CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797

CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
YES!!! SEPTEMBER IS JUST HERE!!!...THE NEW TERM IS ABOUT TO BEGIN.....YOU ARE ENCOURAGED TO BRING YOUR CHILD BEFORE THE CLOSURE OF REGISTRATION!!!....HOTLINE +255 716 230441

Christina Shusho Atwaa Tuzo Ya Mwanamuziki Bora Kutoka Africa Mashariki Katika "Africa Gospel Music Awards"


Hatmaye Kampeni Zilizokuwa Zikiongozwa na Media Mbalimbali Za Kikristo na Kipindi Chako Bora Kabisa Cha Chomoza Ya Clouds Tv zimezaa matunda baada ya Mwanamuziki wa Injili Kutoka Tanzania, Christina Shusho kufanikiwa Kutwaa Tuzo ya Inayowahusu Wanamuziki wa Injili Africa almaarufu Africa Gospel Music Awards.

Christina Shusho anatwaa Tuzo ya Pili kubwa baada ya Mwanzoni mwa Mwezi July Kutwaa Tuzo nchini Kenya kwenye Tuzo za Groove Awards zinazofanyika nchini humo, na katika Tuzo za Africa Gospel Music Awards Shusho alikuwa akishindanishwa na Wanamuziki 6 Kutoka Kenya, Wawili Kutoka Uganda na Mmoja Kutoka Tanzania yaani Martha Mwaipaja.


Katika Usiku wa tarehe 7 July, 2013 wakati Shusho akitangazwa kwenda Kuchukua Tuzo hiyo hakuwepo nchini Uingereza bali Blogger Maarufu Tanzania mwenye Kumiliki Blog ya Gospel Kitaa Ambene Michael aliyeko nchini Uingereza aliwakilisha vema upokeaji wa Tuzo hiyo ya Shusho

Kushoto  ni Blogger Ambene Michael aliyepokea Tuzo Kwa Niaba ya Shusho Nchini Uingereza


Viva Shusho Viva Tanzania.

#...NI MARUFUKU!!#(04)......KUFANYA MAREKEBISO JUU YA JAMBO LA KUAZIMA BILA RUHUSA!!!!

#.....NI MARUFUKU KABISAAAA#
Ni marufuku kabisaa kufanya mambo au marekebisho au matengenezo usiyoruhusiwa juu ya kitu au jambo la kuazima bila ruhusa ya mwenyewe!
Kwa kawaida kitu cha kuazima hakina uhuru wa kutosha,kwani umepewa kwa kipimo....waswahili wanasema...."Nguo ya kuazima haisitiri Matako"
Kuna mambo mengi tunajiamulia wenyewe juu ya vitu vya kuazima na kwa kweli huwa inakuwa sio sawa,kwa mfano;

a)Mtu anakuazima simu yako aongee na mtu mara moja maana yake imeisha airtime ambayo nayo alikopa na hapo mlipo hamna access ya kununua....sasa unakuta mtu baada ya kupiga kwanza anaanza *102#....hivi hicho ndio umeomba au? na haishii hapo unakuta ameongea na simu zaidi ya hata alivyoomba yaani unakuta mtu kajiachia kama yake vile na bado credit ikiisha na kwako eti anakopa na anapiga tena mpaka na hiyo inaisha na hapo hajakwambia kitu...sasa wewe unashangaa ukitaka kupiga yule mrembo anakwambia....hauna salio la kutosha kupiga simu...basi unanunua vocha faster....unashangaa message.....Ahsante kwa kulipa deni.....na bado unadaiwa ......ahhhh dah sasa ndio nini hivi?
Hapo ulipokuwa umemuachia basi kapiga picha,kafungua na picha zako na mpaka bundle yako ya internet imeisha eti kisa anadownload miziki...Sasa wenye tabia hiyo nawaambia Marufuku,acheni kuwakwaza wenzenu,mimi tabia ya hata tu kuazimana simu wala sioni kama ina mashiko sana kipindi hiki ambako simu ziko tele na mawasiliano ni rahisi kwa yeyote!!!.....Umewezaje kununua simu na unashundwa kununua vocha??

b)Mtu anakuazima gari na unampa kwa roho safi tu,halafu anakwaruzana huko na kikimbiza gari gereji mchwara huko wanaanza kukuharibia gari hali angekwambia wewe una fundi wako unayemwamini,sasa anafanya hayo yote na hasemi,wewe ukija kushtuka siku moja unakuta some spears kwenye gari hazipo....ama mtu anakwenda huko halafu anakutana na stickers basi ananunua na kubandika kwa gari yako....hivi umeazima gari yangu ukanipambie au utumie na kuirudisha,tena mbaya zaidi eti mtu anakuwekea masticker ya kipepo kabisa na yeye anafurahia...sijui Majani,Kappa au Monster Power...jamani Ni Marufuku kabisaaa,ukiazima kitu kirudishe hivyo hivyo na usijifanye wewe ndio mwenyejiiiiiiiii

c)Mtu amekuja kwako kukutembelea may be anakaa wiki moja au siku kadhaa,kwa kuwa ni mgeni hapa ni nyumbani pa kuazima...sasa unakuta mtu anaanza kupanga na kupangalua mara kochi hili ageuzie kule,pambo hili aweke kule yaani wewe ukitoka kwa mishe mishe unakuta everything has changed,jamani hapa kwako? hata kama umetamani kunisaidia kwanini usiniulize? unajua kuna saa mnavuruga mahusiano ya watu hivi hivi,yaani mwenyewe mlimbwende amepanga na kupamba na umekubali for sake of love halafu huyu mfukunyuku anakuja na kuharibu kisha anaondoka,unafikiri akija huyo mlimbwende siku moja unamwambiaje kama sio dharau hiyo!!!!

Ipo mifano mingi sana,lakini nimesema marufuku tena marufuku kabisa!!
HESHIMU MIPAKA YA CHOCHOTE UNACHOPEWA,SIO UNAKARIBISHWA SEBULENI WEWE UNAENDA MPAKA CHUMBANI AAAAH!!
......Sema neno na wewe kama tumeelewana!!!

N.B;Hii ni kwa faida ya mahusiano na urafiki wa ko na watu,na hii inawahusu watu wenye akili timamu tu na wanaojielewa na kujitambua!!

@Kwa hisani kubwa ya Chavala Ideas Platform <http://chavalamedia.blogspot.com/>
(c)2013

Papaa On Tuesday.....Tofauti Ya Kuweza na Kutokuweza Ipo kwenye Kuamua


Tunakila sababu ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya siku hii ya leo ya Jumanne ya kwanza kwenye nusu ya pili ya Mwaka 2013, mwaka umeisha ingia nusu wenye kumaliza vyuo wameshamaliza, wenye kuendelea wanaendelea wenye kusoma wanakazana, wenye mipango ya biashara wanakazana, wenye kuanzisha familia  nao wamo wapo pia ambao mpaka sasa hawajajisoma wapo wapo tu yamkini wala hawajui kama na Obama alikuwepo nchini kwetu.

Miaka michache iliyopita niliwahi kuwa na Supervisor Mchina ambaye tulikuwa na kawaida ya kukutana Dept yetu na ku-plan mambo ya wiki na pia kupitia report za utendaji kazi. Ninakumbuka siku moja tukiwa kwenye kikao alichora duara mbili moja ikiwa kubwa na nyingine ndogo ikiwa ndani ya ile kubwa. Namkumbuka Mr. Charles Guo aliniambia duara la nje linaitwa "Uwezo Halisi" na duara la ndani linaitwa "Uwezo wa Sasa". Tofauti ya Kile unachokifanya sasa na Kile unachoweza Kukifanya sasa kipo kwenye kitu kinaitwa "Kuamua". Nakumbuka alitumia mfano huo wakati tunaongea issue za Performance Management alisema Watu wengi sana wanafanya mambo mengi sio katika Uwezo wao halisi, Uwezo walionao kutenda ni Mkubwa zaidi kuliko kile wanacho kifanya na kinachotofautisha kile wanachokifanya sasa na Kile ambacho wanaweza kukifanya kinajengwa na tofali kubwa lenye kuitwa "KUAMUA KUFANYA". Kuamua kufanywa kunaletwa na Kichochezi (motivation) ama Catalyst ama sababu ya mtu kufanya ndio maana kwenye makampuni kuna incentives mbalimbali ili kuchochea uwezo wa wafanyakazi kwenda extra mile.

Wiki hii katika Ujio wa Rais wa Marekani nimekumbuka sana mfano huu wa Supervisor wangu kuwa mambo mengi sana ambayo tunayafanya sasa kumbe tunaweza kufanya zaidi ya pale tunapofanya ambapo ndipo kwenye uwezo wetu halisi iwapo tu TUTAAMUA kufanya kikamilifu. Wiki hii nimeshuhudia jiji la Dar-es-Salaam likiwa safi na likiwa halina foleni zisizo na sababu, barabara za katikati ya Jiji zinapigwa deki usiku na Mchana, Jiji limekuwa safi na Salama likarudisha maana halisi ya Jina tulipopewa na Sultan kutoka Oman kuwa ni "Haven Of Peace" ni "Bandari Ya Salama". Nimeona Watu wakilindwa usiku na Mchana kila kitu kimekaa kama kinavyopaswa, wamachinga wameondolewa kwa nguvu kupisha Obama apite, Barabara ya Ubungo pale kwenye Mataa ilikuwa na Makorogeshi ya Kutosha pametengenezwa usiku na Mchana taa zinawaka vizuri kumbe uwezo wa kufanya tunao sana iwapo tu tutaamua kufanya sisi kama Watanzania pasipo ujio wa Obama.
Kinachofanywa na Serikali ya Tanzania ni Reflection ya Maisha halisi ya Watanzania kama sio Waafrika kwa Ujumla. Nakumbuka Wakati ninasoma mpaka Chuo Kikuu ile wiki ya Kuelekea kwenye Mitihani ndipo unaona watu sasa ndo wanashika vitabu kisawasawa kumbe unajiuliza swali kwanini mtu anakesha namna hii kumbe alikuwa hajaamua kusoma, kama angeanza semester wakati inaanza yamkini maisha yake ya kusoma yangekuwa yako mbali uwezo na upeo wake ungekuwa wa kutisha lakini ajabu ng'ombe analishwa siku ya mnada. Sisi ni watu ambao kwenye nyumba zetu kuna vyombo ambavyo havitumiki mpaka waje wageni, hata kama mtakuwa hamna wageni miaka 800 lakini kuna glass ziko kwenye kabati, kuna sahani ziko kwenye kabati ambazo wenyeji hawazitumii mpaka aje mgeni utashangaa mgeni akija nyumbani ndipo siku hiyo mtakunywa na soda, ndipo siku hiyo mtatumia sahani nzuri, ndipo siku hiyo mtapelekwa kuoga mchana, ndipo siku hiyo utaona mpaka goti la mkeo ama mama akiwakaribisha wageni kwenda kuchukua chakula ajabu ni kwamba Mgeni ama wageni wakisha ondoka tunarudi katika maisha yetu yale yale ya sahani za plastiki na soda za sikukuu kumbe kuna siku tukiamua kama familia tunaweza kula kama kuna wageni na hakuna madhara.

