
Punguza kula mafuta mengi na sukari kwa mbadala wa matunda!

Kuna matunda mengine watu wanaona ni kama viungo tu lakini nataka nikwambie matunda na mbogamboga kama vile NYANYA,KAROTI,LIMAO ni matunda safi sana na viungo kama TANGAWIZI,VITUNGUU SAUMU NA VITUNGUU MAJI unaweza kula kwa kutafuna maana husafisha mwili na damu sana!

UNAPOKULA MATUNDA UNAKULA VITU ASILI,DAWA ASILI,MADINI NA VITAMINI ASILI,MAJI NA SUKARI YA ASILI....Hivyo kama huna utaratibu wa kula matunda basi anza sasa!!!

Huna haja ya kunywa chai asubuhi kila siku,wakati mwingine anza na matunda tu na hata unapolala usijichindilie na chakula kingi kizito,unaupa mwili kazi ngumu na kisha unalala, hivyo utashangaa unamka mchovu na kitambi kinatoka bila mpangilio!!

ANZA SASA KULA MATUNDA KWA AFYA YAKO!!!!

Niulize nikushauri
0713883797