CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

ZOOMING ZONE 0004.......Na PROSPER A. MWAKITALIMA, The T-shirt Printer tycoon!!!



HELLO HABARI!
NAAMINI MKO POA NA MNAENDELEA VIZURI, NILIKUWA KIMYA KWA MUDA NA HII NI KWASABABU ZOOMING ZONE SIO MAKALA YA KILA SIKU AMA KILA MTU, HIVYO LEO LENZI IMEMULIKA KIJANA MMOJA HAPA MJINI NA HUYU NDIO ATAKUWA……Zooming Zone 004
************************************************************************************               
Zooming Zone 0004....Na Prosper A.Mwakitalima
Huyu sio mwingine basi ni kijana mjasiriamali “SWAHIBA” anayetamba na kujulikana sana kwa KUCHAPISHA T-SHRTS vizuri, nzuri na zenye maneno mazuri hapa Mjini, Tanzania.
Naam pia ndio huyu ambaye habari zake zilivuma sana hapa mjini kwa kupona“kufufuka” toka katika ajali mbaya sana sana pale maeneo ya River side Ubungo  23/11/2011 iliyohusisha lori la mafuta na gari yake ndogo,ajali ambayo ilichukua maisha ya watu kadhaa akiwemo mama mmoja mjamzito ambaye alikatika kichwa(ilitisha sana kwa kweli)….lakini Jambo la kushangaza ni kuwa kijana huyu alipona kabisa maana hakuvunjika mfupa wala mshipa Zaidi ya michubuko kadhaa tu,hakuna aliyeamini hata leo lakini huo ndio ukweli!
Huwezi kuamini lakini huu ndio ukweli!

Huyu pia ni mmoja wa washika dau na wawezeshaji wa Mtoko wa marafiki Mjini uitwao “FRIENDS ON FRIDAY (FoF)”, na ndio mbeba maono na mkurugenzi wa “SIFA TANZANIA”Mfululizo wa matamasha ya kumwinua Yesu hapa nchini Tanzania.
Huyu ni PROSPER ALFRED MWAKITALIMA a.k.a SWAHIBA a.k.a “The Next Billionaire” (King Chavala tu anaruhusiwa kumwita “MY PS”)
 
Prosper,Wambura na Chavala Singida
NILIBAHATIKA KUFANYA NAE MAHOJIANO HIVI KARIBUNI KWA KINA NA NIKAPATA MENGI SANA NA HAYA NI MACHACHE KATIKA MENGI, AMBAYO NAAMINI YANAWEZA KUKUSAIDIA KUMFAHAMU VIZURI NA YAMKINI KUJIFUNZA MENGI KUTOKA KWAKE, HUYU NI KIJANA WA KIPEKEE AMBAYE NI MFANO WA KUIGWA NA VIJANA WA KITANZANIA…..FUATANA NAMI KATIKA MAELEZO YANGU KUHUSU 

YEYE NA UKIRI WAKE MWENYEWE NA PICHA MBALIMBALI AMBAZO ZINAONYESHA HISTORIA YAKE HATA SASA!!!

HISTORIA;
Lazima yeye afanye tofauti tu!

Prosper A. Mwakitalima ni mtoto wa mwisho wa Mchungaji Alfred Mwakitalima, mnyakusa alijichimbia na kujenga maisha yake huko Singida-Tanzania…Na huyu kijana mesema yeye ni MNYATURU ingawa baba yake ni Mnyakusa, 
 
Prosper na nduguze enzi hizo...
na nilishangaa kwanini iwe hivyo lakini akaniambia KABILA HUWA HALIRITHIWI (TRIBE IS ACQUIRED)….Prosper alisema hawezi kuwa mnyakusa hali amezaliwa na kukulia Singida kabla ya kuja Dar es salaam.
Tangu kale hata sasa Prosper ni mchangamfu....
Prosper alisoma shule msingi iitwayo MGHANGA PRIMARY SCHOOL na kasha kujiunga MWENGE SECONDARY SCHOOL  zote za mkoani Singida,

Kaka na Dada Skongaaa
Prosper akimlilia Bwana Yesu...




Prosper akipokea Cheti

 kabla ya kwenda High School katika sekondari ya MILAMBO iliyo Mkoani TABORA ambapo alisoma masomo ya Lugha. Akiwa hapo alisoma na watu wengi sana na wachache kati ya hao ambao ni wa muhimu sana hapa nchini ni hawa Mchungaji Mathew Sasali, Mkurugenzi wa Radio Ushindi yenye makao yake makuu jijini Mbeya pamoja na Mwanaharakati Mussa Bilageya.
Prosper akipokea Cheti wakati wa mahafali

Wengi hawaamini kuwa huyu kijana anaweza yote haya
 **********************************************************************
vipaji ndio viko lukuki kwa kijana huyu,ona alivyokuwa hapo kale....
Kipaji cha Ubotozi alikuwa nacho.....

Uigizaji hakukosekana......

Kuimba ndio usisema hata sasa.......
 
#Na hili ni jambo ambalo Prosper alikiri kuwa yeye hakusoma chochote High school kama wengine bali alisoma lugha tu, ambayo hakuendelea nayo huko chuoni ili kuwa mwalimu au mtaalamu wa lugha#

HATIMAYE SAFARI YA KUJA JIJINI DAR IKAANZA…..
Na hivi ndivyo alivyokaribishwa Jijini

Na huo ndio muujiza wa kuja mjini na hata sasa haujabadilika maana makazi yamebaki kuwa jijini Dar….ndio alibahatika kujiunga na Chuo Kikuu Cha Dar es salaam na hapo alisoma Shahada ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa jamii (Bachelor of Arts in Political Science and Public Administration)
Mabibo Christian Fellowship ikiwa changa

Alipokuwa Chuo alikuwa mfano wa pekee wa kuigwa na Alikuwa anakaa Mabibo Hostel na hapo aliimarisha mfumo rasmi wa Mabibo Christian Fellowship ambayo hata sasa wanaifurahia wengi, yeye pamoja na wenzake wanahesabika kama waasisi wa MCF nay eye huitwa Babu wa Fellowship hiyo.
Hatimaye akahitimu Chuo Kikuu

Ni kweli alimaliza hapo lakini jambo la kipekee ni kuwa hajawahi kurudi tena baada ya kumaliza chuo hata leo na anachokifanya sasa hivi mtaani hakiendani hata kidogo na kile alichosomea.

KAZI
Mungu alikuwa mwaminifu sana kwake naye akabahatika kupata kazi nzuri sana, akafanya kazi kama COORDINATOR wa Japan Engineering Consultancy (JEC), kampuni iliyokuwa ikifanya kazi ya ushauri wa kiinjinia kwa mradi ulikuwa unafanywa na Japana International Cooperation Agency (JICA) kwa ushirikiano na Wizara ya Miundo Mbinu wakati huo, kazi ambayo aliifanya kwa miezi 27 na kuenjoy maisha kwa kina……LAKINI JAMBO LA KUSHANGAZA AMBALO ALINIAMBIA PROSPER NI KUWA; ALIPATA KAZI NZURI SANA YA KUMWINGIZIA MAMILIONI AKIWA HANA AKILI KABISA, MAANA HAKUWAHI KUFANYA JAMBO LOLOTE LA MAANA KATIKA KUJENGA KESHO YAKE ZAIDI YA KULA BATA MJINI, NAAM ILISHAPITA, HAJUTII SANA MAANA BAADA YA KUPATA AKILI SASA NDIO AKAANZA KUJIAJIRI HATA LEO.

Prosper Mwakitalima ni kijana mpambanaji mwenye ndoto za kuwa Billionea na katika harakati zake mnamo Sept 2008 yeye na baadhi ya marafiki zake wakafungua kampuni ya Printing iitwayo MANCON (E) Ltd na hapo wakaja na Product iitwayo “Gospel Today”….Hii ilikuwa ni Free Advertising Magazine yenye mlengo wa Kikristo na ilikuwa inatolewa kila mwezi na kwa bahati ya ujasiriamali ilidumu kwa miezi mitatu tu.
Prosper anasema…..Ingawa ile magazine ilitoka mara tatu tu, na tuliumia kushindwa kuendelea lakini ndio ulikuwa mlango na msingi mkubwa sana wa kazi nyingi sana za printing zilizokuja hata leo, maana watu walipenda sana Ubora na Ubunifu.
Pamoja na kuyumbayumba kwa hapa na pale kwa biashara change, sasa kampuni imesimama na wanaendelea na uchapaji wa aina zote….Kuanzia T-shrts, business cards,wheel cover mpaka Advertising boards….wenyewe wana msemo wao; MANCON (E) LTD….MAKES YOU SAY “WOW”
March 2009 alifungua kampuni nyingine ya IT iitwayo “THE BRIDGE” Inayo operate hata leo.
Kijana huyu amefanikiwa Kujitengenezea AJIRA yake na kuwaajiri wengine sita(6) na mbali na hao kuna wengine wengi waliosaidiwa sana kwa kujengewa uwezo na hawa ni kama kumi vile, mbali na wale wanasaidiwa kila siku kwa ushauri na mikopo.

KILA MTU MWENYE NDOTO HUWA ANAKUWA NA MFANO, MWONGOZO AU WATU AMBAO KWAO ANAJIFUNZA NA KUTIWA MOYO ZAIDI ILIMASONGE MBELE SANA, BASI NILIPOMUULIZA PROSPER YEYE ANAVUTIWA NA NANI ZAIDI(ROLL MODEL IN ONE WAY OR ANOTHER)
Prosper Mwakitalima akiwa na Paul Mashauri na rafiki yake

Naye akasema amesoma Vitabu kadhaa  na kuwa inspired na Robert Kyosaki sana and among the books, here are “7 Strategies for Wealth and Happiness”; “Who Moved My Cheese” and “The richest man in Babylon”…..na kwa hapa Tanzania amekuwa anamfuatilia na kumfurahia sana kijana mmoja anaitwa PAUL MASHAURI, Mwenyekiti wa East Africa Speaking Bureau…..prosper anasema “Anamfahamu sana toka zamani akiwa chuo na anamfurahia akiwa anakua kimaendeleo kila leo, na hata lile wazo la kuanzisha “Gospel Today” nilijifunza toka kwake.

NI IPI MISINGI YA NDOTO ZAKO?
Prosper alisema anaendeshwa na ndoto hii;
“…..I WANT TO MAKE JESUS FAMOUS!”,By raising people with God’s character “Christian Celebrities”, that is why I have invested in Media, I started in printing and now I am now going to Radio and TV.

Sifa Tanzania


CHANGAMOTO AMBAYO AMEISEMA ni kuwa “single”, anasema ukiwa Single unakuwa unbalanced!....japo amepitia changamoto kadhaa katika mahusiano(Rasmi kama tatu hivi) anasema akioa Mtakamatia mbali.

NILIMUULIZA PROSPER NI NINI MTU ATARAJIE KWAKE AKIHITAJI MSAADA?
Naye akasema Akija Mtu mwenye Ndoto/ Maono anaweza kupata mambo mawili matatu na PIA asiyejitambua anaweza kumsaidia Akajitambua.

NILIMUULIZA PROSPER, NI NANI UNATAMANI KUMPA SHUKRANI KWA SASA AMA KUUTAMBUA MCHANGO WAKE KWAKO MPAKA HAPA ULIPO?
Prosper alisema Anamshukuru Kila mtu aliyemsaidia kwa namna moja ama nyingine mpaka kufika hapo alipofika, lakini aliwataja hawa wachache kipekee na kusema hawa haachi kuwashukuru san asana kwa jinsi walivyo muhimu sana kwake( sio kwamba wengine sio muhimu bali hawa wana kibali cha pekee)
Alfred Mwakitalima na Nathanael Sasali(Wachungaji)

Kwanza anawashukuru sana Wazazi wake; Mama yake ndio mjenzi mkubwa wa maisha yake ya kiroho, maana yuko deep katika neno la Mungu na ni mwombaji sana; na Baba amemfundisha kuwa na utegemezi kamili juu ya Mungu na kuishi kwa imani, maana anasema hajawahi kumwona baba yake akiwa na hofu hata kuwa na nini.
Lakini pia alisema anawashukuru sana marafiki zake kama Andrew Mzava, Papaa, Mussa Bilageya, Jacob Mtalitinya na wengineo, lakini pia Anamshukuru sana Dk.Rev Huruma Nkone mchungaji wa Victory Christian Centre Tabernacle (VCCT) maana ALIMWAMINI SANA TANGU ZAMANI, na Imani ya mchungaji huyo ndio ilifanya hata watu wengine wengi wamuamini.
NA KWA SASA MARAFIKI ANAOTAMANI KUWASHUKURU NI HAWA;
(Na haya ni maneno yake mwenyewe)
Ninawakubali sana na kuwashukuru marafiki hawa kwasababu zifuatazo;

1.SAMUEL SASALI a.k.a Papaa

Prosper na Papaa
…..Ni rafiki mzuri sana tangu zamani na kinachonifurahisha kwake ni kuwa Ni mtu ambaye ni VERY APPRECIATIVE!!!...Yaani hata kama wengine hawaoni wala kukubali unachokifanya,lakini huyu amekuwa mtu wa kunitia moyo na kunikubali sana, nah ii inanitia moyo kusonga mbele kila siku.

2. KING CHAVALA (MC/COMEDIAN)
Prosper na King Chavala

….na huyu amekuwa rafiki ambaye ananikubali na kuniamini sana, na nampenda kwasababu ya Ushauri na ni mtu anaeona mbali na anajitambua……Thank you man for being appreciative hahahaha!
(Haya hakusema kwasababu nilikuwepo, lakini naamini anamaanisha toka moyoni)
3. AMANI PAUL 
Amani Paul
… na huyu amekuwa karibu sana na mimi kwa ushauri na kunitia moyo sana, na kwasababu naye ni mpambanaji basi tumekuwa naye karibu sana wakati tunaanza kujisimsmia kibiashara na hata sasa baada ya kupiga hatua bado ananichangamotisha.

PROSPER ANAWASHUKURU SANA MARAFIKI HAWA PAMOJA NA WALE AMBAO HAWAJATAJWA HAPA NA KWA NDUGU MSOMAJI NATAMANI UJIFUNZE JAMBO HAPA, HATA KAMA WEWE MWENYEWE HUJAFIKA MBALI SANA LAZIMA UJIFUNZE KUWAKUBALI WENGINE “APPRECIATE NEVER HATES”
PROSPER NI KIJANA AMBAYE ANAMPENDA SANA MUNGU NA ANAAMINI KAMWE HAWEZI KUFANIKIWA NJE YA MUNGU, NINAJUA KUNA VIJANA WENGI AMBAO WANAFIKIRI ELIMU, KAZI NA BIASHARA NDIO VINAWEZA KUWATOA NA WAKASAHAU MUNGU, AMBAYE NDIO KILA KITU KATIKA YOTE.
NA HAYA NDIYO YALIKUWA MANENO YAKE YA MWISHO KWA KILA MSOMAJI;
“Ishi kwa kujiamini, relax, Acha woga, Life is Adventure, Acha kuishi kwa kuwazia kula na kulala tu, lazima uwe na ndoto ambazo hata wewe zinakutishia….Think things that challenges You!”
AHSANTENI SANA KWA KUSOMA NA KUMFAHAMU VIZURI PROSPER MWAKITALIMA, NAAMINI UTAKUWA UMEJIFUNZA VYA KUTOSHA NA IWE NI CHANGAMOTO KWAKO KUJENGA MSINGI BORA WA MAISHA YAKO KAMA KIJANA!

Imeandaliwa na
King Chavala
+255 713 883 797
©Zooming Zone’2013