Ninakumbuka enzi hizo ninasoma shule ya Msingi ilikuwa siku kama kuna wakaguzi wanakuja ama mgeni fulani kututembelea siku hiyo bustani zote ndipo zitatifuliwa, zitamwagiwa na kupendeza, kwaya ya shule itafanya mazoezi ya nyimbo za kumpamba mgeni rasmi mpaka atajiramba kwa sifa, tabia hii ipo kwenye nyumba zetu za Ibada na Makanisa penye ugeni tutafanya zaidi ya kawaida hata sare tutashona, tabia hii ipo kwenye maofisi yetu, tabia hii ipo kwenye familia zetu, zipo kwenye mahusiano ya boyfriend na girlfriend na wachumba uwezo wa kufanya zaidi ya kile unachofanya sasa na kuzorotesha ndoa yako upo kwenye KUAMUA. Kwneye maisha yetu ya kawaida pia kuna watu ambao hawavai vizuri mpaka wawe na ugeni hawasafishi vyumba vyao mpaka siku akisikia anatembelewa, hawabadilishi mashuka na mapazia mpaka uwepo ugeni haya mambo ndiyo ambayo yapo kwenye Jamii yetu tofauti ya kile tunachokifanya sasa na Uwezo wetu wa kufanya upo kwenye Kuamua.

Kila mtu anaujua uwezo wake wa kufanya zaidi ya kile anachokifanya sasa lakini tatizo hujaamua kufanya, yamkini unaimba, yamkini ni mwandishi, yakini unasoma, yamkini ni Mwajiriwa ama Mwajiri kile unachokifanya kwa sasa kama ukiamua kikweliii ukaweka miguu yote ndani ya hicho ukifanyacho basi ungekuwa mbali kupita maelezo. Inawezekana unachukulia pouwa kile unachokifanya kwa sababu hujaamua kwenda extra mile, assume leo ukaamua ubadilike ubadilishe aina ya huduma unayofanya, ukaamua leo upate feedback ya kile unachokifanya uone watu watakuambia nini yamkini unafanya kitu ambacho kinakuharibia biashara yako, yamkini unaweza ukawa unafanya jambo chini ya kiwango ambacho wateja wanategemea ukijichunguza kiukweliii unaweza kufanya zaidi ya hicho unachofanya. Leo hii ukiamua ufanye kwa uhalisia wako uwezo wako wa juu kabisa kufanya unadhani utakuwa wapi, leo hii nikaamua kusaka news kwa uwezo wangu kikweliii ninaweza kuwa na gazeti la Gospel Today, leo hii ukaamua kuboresha ndoa yako kwa uhalisia wake utafurahia ndoa yako, ukiamua leo kuongea na Wateja unaowafikia kwa biashara ama huduma yako unadhani wataongea namna gani yamkini kuna kazi umewahi fanya ukaharibu na yule uliyemfanyia amekuwa wakala wa kusambaza uharibifu wa kile ulichofanya kwenye kazi yake, yote yawezekana kwenye maisha UKIAMUA.

Tofauti ya waliofanikiwa na kwenye maisha na wale wasiofanikiwa ipo kwenye KUAMUA. Wengi wetu tumebaki kuwa wachambuzi na wakosoaji na sio watu wenye kuamua, wengi huwa wanasisimka wakisoma Papaa On Tuesday lakini kasheshe iko kwenye Kutendea kazi. Yesu akasema anaheri yule anayesikia na Kutenda. Upo hivyo ulivyo kwa sababu ya aina ya maisha uliyoyaamua na siku ukiamua kufanya utashangaa kwanini ulichelewa kufanya maamuzi sababu kubwa Unaweza kufanya lakini yamkini hujaamua kufanya ingawa unajua ndani ya Moyo wako UKIAMUA kikwelii kufanya unaweza kufanya na kubadilika. Yamkini umekuwa ukitamani kubadilika tabia fulani kwenye maisha yako lakini umekuwa ukiindekeza ili uendelee kuwa nayo huku ukitambua fika tabia hiyo ndiyo imekuwa kikuharibia kila siku kwenye maisha lakini hujaamua tu kubadilika ukiamua inawezekana.

Hatma ya Maisha yako yanategemeana sana na MAAMUZI unayoyafanya kwenye maisha, ukiamua kubadilika utaona mabadiliko ukipotezea mabadiliko utajipoteza mwenyewe, ukitazama duara lako kubwa la uwezo ulio nao halifanani kabisa na kile ambacho unakifanya na unajua UKIAMUA inawezekana tatizo halipo kwenye kile unachokifanya tatizo lipo kwenye Maamuzi yako ya kuamua kufanya kwa utashi wa ndani kabisa.

Kuna bloggers wengi sana bado hawajaamua kufanya, kuna wafanyabiashara wakubwa sana wenye mafanikio wanaogopa kufanya, kuna presenters wazuri sana lakini hawajaamua kufanya kile walichoumbiwa kufanya sababu ya wasiwasi wa ndani,sababu ya maneno ya watu, yamkini sababu ya kiimani, ama una mashaka watu watakuonaje watakuchukuliaje utaendelea kubaki kama ulivyo sababu tu hujaamua kuwa vile unavyotaka kuwa kwa kuangalia tu mazingira ya nje, adui nambari one wa mafanikio yako ni nafsi yako mwenyewe. Ukimtafuta mtu yeyote aliyefanikiwa kwenye maisha atakuambia "aliamua".

Tofauti ya Wewe na wale uonaoona wamefanikiwa ipo kwenye Kuamua, ukiamua kulala njaa siku 7 ili kutimiza ndoto yako itakuwa, ukiamua leo kuacha tabia za kijinga kwenye maisha yako utapiga hatua, ukiamua kutulia utaoa ama utaolewa, ukiamua kukuwa kiufahamu ndipo utakapofanikiwa kumbuka kuamua ndiko kutakutofautisha na wasio amua.

Amua Sasa.

Ze Blogger
0713 494110

Breakthrough Conference Kuanza Rasmi Leo...Kawe Makuti



Lile Kongamano Kubwa lenye jina la "Kongamano La Mpenyo" linatarajiwa kuanza rasmi leo katika Kanisa la Kawe Makuti chini Ya Apostle Onesmo Ndegi...

Akiongea na Chomoza Pamoja na blog Hii, Apostle Ndegi amesema Kongamano hilo litahudumiwa na watumishi Wa Mungu Kutoka Ndani na Nje Ya Tanzania. Kongamano hilo linatarjiwa kuanza rasmi tarehe 25 Mpaka Jumapili nani ya Kanisa la Hilo.

Campus Night 2013 Ndani Ya Mikoa Minne



Ile Event Kubwa ya Kujumisha Wanafunzi wa Tanzania almaarufu kama Campus Night mwaka 2013 itafanyika kwenye Mikoa Minne chini ya Coordination ya Kanisa la VCCT na Makanisa Shirikishi katika Mikoa husika.

Mchungaji Dr. Huruma Nkone aliongea na Blog Hii pamoja na Kipindi chako Nambari One Chomoza Ya Clouds Tv kuhusiana na Maandali ya Campus Night 2013 itakayofanyika Dar, Kilimanjaro, Arusha na Mbeya

KULA MATUNDA SIO LAZIMA USHAURIWE NA DAKTARI!!!

Habari zenu!
Watu wengi sana hawana tabia ya kula matunda ipasavyo! wengine huona kama ni chombezo mezani,wengine ni ziada na wengine ni mpaka daktari aseme!

KULA MATUNDA KUNA FAIDA NYINGI SANA,HIZI NI BAADHI YA HIZO CHACHE;
a.Matunda mengi ni dawa, maana yana virutubisho asilia
b. Matunda yana Vitamini nyingi sana na madini, na matunda mengi yana Vitamin C
c. Matunda hususani yale yenye nyuzi nyuzi (rouphages) husaidia mmeng'enyo na uyeyushaji wa chakula mwilini.
d. Matunda huongeza damu mwilini na kusafisha pia mfano ndizi huongeza vitamini K ,ambayo inasaidia sana kwa WALE WENYE MATATIZO YA KUTOKA DAMU PUANI.
e. Matunda yenyewe ni mlo wa kutosha kabisa na kwa mujibu wa wataalamu mtu anaweza kuishi kwa matunda tu na bado akawa na afya njema kuliko mtu anayekula vyakula vingine!
Punguza kula mafuta mengi na sukari kwa mbadala wa matunda!

Kuna matunda mengine watu wanaona ni kama viungo tu lakini nataka nikwambie matunda na mbogamboga kama vile NYANYA,KAROTI,LIMAO ni matunda safi sana na viungo kama TANGAWIZI,VITUNGUU SAUMU NA VITUNGUU MAJI unaweza kula kwa kutafuna maana husafisha mwili na damu sana!

UNAPOKULA MATUNDA UNAKULA VITU ASILI,DAWA ASILI,MADINI NA VITAMINI ASILI,MAJI NA SUKARI YA ASILI....Hivyo kama huna utaratibu wa kula matunda basi anza sasa!!!

Huna haja ya kunywa chai asubuhi kila siku,wakati mwingine anza na matunda tu na hata unapolala usijichindilie na chakula kingi kizito,unaupa mwili kazi ngumu na kisha unalala, hivyo utashangaa unamka mchovu na kitambi kinatoka bila mpangilio!!

ANZA SASA KULA MATUNDA KWA AFYA YAKO!!!!

Niulize nikushauri
0713883797

Papaa On Tuesday...Usione Ukadhani

Ikiwa ni siku ya pili tangu nilipoutangazia umma rasmi kuwa sasa nimeamua kuvunja Ukimya na Kumtangaza Mchumba wangu ninayetarajia kufunga nae ndoa nimekwisha anza ku-experience maisha mengine tofauti ya yale ya kabla ya Jumapili. Ni Kwa neema ya Mungu leo nimefika hapa.

Leo nimejisikia vema tukatazama kile ambacho Diwani ya Mloka tulikisomaga kinaitwa Usione Ukadhani. Watu wengi sana wakiona jambo ama wakimuona mtu wanadhani kwenye Kiingereza wao wanasema "dont judge a book by its cover" ingawa kuna mdhanio mwengine ni wakweli mwingine vema ukasikia ama ukapitia ilikuweza kuwa na majibu sahihi. Mara nyingi sana jamii imekuwa na wepesi wa kufikia hitimisho ya kile ambacho wao wanakidhani ni sahihi kumbe sio. Mara kadhaa kwenye maisha yangu kuna watu waliwahi  nidharau kuwa siwezi kufanya kitu kutokana na muonekano wangu kumbe sio kabisa usione ukadhani.

Kutokana na mfumo wa maisha ya Watanzania na Waafrika kwa ujumla mambo mengi sana tunajifunza ukubwani tukiwa wadogo ni familia chache sana zinatoa mwanya wa mtoto kuji express feelings zake na ndoto zake na tangu utotoni tulifundishwa kuwa mambo mengi ni mabaya pasipo kuambia ubaya wake na tulifundishwa kukosea jambo lolote ni vibaya zaidi ndio maana kuna watu wakifeli mitihani wanaamua kujiua sababu kwenye maisha yake ameambiwa kufeli ama kushindwa jambo ni kitu kibaya. Ukiwa mtoto ukiongea ongea sebuleni na kupiga piga meza ukawa unaimba nyimbo za kitoto utaambiwa kelelee, nyamazaaa basi unakuta unapoteza confidence na saikolojia yako inaambiwa hutakiwi kufanya jambo hili mbele ya wazazi. Ukiwa mtoto ukasema "mama mie mchumba wangu mtoto wa Mzee Charle" usiku huo huo utachapwa fimbo kuwa umeanza kuharibika matokeo yake saikolojia ya ufahamu inaambiwa kuwa kupenda mtu ni vibaya na kwa kuwa umri wa kutoka nyumbani kwa wazazi kwetu sisi ni pale unapoweza kujitegemea unajikuta mambo mengi sana unajifunza sio mbele ya wazazi ama watu waliokulea ndio maana kuna mambo mengi sana wazazi wetu hawajui kama tunajua kwa ufahamu wao wazazi wanadhani watoto wao hawajui kumbe watoto ndio wamegeuka waalimu.
Nakumbuka zamani enzi zetu wakati tunakuwa kabla video hatujaja kuangalia sebuleni baba na mama wanakuwa wanaingalia kwanza kama kuna sehemu sio nzuri basi alikuwa anakaa na remote control ikifika lile eneo anazima anapeleka mbele kidogo kisha tunaendelea. Kwa sisi watoto watundu tangu zamani tulikuwa tunamaswali hivi pale anapopeleka mbele kuna nini?basi wengine walienda extra mile tukavizia wakati baba na mama hawapo tukawasha tukaangalia mwanzo mwisho ila baba na mama wakirudi wanajua hatujui kuna nini. Tofauti na Kizazi cha sasa ambacho wao hutazama kanza kupitia mitandao kisha kama watatazama na familia watoto ndo wanawaambia wazazi sasa "baba hapo forward kidogo sio pazuri" sasa najiuliza mtoto ndo anamwambia baba aforward kwa manufaa ya nani baba ama yeye mtoto??Usione Ukadhani watu kizazi hiki hawajuio kwa taarifa yako watu huwa wanaambiana.

Usione leo mtu hana chochote ukadhani ataendelea kuwa kama alivyo, watu huwa wanabadilika kwenye maisha priorities nyingi sana za wanaume huwa zinabadilika pia kutokana na umri aliokuwa nao, majukumu aliyokuwa nayo na Marital Status yake pia. Kabla ya kuwa na mpango wa kuoa kwenye maisha atakuwa anawaza kula bata atakuwa anawaza kukutana na Jack, Rose, Mwamntumu, kwenda movie, kwenda mlimani City, akishaanza kuwa na mahusiano majukumu yanabadilika harusi ikikaribia kama mimi utakuwa unawaza Shella la Bibi harusi, Kiatu Cha Bibi harusi, Suti ya Bwa. Harusi Ukumbi, Mc pole pole akili inaanza kuwaza majukumu. Ukishapata familia sasa na mtoto utaanza kuwaza Pumpus za mtoto, mara bima ya afya ya Mtoto, ada ya shule, Mke nae avae,afanya kazi, mtaanza kufikiri Miradi ya kifamilia,mtawaza kujenga usione leo mtu yupo yupo ukadhani ataendelea kubaki alivyo. Akili hukuwa kwa kuzoeshwa ingawa inawezekana sio wote lakini Kibongo bongo tunakuwa kwa kukosea sana ukubwani hata namna ya kuishi na mume na mke tangu utotoni akili imejizoeza kujificha ficha hata kama ni halali.
Jambo usililolijua ni kama usiku wa giza unaweza ukaona leo mtu amekuwa na mafanikio ukadhani yalikuja kirahisi rahisi kwenye maisha. Kuna watu ukisikiliza hatua zao za maisha unajiona kabisa wewe unadeka unataka mafanikio wakati hata kushinda njaa mchana tu huwezi kuna watu mpaka leo wametoboa kwenye maisha wanahistoria ambazo ukizisikiliza kuna nyakati waliomba usiku usiingie sababu hawana sehemu za kulala walitamani kama kuna mahali wanaweza uza njaa basi wangeuza kwa bei yoyote ili wasiwenazo milele kuna watu walishinda njaa si kwa sababu walitamani kufunga la hasha hakuna chakula usione ukadhani kila kitu kinakuja bure. Tamaa mbaya ya mafanikio ya haraka haraka ndio inayopeleka mtoto wa masikini akiwa form four anawaza kuwa na blackberry yuko tayari kufanyiwa chochote apate blackberry used. Usione Mtu ukadhani kila mtu anaendesha gari leo amenunua kihalali wengine wamenunua ka kudhalilisha maisha yao ili waonekane. Usione leo watu wameajiriwa kwenye makampuni makubwa ukajua wameshinda interview za kazi walishinda interview za ngono ndio wakapataKama kuna kitu Watanzania kinatutesa ni Ulimbukeni. Usine Ukadhani.

Usione wanandoa wanaongoza kuingia kwenye ukumbi wa harusi wako pamoja wamevaa vizuri ukadhani hilo tabasamu ndilo walilokuwa nalo wakiwa nyumbani. Ungepata fursa ya kujua undani wao ndipo ambavyo ungefuta dhana yako ya kuolewa ili na wewe tu uwe na mume sababu uliosoma nao wameolewa, uliocheza nao wanawatoto, ungefuta dhana ya kuoa sababu mke wako ana umbile la namba 8, mke wako aonekane ana makalio, ama mweupe au mweusi kwani unaolea jamii ama unaoa kwa utashi wako mwenyewe wengi waliokimbilia ndoa kwa sababu za kijamii wamejikuta wamekwama na kama ingekuwa dini yetu ya Kikristo inaruhusu talaka wengi wangechukua talaka pamoja na kuto kuruhusu watu wanatoka wamechokaaaa. Rafiki yangu mmoja alinichekesha akasema kuna wengine wamefika stage wanaombea basi hata wafe ili wapumue maana hawa wanandoa wakiwa mbele za watu full matabasamu full kushikana mikono lakini wakiingia tu kwenye gari kurudi nyumbani maisha ya Chui na Paka yanarudi kuna wanawake leo wanatamani  wangeolewa na wanaume masikini wachume pamoja kuliko waliowachagua wanaume wenye uwezo wamejikuta wanaambulia majuto kuliko furaha usine ukadhani.

Usione watu wanavaa tai na sketi nzuri wanafanyakazi kwenye maofisi ukadhani wanafuraha na kazi zao, shida ndio zinasababisha waendelee kwenda ofisini wengine hawana hata mishahara wana mikopo kupita Serikali ya Tanzania, kuna watu wanaenda maofisini hawana hata mikataba ya ajira zao yaani hawana hatma ya kesho yao itakuaje kiajira, we usione watu wanavyojiupara na kula chips kuku ukadhani mambo yao safi, simu zao nzuri hazina vocha, mabegi yamejaa vipodozi vinavyokaribia kwisha, nguo wamekopa pale kwa mdada anayepitisha ofisini kwao kwa muonekano wa njee utadhani wanaraha kuliko wewe, ukitaka kujua uhondo wa ngoma uingie ucheze usione ukadhani ndugu yangu.

Maisha kila siku ni kujipanga unaweza ukadharaulika leo ukajipanga ukashangaa wale aliokuwa wanakucheka ndio baadae wanakupongeza watu huwa wanakawaida ya kudharau watu usitegemee kupendwa kabla ya kudharauliwa kwanza. Mtu mmoja anayekutia moyo wakati wa shida ni muhimu zaidi kuliko jeshi linalokushangilia baada ya ushindi. Usione ukadhani wewe jipange ili kuweza kusonga mbele. 

Think Differently and Make A difference.

Usione Ukadhani.

Samuel Sasali
0713 494110
Facebook: Samuel Sasali
Skype: SasaliJr

Samuel N. Sasali HAS THOUGHT DIFFERENTLY and HE HAS SHOWN A DIFFERENCE!!!!

Hello friends,fans and readers!!
I do believe that we are all doing well and we are fine!
Well then i am humbly inviting you very specially to CHAVALA MEDIA Blog
When the Sasali was vowing to MILEMBE

Zoomed edition
.....HE WAS CARRIED JUST LIKE A PIECE OF SOMETHING!!!!

Today i have a very testimonial post/news about a SAMUEL SASALI a.k.a Papaa /The Blogger/ The MC na may be you know him as TV Presenter,Motivational Speaker and May be Event Organizer but all in all he is the same guy, He is the thinker, ambitious and very unique friend of friends, allow me to declare my interest,Yes He is my Twin!


In most of his writings and presentations he has this say "THINK DIFFERENTLY TO MAKE A DIFFERENCE"...I real admire this say and i understand it more than what it says....Yes! among many things he has said and done this one was proved his uniquness!!
 ....Here Milembe was also vowing to Sasali....
 Samuel Sasali used that opportunity to give special offering to God, and he did that for two reasons and that are getting a beautiful girl and having another job as TV presenter...this also imply that the guy thought differently and surely the mass was very differnt!!!
Senior Pastor of VCCT, Rev.Dk Huruma Nkone with couples

Being a first born of a Long time pastor Rev.Nathanael Sasali and a brother of Pastor Mathew Sasali who got married 8 years ago with three children now, being MC of very many events and being involved in a number of relationship THEN last sunday we have all witnessed a DIFFERENT THOUGHT that is not relating to any of anybody and it has never seen anywhere else......YES THE BROTHER HAS FINALLY ENGAGED A BEAUTIFUL LADY,Doctor by proffessional and polite by nature; MILEMBE JOHN MADAHA.

Sometime back Papaa ever told me that....WHEN A POPULAR DATES....It is a challange! and from experience he said he will write a book soon after getting marriage and i have real realized that it is not as simple as someone can imagine....i am in the same trailer and i always pray that i don't mess on this matter.
....I WILL BE WAITING FOR THE BOOK FROM SASALI NOW!!!
 Special Lunch at Kawe beach together with friends!!

The way Papaa has configured and potrayed himself in his community, the way he has contributed his efforts and finances to others' visions and the level of his committment to his friends  and how he has touched people's hearts....it is what many friends and other people has experienced on sunday!!

Very many people came from different angles of the city and for sure the church was packed, great celebration, massive cameras of private and public mass medias and prolonged busy scheduled continuous party
Samuel intruducing Milembe at home party

The Event took place At VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE (VCCT) soon after the Sunday Mass.
 and THERE after  friends came together at Kawe beach for Lunch and because Samuel is the man of the people,then he just ate his lunch and went for live interview at DPC where there was an event "YOUTH TALENTS EXPLOSION CONCERT" and then he went to moderate another FUNDRISING Oriented Concert by Hananasifu Orphanage Centre Children who were also launching their DVD,at Victorious Church around Mabibo External then afterward there was a special dinner party at his father's house at Tegeta.

Hope now you can understand when i say this guy is unique is always thinking differently....can you imagine his younger brother married 8yrs back but still he had cataut to assist him dearly, The day of his engagement he has very many events to attend and made it!

I ARGUE ALL READERS AND FRIENDS TO SUPPORT THIS BROTHER VERY CLOSELY AND LOVELY AS HOW HE HAS PROVEN WORTHY INTO YOUR ISSUES...THE JOURNEY HAS JUST BEGAN AND THERE ARE LOT OF ISSUES TO DO FOR HIM....HE IS FAMOUS AND HE DESERVE THE BEST FOR WHAT HE HAS CONTRIBUTED INTO THE SOCIETY SO FAR.

Finally i would wish to encourage you all to support the work, the ministry and talents of my twin in any way you can but willingly...you can choose to be his friend in SOCIAL MEDIA, you can choose to Watch his Tv program "CHOMOZA" via Clouds TV at every sunday on 1800hrs, all read his educative posts in social media profiles or in blogs such as 
http://samsasali.blogspot.com http://chavalamedia.blogspot.com
And may be attending "FRIENDS ON FRIDAY"(FoF).

I HAVE WRITTEN ALL THIS TO YOU VERY CLEARLY AND CONFIDENTLY AS I AM VERY CLOSE TO HIM AND I EVEN MODERATED THE DINNER PARTY IN TAGETA, THE WEDDING IS ANTICIPATED TO BE ON 26TH OCTOBER 2013....All other detailed informations to be communicated to you via different medias including this one!!!


>>>BUT YOU CAN CHOOSE TO PLEDGE/SEND YOUR CONTRIBUTION NOW TO 0713494110
IN ORDER TO RESERVE YOUR SEAT or TO SHOW YOUR LOVE!!!
Samuel & Milembe
......THIS IS HOW THE DAY WAS CONCLUDED AT TEGETA!!!!

Thank you all and i wish him all the best in every single step untill marriage and ever
 BY
+255 713 883 797
King Chavala-MC

#....NI MARUFUKU!!!#(03).....Kuvaa nguo zenye maandishi ya AJABU AJABU!!!

#....NI MARUFUKU!!!#
Ni marufuku kwa mtu yeyote mwenye akili timamu,mstaarabu na mwenye future na anayejiheshimu kuvaa fulana/nguo au niseme T-shirts ambazo zina maneno asiyofahamu maana yake au hata kama ana fahamu maneno yasiyo faa....yaani wewe unanua tu bora ni Tshrt,zingine zina matusi aitha kujitusi mvaaji,au wengine wanaosoma au hata kuaibisha jamii yako.....Nimekutana na mtu amevaa tshrt imeandikwa..."I am proud of My Virgin Grandma" na mtu yuko happy tu dah! inawezekanaje Bibi yako mama yake na mama yako awe bikra hata sasa kama sio matusi hayo? 

MAMA YAKO ALIZALIWAJE NA BADO BIBI YAKO AKABAKI BIKRA KAMA SIO USHIRIKINA HUO????

 Unajua maana ya haya maandishi kwa tshrt hii?
Au mtu unavaa tu?

Kwanini basi usiulize kwanza kabla au mara tu unaponunua?\

Na watu wengine wala hawatakwambia utashangaa wanakucheka tu,kila ukivaa na wewe unaweza kudhani wanakufurahia kumbe kejeli!

JE UNAJUA KAMA NGUO KAMA HIZI ZIMEBEBA MAANA NA KUPIGIA DEBE MASHOGA NA WASAGAJI?

Nimeona nyingi sana lakini masikini wengine huwa hawajui maana yake hivyo wanavaa tu, na sehemu nyingine wazazi wengine huwanunulia watoto wao dah! haiwezekani mtu mzima akavaa Tshrt inayomtambulisha kama "kahaba mpole" mbona zipo nguo kibao zenye maneno mazuri tena ya lugha yetu ya kiswahili kwanini kuvaa kitu unachokielewa....najua unanielewa na yamkini umewahikuona na wewe mtu akiwa amevaa kituko....kama unakumbuka basi tupia mfano wa uliyowahi kuiona na useme ...HATA HII MARUFUKU KABISA!!!
ANGALIZO:Kwa wale wanaopenda kuvaa hivyo hivyo makusudi kabisa basi yamkini wana maana zao ambazo wangependa watu wajue bila wao kuongea kwa mdomo....hao ni issue nyingine,lakini wewe sio mmoja wa WASIOJITAMBUA NA KUJIKUBALI SAWASAWA NA UUMBAJI WAO,basi nimesema marufuku kabisa!!!

>>>Hii ni kwa ajili ya watu wenye akili timamu tu wanaojitambua na kujiheshimu tu.....vigezo na masharti kuzingatiwa!!

@Kwa hisani kubwa ya Chavala Ideas Platform <chavalamedia.blogspot.com>

NAMNA MBALIMBALI YA KUPIKA WALI!!!

Habari zenu!
Najua watu wengi sana wanapenda wali kuliko chakula kingine chochote na hata wale wasioa na kuolewa basi pishi lao kubwa ni Tambi na Ubwabwa na wale wa mikoani(nje ya Dar hupendelea kupika ugali)
Yamkini wewe unajua kupika wali na Rice cooker basi!
Lakini mchele una aina nyingi sana za kuupika kama vile wali wa maua,wali uliokaangwa na mbogamboga na kutaja aina chache;
Naam hivi ndivyo asemavyo
Chef Issa Kapande
KWA WALE NDUGU ZANGU MLIOKO UGHAIBUNI MCHELE ASILIMIA 90% HAUNA LADHA NA HARUFU NZURI KAMA TULIOUZOEA NYUMBANI CHUKUA UJANJA HUU ILI UFANYE WALI WAKO UWE WA KUNUKIA NA LADHA SAFI KABISA



Karoti iliyokwaruzwa vizuri, nyanya na vitunguu vilivyokatwa katika umbo dogo dogo rahisi kwa kuiva


Mchanganyiko wa karoti, kitunguu na nyanya katika kikaango chenye mafuta na moto mkali pika kwa dakika 5 tu usiache ziive sana kisha changanya wali wako ambao umeshaiva.



Huu ni wali ulioiva na ukachanyanywa na mchanyiko wako wa caroti, utapata harufu nzuri na ladha nzuri sana kwa kupata harufu na ladha nzuri zaidi unaweza ongezea pilipili hoho au girigilani ( Corriender leaves).


Mahitaji
720gram caroti iliyokwaruzwa

480gram Basmati rice ( mchele wa pishori) iliyopikwa

2 vitunguu vikubwa vikate katika size ndogo

1 Nyanya moja kubwa ikate katika size ndogo

1 fungu la majani ya girigilani

2 kijiko kikubwa cha chakula karanga zilizokaangwa kwajili ya kupambia

3 kijiko kidogo cha chai cha mafuta ya kula

Chumvi weka kulingana na ladha na mahitaji yako

Jinsi ya kuandaa:

Pasha moto sufuria lako au kikaango weka mafuta kisha weka vitunguu kaanga kiasi tu visiungue au kua na rangi ya kahawia vilainike tu inatosha.

kisha weka nyanya zikaange mpaka zichanganyike kabisa zitengeneze rojo rojo
Kisha weka caroti zilizokwaruzwa katika mchanganyiko wako kaanga na zichanganyike vizuri

Kisha weka wali wako wa basmati ulioiva katika mchanganyiko wako wa karoti changanya vizuri kisha mimina majani ya girigilani na changanya pole pole mwisho kabisa weka karanga zako ambazo zimekaangwa vizuri kama unatumia.

Mapishi haya unaweza tumia mchele wa aina yeyote ile sio lazima mchele wa basmati 
Source; http://activechef.blogspot.com

Papaa On Tuesday…..Unao Uwezo Wa Kuchagua Cha Kufanya Lakini Huna Uchaguzi na Matokeo Ya Kile Ulichokichagua Kukifanya.

Tukiwa bado katika Maombolezo ya Kupoteza ndugu zetu katika Mkoa wa Arusha kwa sababu zinazosadikika ni za kisiasa nachukua fursa hii kuwapa pole ndugu zetu wote ambao wamefariki lakini pia na wote waliojeruhiwa hasa hasa Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha rafiki yangu na mtumishi katika Shamba la Bwana Bw. Amani Golugwa pole sana na “majanga” ya Kisiasa. Nimeamini kweli tunao uchaguzi wa nini cha kufanya lakini hatuna uchaguzi wa kuzia matokeo ya kile tulichokichagua kinapotokea. Ukichagua Siasa basi matokeo ya Siasa ujue huna maamuzi nayo.

Wengi tuko leo hivi tulivyo kama matokeo ya kile ambacho tulikichagua katika maisha, na wakati huo tuliona sie ndio wenye mana kuliko wengine wote wakati wa kuchagua lakini hatukujua kuwa kile tulichokichagua hatuna uwezo wa kuhimili matokeo yake ya kwenye maisha. Wengi wetu wakati tunahimizwa kwenda shule tuliendekeza ubishoo na usharubalo, tulikuwa na uwezo wa kuamua either kusoma ama kuendekeza ujinga wa makuzi wakati huo kwa kufuata mkumbo wa mambo yaliyokuwa yakiendelea. Pengine kila ukikaa unajicheka kwa kile ambacho ulikichagua wakati huo na ukasahau methali ya Majuto ni Mjukuu waliponena wahenga, tulijiona sisi ndio tunaojua kuliko wale waliokuwa wakituasa na kutuhusia. Leo tumekuwa na akili tunatamani zile zama tulizokuwa tunakula chips na kuvaa raba za gharama na kuendekeza ubishoo zirudi tena ili tufanye kweli, lakini wapi kila jambo na majira yake. Wengine tunasoma Elimu za Watu wazima sit u tulikuwa na tatizo la ada kipindi hicho la hasha ila tulipokuwa nacho tulitumia na kilipoisha tukajijutia kwenye maisha.

Kuna mdada mmoja rafiki yangu anaishi kwenye mateso makubwa ya ndoa yake na amebaki kujutia maamuzo aliyoyachagua kuyafanya kisa na mkasa anasema hakujua, kama angelijua angechagua kuendelea na maisha yake kwanza ndipo achague kuolewa akiwa na akili timamu. Majanga mengi sana ambayo tunapitia kwenye ndoa na mahusiano ni kutokana na maamuzi yetu ya kukurupuka, maamuzi yetu ya kujiaminisha kuwa tuko sahihi kuliko wengine matokeo yake tunabakia kufa na tai shingoni. Kwani uwongo??ukikaa mwenyewe hujiambia kuwa laiti kama ungelijua usongechagua kuolewa ama kuoa Fulani kisa na mkasa matokeo ya kile ulichokichagua kwenye maisha. Kuna wengine walitaka kuolewa so kilichotokea wakabeba mimba wakidhani maisha yale ya honey baby and sweetheart yataendelea, kongwa walilojitishwa na nira walizojifunga wamebaki kulilia moyoni, mkiwaona barabarani na kwenye facebook utadhani ni ndoa ya mfano kumbe si lolote si chochote kila mtu analala chumba chake nyumbani hakuna furaha ambayo inadhaniwa ipo wakiwa nje ya mlango wa nyumba yao wakikaa wenyewe wanatamani sana kurejesha maisha siku ambazo walikuwa wanacheka na kwenda kula bata na kuitana majina ya mahaba, leo yamebaki kuitana “wewe”, “Nanii”, “Stella”, “Sultani” dry dry dryyyyyyyyyy. Lady Jay d anasema anatamani kuwa kama zamani lakini ndo zama zimeisha tena maisha yamebaki kuishi kwenye matokeo yake.


Kuna Ofisi Fulani nilifanya kazi zamani kuna jamaa alicha kazi baada ya kupata kazi sehemu nyingine kwa ahadi ya project mpya alipohama kwetu akaenda kwingine ambako huko project ikakosa hela akabaki mtaani akajuta sana kwa uamuzi wake wa kuacha kazi alikuwa na muda wa kuchagua kuacha kazi ama kuanza upya sehemu nyingine matokeo ya maamuzi yetu mengi hayamo ndani ya matakwa yetu. Unaweza kuacha kazi sehemu moja ili ufanye kazi kwingine ukashangaa ulikokwenda ndo unapunguzwa wewe ama unahama nyumba moja kwenda nyingine kumbe unakokwenda ndo kuna zoezi la upanuzi wa barabara unabaki kusema ng’ombe wa masikini hazai. