CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha!!


John Shabani:Mwalimu na Mwimbaji wa Injili aliyepitia magumu ya maisha.
John Shabani

JOHN Shabani si jina geni masikioni mwa watu hasa wapenzi wa muziki wa injili na wanafunzi wa muziki huo.

John mzaliwa wa kijiji cha Kirando katika kitongoji cha Nyankima, kata ya sunuka, Wilaya ya Kigoma Vijijini, anatokea katika ukoo wa waumini wazuri wa dini ya kiislam.

Muimbaji huyo ambaye umaarufu wake uliwika baada ya kushiriki tamasha la pasaka ambalo anasem akuwa liliinua uimbaji wake na anatamani kama atapewa nafasi ya kushiriki tena kwa miaka ijao ikiwemo mwaka huu.

Anasema kuwa historia yake baada ya kumaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi kirando, alijiunga na elimu ya sekondari, lakini kutokana na itikadi za kidini, alijikuta akiwa katika wakati mgumu wa kupigwa vita na wazazi, kwasababu ya uamuzi wake wa kujiunga na Dini ya kikristo hali iliyomsababishia muimbaji huyo kuishi miaka mingi akiwa mbali na wazazi wake.

Mwaka 1992, John akiwa kijana mdogo, alipata ufadhili wa kwenda nchini Kongo ambako huko alijifunza muziki na kusoma Chuo cha Biblia na ndipo kipaji chake cha kutunga nyimbo na kuimba kilijitokeza kwa kasi.

Muimbaji huyo anasema kuwa hakutaka kuona mtu yeyote akiwa katika hali ya kukata tamaa, maana alifahamu madhara yake kwasababu hiyo, alianzisha vikundi mbalimbali vya vijana akiwa na lengo la kuwaelimisha ili kujikwamua katika hali ya kukata tamaa na kutokujihusisha na vitendo viovu kama vile madawa ya kulevya, Ukahaba na anasa za kila aina mambo ambayo aliyapiga vita.

Shabani anasema kuwa ameishi miaka mingi kama yatima, lakini hali hiyo imemsaidia kujifunza mengi na kuwa na tabia njema, kumheshimu na kumthamini kila mtu, hali hiyo ilimfanya kupata kibali machoni pa wengi.

Anasema kuwa amekuwa msaada kwa vijana wengi ndani na nje ya nchi na kuwakwamua waliokuwa wamekata tamaa na kujihusisha na vitendo viovu.Pia kutokana na ujuzi wa muziki alioupata na kipaji alichonacho cha kutunga, kuandika nyimbo na kuimba, anasema kuwa amekuwa msaada kwa waimbaji mbalimbali binafsi na vikundi , hasa nyimbo za Injili.

Mwaka 2001 John alifunga pingu za maisha na Debora Shabani na mwaka 2002 walifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwae Joyce, akiwa na maana ya kuyasahau maisha ya huzuni na shida na kujitabiria maisha ya furaha.

Mwaka 2004, John aliajiriwa katika kampuni ya Msama promotions ya jijini Dare es salaam, kampuni inayojihusisha na kuinua vipaji na pia kuwainua vijana na watu wa rika na jinsia zote waliokata tamaa ya maisha na hasa wale walioko vijiweni wakijihusisha na madawa ya kulevya, ukahabaa

Albamu yake ya kwanza Marufuku kukata tama anasema kuwa imewasaidia wengi waliokata tamaa na kuwapa matumaini mapya albamu hiyo na nyingine alioirekodi mwaka 2009 zilizoitwa huu ni wakati wangu na Moyo wangu.

John ametembelea nchi mbalimbali, akijifunza maisha ya watu ikiwemo kugundua kwamba karibu asilimia kubwa ya wanadamu, awe maskini, tajiri, msomi au asiye na elimu, wenye vyeo au waajiriwa, watoto kwa wakubwa, wanaume kwa wanawake, awe mzungu au mweusi n.k, wote kwa njia moja au nyingine wamepitia katika hali ya kukata tamaa au kukatishwa tamaa na jambo fulani, mtu, watu, hali au mazingira fulani.

Ndipo mwaka 2006, alipata maono na msukumo mkubwa wa kuandika Kitabu ambacho kitakuwa msaada kwa njia moja au nyingine kwa kila atakayekipata. Kitabu hicho kinaitwa Marufuku kukata tama. Kitabu hicho pamoja na kile kiitwacho “Mafanikio yatokanayo na kusifu na kumwabudu Mungu” vinategemea kukamilika baada ya miezi miwili.

Mwaka 208 sitausahau  ilikuwa ni siku ya huzuni na majonzi, siku ya kilio na kuomboleza. ni siku alipofariki mke wake mpendwa na mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili, Debora Shabani, mwimbaji aliyegusa mioyo ya watu wengi ndani na nje ya nchi, niliumia sana lakini sikukata tamaa”anasema.

Shabani alitunukiwa tuzo ya heshima pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake kwa ajili ya kuinua vipaji na pia kuchangia kuinua muziki wa Injili Afrika mashariki na kati. Pamoja na hayo amekua akianzisha vikundi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu Tuzo anayosema kuwa ilitolewa na kampuni ya Christian promoters Ltd, Pia ni miongoni mwa waanzilishi na kiongozi wa Chama cha muziki wa injili Tanzania (Chamuita).

Mwaka 2011, John alipata heshima kubwa kama mwalimu, kuongoza kundi la waimbaji (Tanzania gospel all stars) kuimba wimbo maalum wa miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.

Anasema kuwa pamoja na mzigo mkubwa aliokuwa nao kwa kidogo anachopata,amehakikisha kuwa anaisaidia jamii, hasa watu wenye ulemavu, wajane na yatima Vijana waishio katika mazingira magumu, pamoja na wakimbizi. Tayari ameanza mikakati ya kusajili Taasisi Hope Foundation kwa ajili ya maono hayo.

Pamoja na malengo mbalimbali aliyonbayo Shabani, lakini pia ni kuwa na kituo cha watoto na vijana, lengo ni kuandaa kizazi chenye maadili mema, kuibua, kutambua na kuinua vipaji vya watoto na vijana, mbinu na mikakati ya kuwakwamua watoto

Pia anasema kuwa mpango huo unalenga kutafuta ufadhili kwa ajili ya kuaendeleza vijana kielimu pamoja na kuwawezesha pale inapobidi, kuandaa matamasha ya watoto na vijana, kuunganisha watoto na vijana wengine duniani, kuwapa kipaumbele watoto na vijana wenye elemavu, kuwa na kiwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali ya watoto na vijan.

Kwa sasa anajishughulisha na kufundisha bendi,vikundi na waimbaji binafsi na kusema kuwa lengo ni Kufundisha kuimba au kunyoosha,Jinsi ya kuitumia sauti kuitunza na kuitawala,  Historia ya muziki na maadhi ya muziki, Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora, Matumizi ya kipaza sauti,Kuwatungia nyimbo au kurekebisha nyimbo zilizotungwa tayari, Kutoa ushauri kwa wanaotatarajia kuingia studio, mbinu za kuitangaza albamu au nyimbo zikubalike na Kutengeneza muziki wenye viwango.


Papaa On Tuesday...Hata Ukizima Mshumaa Wa Mwenzio Haufanyi Wako Uwake Zaidi

Ninakila Sababu Ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya siku ya Leo kwa Kuweza Kutupa tena Uzima katika Maisha haya tuliyo nayo. Kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu,kuna rafiki yangu Zulfa alitoka kwenda Matembezi ya Weekend amepata ajali wamekata Mguu sasa ni Kilema. Hata kama hakuna aliyekufa ama kuwa kilema kuna Kila sababu ya Kumshukuru Mungu kwamba tunaishi.

Mwanamuziki Elton John akiwa na Bernie Taupin Mwaka 1973 waliuandika wimbo "Candle In The Wind" ukiwa maalum kwa ajili ya heshima ya Marehemu Marilyn Monroe. Maisha 


yetu ya kila siku kwenye dunia hii ni kama Mshumaa, Ka nafasi ulikonako hapo ofisini 
kwako ni kama ka mshumaa, sehemu ya biashara uliyopo ni kama ka mshumaa, maisha yetu

 ya kila siku ni kama Mshumaa ambapo mishumaa hii inatufanya kuwa nuru, Mishumaa hii 

inatufanya kufahamika na kukubalika kutokana na mwanga tunaoutoa, njia tunayoionesha

yenye kuleta mafanikio.

Ingawa Kila mtu ana mshumaa wake kuna wengine wamekuwa na jitihada mwamwi 

(Mwanzo Mwisho) kuhakikisha mishumaa ya wengine inazima ili ibaki peke yao kutoa 

mwangaza na kuonekana wao ni bora kuliko wengine. Kumulika kwako wewe na kutoa

mwangaza na kung'aa kwenye maisha kuna wanyima usingizi wengine, kuna wakosesha raha

 wengine, ukiuliza hasa kama kuna sababu ya msingi wala hakuna sababu ila tu yeye 

hafurahii mafanikio wengine wanayopata hata kama nae ana mafanikio lakini unakuta

 anahitaji zaidi. Maisha yenyewe haya yetu ya kila siku Unafukuzana na hela ya Unga, 

Ukipata hela ya unga unagundua Chumvi imeisha, unakimbiza hela ya chumvi ukipata 

umegundua pampass zimeisha kila siku ni mbio mwamwi lakini ajabu from no where kuna

 mtu hapendi mafanikio yako.


Kwa kadri ambavyo tumekuwa tukiwaponda wengine kwa kile wanachokifanya basi vivyo


 hivyo na sisi tumekuwa tupondwa mahala pengine kwa kile tunachokifanya. Kuna watu 

hawapendi mafanikio yako live live ama kuna wale wa Silent Killers ukipata tatizo ama 

baya likikufika wanakutana wanagongeana mikono wanasema "Tulijua hafiki mbali" wewe 

ni Mkristo au Muislam wa wapi unayefurahia kushindwa kwa Mwanadamu Mwenzio. Wewe 

umekuwa Mtu wa Kushangilia kwa matatizo ama kukwama kwa wengine??maisha ni 

Mzunguko zamu yako itafika tu.




Kwenye maisha nimekutana na Watu ambao bila sababu wananichukia, inawezekana hata 


wewe umekutana na watu ambao wanachukia mafanikio yako bila sababu. Akipatikana mtu

 akamuuliza pengine hata pasipo kufahamu akamuuliza "Inaonekena Stella biashara

 zinamuendea pouwa sana ndo maana ameweza nunua gari", basi huyu anayekuchikia bila

 sababu utadhani ndo ana majibu yako yote atasema "aaah wapi unadhani hela yake,

 kahongwa lile gari, umalaya tu hakuna kitu anafanya mjini.." huyu mtu anaongea sana

 negatives kuhusu wengine. Kila anachoulizwa cha kwako yeye anaponda mbaya anaongea 

negatives mwanzo mwisho, kama ni kazi ofisini anakuongelea vibaya mpaka wengine 

wanashangaa, anatamani kuzima mshumaa wako ili wake ubaki unawaka raha yake wewe

 ufukuzwe kazi abaki yeye ndo aonekane bora,ukiwa na tabia hiyo kwisha habari yako.


Kuna watu wanachukia mafanikio ya wenzao bila hata sababu, furaha yao wao ni kuona


 wenzao wana huzuni siku zote, ukikutana nao wanakupa pole mpaka machozi yanawatoka

 kumbe mioyo yao ina kung'ong'a, anachukia kila hatua ya maendeleo yako. Kwanini kuzima

 Mshumaa wa mwenzio ili uonekane wako ndo unawaka??maisha hayako hivyo, unaweza

 ukamfanyi mtu leo ubaya ili uonekane wewe ndo boss, unataka uonekane wewe ndo Alfa

 and Omega, jua kitu Kimoja wewe sio Mungu wa Kumpangia Mtu maisha yake inawezekana

 hujui kuwa unatumika kumuandaa hiyo unayomfanyia huyo mtu kuwa na future nzuri. 

Kumpiga teke Chura ni Kumsaidia Kuruka. Kama tunajisikia raha kuumiza mioyo ya watu ili

sisi tuonekane bora kuliko wengine. Kuna Wakristo kabisa lakini ni wanafiki wakubwa 

kutwa kucha kutamani wenzao wakwame ili wao waonekane bora zaidi.


Kwenye maisha tunayoishi nasema tena kumpiga teke chura ni kumsaidia kuruka kuna 

wengine wala hawajui kuwa wanatumika kuwaimarisha wengine kwa maneno yao, leo

 ukinisema pembeni kwa watu inakusaidia nini, kama kuna mtu unajua hafanyi vizuri kuhusu

 kitu fulani kwanini usimwambie??Kuna watu wao ni Ma-Master of everything kama redio

 moja maarufu hapa nchini wao wanajua kila kitu kwenye vipindi vyao. Tunatamani

 wengine wachemshe ili unachokifanya wewe kionekane kuwa bora. Huu sio Ukristo wala

 sio Uislam hata ma Ma-Budha hawafanyi hivyo ni Upagani wa hali ya Juu. Inakusaidia nini

 kumsema mtu kuzima mshumaa wa mtu wakati unajua Mshumaa wako hautafika mbali.

 Usilewe Sifa kwa sifa unazozipata leo, leo watu wanakushangilia sababu una hela ama una

 kipawa kila sifa iko kwako, kuna siku vitaisha kuna siku atakuja bora kuliko wewe kama 

wenzako walivyoachwa ndivyo ambavyp utaachwa, niliwahi kuandika Usitukane Wakunga

 wakati Uzazi Ungalipo. Usijione bora kwa Mshahara unaoupata kwa kazi ya sasa maisha ni

 kupokezana ndugu yangu. Mungu sio Filikunjombe mwenzako itafika zamu yake. Wewe 

wadharau watu sababu wewe unajiona bora kuliko wao, roho mbaya haojawai kupanda bei

 tangu imeanza kutumika zaidi ya kushuka bei, tafuta wenye roho mbaya kama wewe 

ambao kwenye maisha wamekuwa wakitamani wengine wasitokelezee wabaki wao kama

 miungu watu kama waliwahi kufika mbali, ukizima mishumaa ya wengine jua tu na wako

 utazimwa tena ghafla mno saa usiyodhani, maana kabla ya wewe alikuwepo mwengine

kama wewe.



Ipo haja ya sisi kama Vijana, Watanzania na Wakristo Kusaidiana, kuna watu wana mawazo

 ya ajabu sana wanaonaga eti ukimpa "deal" fulani eti atatoka, unaogopa kumtoa mtu??

unataka utoke peke yako basi wewe sio Mungu ukigoma kutoa watu utashangaa wanakupita

 wewe bado umesimama pale pale. Biblia inasema wazi ni heri Kutoa kuliko Kupokea,

 haijakataza kupokea ila heri ipo kwenye kutoa, Unavyotaka watu Wakufanyie kwenye

 Maisha Wafanyie wewe wengine, kama unataka Kutolewa kwenye maisha ukatoka, basi

 kwanza anza kusaidia wengine kutoka leo. FM Academia wana Chorus inasema "Aliyekupa

 wewe ndiye kawanyima wao, dunia mafungu saba" kuwa makini.


Think differently and Make a Difference, kumbuka Muosha huoshwa, Kila aliye mwalimu leo

 aliwahi kuwa Mwanafunzi.



Papaa Ze Blogger.

0713 494110.

SHUJAA WA KIDATOORGA ALIYEUA SIMBA!!!

 UKIMUONA UNAWEZA USIAMINI, LAKINI HUO NDIO UKWELI NA NILIMKUTA HUKO HYDOM, NILIVYOENDA SOME WEEKS BACK!
 NA HAWA NI WALIMBWENDE WANAOMPAMBA NA KUMHUDUMIA KWA HESHIMA HIYO!
YAANI MPAKA RAHA, NYUMBA NI YA ASILI, KILA KITU HUMO NI ASILI NA HATA HAWA WALIMBWENDE WAMEVALIA KIASILI!

HII SIO MOVIE NI MAISHA HALISI....NITARUDI KUONGEA KWA KINA KUHUSU UTAMADUNI HUO WA KIPEKEE AFRIKA!!

Le African Adventures!

Papaa On Tuesday......Mwanga Wa Mbalamwezi Haukaushi Muhogo!!


Nimatumaini yangu ya kuwa wote tu wazima na tunaendelea vema na shughuli zetu za kile siku.

Katika kabila letu la Wanyasa, chakula cha asili cha kikabila ni ugali wa muhogo pamoja na dagaa kutoka Ziwa Nyasa. Kwa mnyasa kupata chakula cha namna hii basi unakuwa umemfikisha nyumbani kabisa kuliko kumpa chipsi mayai au kitimoto na ndizi. Nilipokuwa kijijini wakai fulani niliona jinsi mihogo inavyokaushwa, akina mama wa Kinyasa watajihimu asubuhi kuimenya mihogo hiyo na kuiloweka kwa muda kisha kuwekwa juani ili iweze kufaa baadae kwa kutwangwa kisha kupatikana unga wa muhogo wenye kupikwa ugali hupatikana. Kuna familia zingine ukifika wakati wa jioni huanua mihogo hiyo kwa kuiweka ndani kuhofia isiharibiwe na wanyama ama hata kuibiwa pia maana ndo deal kwa familia zilizokuwa zinaaminika kwa uchawi walikuwa wanaacha tu anayeiba yatamkuta ya kumkuta. Siku moja nikamuuliza Marehemu Babu yangu "Kwanini Wengine wanatoa Mihogo kuingiza ndani"?akaniambia kule kijijini kuna msemo wanautumia "mwanga wa mbalamwezi haukaushi muhogo". Nilitamani kufahamu maana ya msemo huo wenye kubeba maana kubwa sana nyuma yake.

Kuna mambo ambayo kwenye maisha huwezi yabadili ni kama kutaka kulazimishia mwanga wa mbalamwezi ukaushe mihogo, mihogo yake ni jua. Kuna watu wana tabia ya kulazimishia kufanya mambo wasiyo na uwezo nayo. Yaani unataka kufanya mambo ili watu wakukubali kuwa wewe mambo safi, unataka watu wakuone na wewe uko juu una Samsang Galaxy wakati matumuzi yako ni kupiga simu na kutuma SMS, unapiga picha event moja kesho una delete picha hizo hizo kuweka event ya pili. Kwenye vikao vya harusi walizojaa marafiki zako unatoa ahadi kubwa kubwa za harusi uonekane na wewe mambo safi. Kuna mambo ya mbalamwezi kuna mambo lake jua ndo yanaenda.
Kwanini unataka uishi zaidi ya vile ya ulivyo, kwanini unaishi maisha ya kujitahidi??kwanini usiishi vile ulivyo kwani unapoteza nini unapokuwa unaishi maisha yako ya kawaida. Hii tabia ya kutembelea kwa watu kishaukakuta wenzio wana flat screens na wewe ukataka, ukakuta wana Sub Woofers za Ukweli mwisho wa siku na wewe ukataka, Ukaenda kwa watu ukakuta wana Kengere na wewe ukataka, ukakuta mtu ana BlackBerry na wewe unajinyimaaaaaaaaaaaaaa eti na wewe uonekane upo kwenye Class kama uwezo wako ni kutoa mwanga basi usitake kukausha mihogo kuna mambo hayawezekani kwa sasa wala baadaae kwanini uyalazimishie?

Kizazi chetu kimekuwa na changamoto sana eneo mojawapo lenye kuleta changamoto ni kuoa na kuolewa. Unakuta saa nyingine kuna watu wanawafukuzia watu mpaka wanakera, na siku hizi wanawake wenye uwezo wamekuwa ni sababu ya kunyang'anya wanaume wa wanawake wasio kuwa na uwezo na wanaume wenye tamaa wamejikuta wakidondokea kwenye mikono ya wanawake mabaradhuri. Fedha ina ushawishi, fedha inatakatisha, fedha ni jawabu la mambo yote sababu ya uwezo wa mwanamke kuweza kumudu kununua mambo yanayoweza mfanya mwanaume aonekane nae katika jamii wamejikuta wakiacha mapenzi ya kweli na kuingia kwenye tamaa, kuna rafiki yangu amehongwa gari, gari kabisaaa lakini jamaa hana uhuru kabisa, kuna rafiki yangu amehongwa chain ya 1.5 Milioni na Blackberry juu lakini anafungwa kupita mbwa wa kizungu, inakufaidia nini kupata kila kitu na huku unapoteza mpaka uhuru wako wa kucheka, unayemcheka fulani unaulizwa, unapomtazama mtu mara mbili unaulizwa why?ni mara kumi kuwa na simu ya kitochi na kubaki na mapenzi ya kweli. Kuna wanawake na wanaume wako tayari kufanya chochote wanachoweza kutimiza tamaa zao za mwili, unaweza kupewa nyumba bure, unaweza kupata gari bure, unaweza kupewa investment bure lakini huwezi kupata amani ya kweli na uhuru wa kweli for free, kama unajua uwezo wako kutoa mwanga usitake kukausha mihogo.

Heshima ni kitu cha bure sana, lakini nani anataka kutunza heshima yake, rafiki yangu aliwahi niambia "Papaa tangu nimeanza kutunza heshima haijawahi nisaidia". Kwani unataka utunze heshima ili iukusaidie?kuwa na heshima ni msaada mkubwa sana kwenye maisha, kujiheshimu, kuheshimiwa, kushemiana ni jambo ambalo naona sasa linapoteza mkondo wake watu wanakuambia its a matter of time itashuka leo kesho watu wanasahau, leo unafanya jambo la kusikitisha jamii lakini kesho heshima inarudi mjini, katika kila uovu kuna mtu wa kukutia moyo. Mwenye mbili havai moja, na mwanga wa mbalamwezi hata siku moja hauwezi kausha mihogo, lina heshima yako ili uheshimiwe.

Kufikiria kutumia mwili wako kupata kazi, kufikiria kutumia mwili wako kupata gari ama nyumba basi jiandae tena kutumia mwili wako kupanda cheo, jiandae mwili wako kupata nafasi ya kwenda kusoma, jiandae kutumia mwili wako ili usipunguzwe kazini, jiandae kutumia mwili wako kupata hela ya mafuta, jiandae kutumia mwili wako kufanya service ya gari, jiandae kufanya chochote kutumia mlango ulioufungua kwenye maisha yako, kama unajua wewe ni mbalamwezi usitamani kazi za jua kila jambo lina makusudi yake hapa duniani.

Kila mtu atavuna alichopanda haijalishi unapanda hadharani ama gizani, mchana jua humulika na usiku mbala mwezi hutoa mwanga. Mwanga wa mbalamwezi haukaushi muhogo.

Think differently and make a difference 

....//Papaa
0713 494110

TERABYTE LOVE (UPENDO BABKUBWA)......Part 1


Always Quality love is for Quality people!
UTANGULIZI;
......Ninakuletea cha kijana mmoja msomi mwenye shahada mbili alizozipata ughaibuni, mtaalamu ya falsafa, mtoto wa Mtumishi mkubwa wa Mungu mwenye heshima ya pekee katika jamii,Askofu wa Pentekosti ambaye pamoja na upinzani na maroroso yooote ya jamii yake alimpenda na kuamua kumuoa Dada mmoja fundi cherehani, mlutheri aliyedharaulika na ni mlemavu wa ngozi (Albino) na hata sasa wanaishi pamoja kwa furaha....unajua ilitokeaje tokeaje? Basi ungana nami taratibu tujifunze kupitia hadithi hii!
.............SIJAWAHI ONA UPENDO KAMA HUUUUUUU!

ENDELEA SASA.....
Katika maisha yangu ya pita pita hapa na pale nilikutana na jambo ambalo lilinishtua kibinadamu maana sio kawaida na nikatamani kupuuzia na nikaenda zangu,lakini nilipoondoka niliendelea kujiuliza hivi kwanini sikufuatilia kwa kina? basi tena siku zikaenda na jambo lenyewe likawa limepotea kichwani kama vile tamthilia inavyokwisha.

Basi nikajifariji ya kuwa ni jambo la kawaida tu na yamkini ni hisia zangu tu au ni maneno ya watu katika huo mtaa, maana watu nao wana visa hatari aisee!
Basi siku zimeenda na sasa imepita miaka mitatu, nikiwa nimemsindikiza mwenyeji wangu hospitali maana alijikata na bati wakati akitengeneza banda la mbwa wake, baada tu ya kupaki gari kwa mbali nikamuona kama ni mtu ninayemfahamu kwa mbali, lakini nikajiambia anyway yamkini nimechanganya tu habari, basi tukaingia hospitali na huyo ndugu yangu akasafishwa na kushwonwa na hatimaye kufungwa na pamba vema kabisa.....sasa wakati huyo ndugu yangu anasubiri kuingia theatre ili akashonwe maana palikuwa ni pakubwa sana, basi mimi niliamua kujipa tour ndani ya ile hospitali kubwa ya mkoa, ili nione ni kwa namna gani imejengwa na kupangiliwa, basi nikapiga mizunguko ya kutosha, niliporudi kwa rafiki yangu, nikakuta bado hajatoka, ndio hapo nikajiambia ngoja nikatishe kwenye moja ya mawodi, basi wakati napitta hivi mara nikamuona Dada, kimsingi ni mama kwasababu alikuwa amejifungua watoto wanne kwa pamoja na hapo kila mtu alikuwa anamshangaa na kumpiga picha, hususani waandishi wa habari, basi na mimi ikanibidi nisogee karibu kuangalia, jamani kumbe huyu mama ni albino lakini mbona amejifungua watoto wote wana ngozi nzuri kabisa (yaani wasio albino)?

Basi nikahisi kama vile anasumbuliwa sana, na hapo nikaamua kuingilia kati na kujipa majukumu ya kuwaondoa waandishi wa habari na watu wote waliokuwa wakimshangaa katika chumba kile....haikuwa kazi rahisi sana, lakini baada ya mivutano ya kutosha, basi nikafanikiwa kuwatoa wote.

Sasa walipokuwa wameondoka, mara nikaona mtu mmoja anaingia ndani na hapo nusura nimbamize kofi maana nilidhani ni mmoja wa wale waandishi wasumbufu, basi nikashangaa tu nimekaa kimya na sisemi kitu, akafika pale akamwangalia yule mama kisha machozi yakamtoka na hapo akapiga magoti pembeni ya kitanda na kulia sana sana, na hapo kuna waandishi walitaka kulazimisha kuingia kana kwamba kulia kwa ndugu huyo nayo ni habari.
basi mimi nikabaki nimeduwaa maana simjui huyu dada au mama kwa jina wala kwa lolote na huyu naye ameingia na kuanza kulia, sasa nikajiuliza huyu kaka anahusianaje na huyu dada? na hapo nikaanza kuwaza...labda huyu kaka amewahi kujaribu kumfanyia ubaya dada huyo hivyo anajutia, au amewahi kumuokoa katika janga fulani hivyo anafurahi kwa kuona huyu dada ni mzima pamoja na matishio mengi sana ya kuuwawa kwa albino.

Sasa hapo nikawa natamani sana amalize kulia haraka ili nimsemeshe kidogo lakini haikushindikana, na hata huyu maana alikuwa kimya muda wote akinishangaa tu maskini, basi wakati nataka nikae tu,simu yangu ikaita na kupokea alikuwa ni yule rafiki yangu aliyekuwa kushonwa  na akadai amemaliza kwa hiyo anataka tuondoke zetu.......sasa hapo nilitamani nijue chochote kitu lakini haikuwezekana, basi nikatoa kadi ya mawasiliano (business card) ili nimpe yule mama, lakini akagoma kabisa kuipokea, na mimi niliwapenda sana watoto na ile adventure ya albino kuwa na watoto wanne kwa pamoja, sikuelewa kama amenifurahia au nimemboa, aana nilishindwa kutafasiri sura na ule mwangalio wake kwangu, nilitamani sana kujua stori ya maisha yake na zaidi kujua anajisikiaje, na kwakuwa alikuwa hasemi kitu, nikatamani kujua je mtu huyu ni bubu au anaongea? au ana aina fulani ya udhaifu na akilini pia, lakini wakati naendelea kujibaraguza angalau nijue mawili matatu, simu ikawa kero maana huyu rafiki yangu naye anataka kuondoka haraka, na hawezi kuniacha kwasababu funguo ninayo mimi, basi nikaamua kuondoka zangu huku moyoni nikidhamiria kuwa lazima nilete zawadi kwa watoto na mama huyo maana mimi binafsi napenda sana mapacha, Na niliamini ipo saa tutakutana tena kwa karibu na mimi nitasema nae kwa kina kuhusu maisha yake, yamkini nikapata jambo la kujifunza maana pia mimi ni mtu ninayeamini kwenye uhalisia wa maisha na sio hayo maigizo,basi nikaaga zangu (Japo sikupata muitikio wowote, japo wa macho tu) na wakati ndio natoka tu nilipofika mlangoni, wakati nafungua tu mlangoni NILISHTUKA SANA, nusura nianguke kwa mshtuko na mshangao maana punde tu bila kutarajia kabisa nikagongana uso kwa uso na ...................ITAENDELEA!!

(Je unajua niligongana uso kwa uso na nini? Unaweza ukajitahidi kuhisia kodogo?,Unafikiri yule kijana ni nani na alikuwa analia nini? basi tuonane hapa weekendi ili nikujuze hasa nini kiliendelea baada ya hapo.....TOA MAONI YAKO PIA.....Usijaribu kukosa!!!)

HABARI HII INAKUJIA KWA UDHAMINI MKUBWA WA Chavala Ideas Platform <http://chavalamedia.blogspot.com>
(c)2013

Na
King Chavala MC
+255 713 883 797
lacs.project@gmail.com
Facebook; King Chavala MC
Twitter @kingchavala
http://kingchavala.blogspot.com

Chavala Ideas Platform to launch "LADIES TALENTS BATTLE" on 13rd OCt 2013 in Dar!!!




“LADIES TALENTS BATTLE” Series
IDEA CONCEPT NOTE
What is it?
This is the special project aiming to discover, nature, nourish, brand and place on market board, different talents such as singing; playing different music instruments; dancing; dramatizing; fashion and designing; story telling; poetry; comedy; moderation and all other natural talents that are lying within ladies’ natural potentials along with spreading the good news, new hopes and new motivation to themselves (Ladies at large) and the whole community concerning different sensitive issues that are termed as challenging challenges within the society of ladies and at the end to leave them with clear understanding and confidence about themselves for the Glory of Kingdom of God.

Why is it?
Because they have talents and their talents are real, why not creating the room/platform for them to manifest fully?.... Yes! no more hiding, no more trying, it the time to it for real! Personally I believe that giving them a unique and zoomed platform for them to show what they have, it will encourage many of them who are still hesitating to start doing something; it will enforce those who are doing to be more serious and it will give the society a special eye (consideration) to them.

Why now?
It has to be done now because the right time is always now and the vision has come very clearly for now generation. In the other side there are several groups of NGOs, world religions and the so called Gender activists are very busy feeding our ladies with negative information, negative beliefs and negative perspectives about them and that may yield the society of lesbians and women who has completely negative perceptions toward their husbands if they got married, and so we ought and we must do something for the sake of our future. One Wiseman said “The triumph of evil grows when good people are doing nothing”

How will it be?
All of our activities in this project will be done in a form of a special campaign by which there will be special Concerts and tours in different places such as churches, schools and higher learning institutions. Furthermore there will be a special TV program/show that will comprise different issues including feedbacks of concerts and tours from different fields, hope that will help millions of ladies to be informed all over the country. There will also be a magazine and small bulletins with different information that can help them read slowly and understand.


Where to be done?
It is to be done in Tanzania and we have choose to start in the largest city of Dar es salaam; all activities and tasks will be done in Tanzania and all requirements we need will be found in Tanzania, Local media to be used and the magazine and bulletins will emanate from Tanzania.

Objectives;
There are vast of objectives but here are major of them;
v  To discover, nature, equip, coach, exercise, brand and market all the natural talents that are lying within ladies potentials
v  To zoom and place different ladies with different potentials on top where everybody can see, and thus whoever will be in need of such potentials will easily sight out.
v  To equip them with truth, moral and our country’s civilization as they grow and understand more about themselves and their roles in their society.
v  Life coaching; Carrier guidance and individual capacity building
v  To nature and produce true patriot of African natural beauty, who are futuristic and have bet to remain pure until when they got legal permit (Marriage)
v  To prepare brave leaders who can stand for what they know and believe is true and legitimate, ladies who can utilize the ample of their potentials to educate themselves and others in the society and the whole society at large.

Expectations;
To see ladies who are proud to be who they are, proud of their talents and other potentials that they have, ladies who can’t abase themselves and can’t compromise to ungodly matters; ladies who can’t trade their humility such as offering sex in order to get what they deserved to get by just who they are such as Jobs that they are qualifying to, pass mark in schools and access to different leadership posts. To see ladies who are proud of their natural African beauty, patriot of their culture, ladies who have pledged to remain pure and the one who have aimed to be good women and best wives in future; To see ladies who will say NO! to western cultures and abase whites’ civilization which abuses our civilization, ladies who will work hard than harder and not ladies who will wait to receive from men because that might be very lazy society.

Participants;
Everybody in our society has to be part of this project for the results of it will benefit the whole society….let the church be ahead in praying for them and wishing good for them to succeed……let ladies with different talents and potentials be ahead on stage and others be down watching and learning from them and from what they are doing…let others support the project in all spheres such as financially, morally, intellectually and psychologically….let the parents encourage their children especially their daughters to work hard on their talents and to have sense of future with whatever they are doing….let the government support them by any means possible and practical……let the media be ahead on promoting such talents and airing the contents of presentations and the society as the whole will be participating by altering positively what they have learned!

Author’s note
This is the vision that has come to me very clearly that we have to do something to support this natural potentials which most of them are living unutilized and are buried unleashed. It is true that there are different few platforms where gifts and talents are being natured and traded but that is not enough compared to reality, it is the fact that female mankind is bigger that male mankind but in manifestation of different potentials female mankind are not clearly seen while they are the one who shape the future of any society for what they feed their babies;
 Sex business, drug abuse, moral deterioration, early pregnancies and artificial beautification is the result of Identity crisis among our people including this group (ladies) now we can’t just stay idle complaining but we have to do something about it, I believe if female mankind will be empowered, motivated, natured and well informed then the whole society will be strong and futuristic. It is my desire to see different gifts and talents by Tanzanian ladies excelling and shinning out to the world, promoting our country, our culture and our God!
Personally I have strong trust over ladies and women for my mother has proven it into my life, I have seen the need (other call it a challenge), I have sited out a solution and I am ready to invest my intelligent, my creativity, my time and my finance over this matter just to see a better futuristic society that will cater, maintain and keep our true values in generations to come for the sake of the Glory of God in Tanzania.
It might be very minute to the world but I am sure it will mean a lot to someone who will be the beneficiary of this project, I won’t stay idle complaining to issues that I am capable of doing something, so no matter what I will do something anyway and THIS IS IT…my purpose is my destiny, I am a solution to whatever challenge that counterfeit with my natural potential, YES! I live for mankind!

Conclusion;
Hope the idea is clearly understood and you are already challenged and you are thinking to do something, Yes! This is the right time and you must do something that is lying within your capacity. Whatever opinions, advise and contributions that you think can be of great importance to this project, please you are welcome and above all you are very invited to be part of this new movement.




Idea & Concept note by
Chavala Ideas Platform
Fredy E. Chavala <King Chavala-MC>
+255 713 883 797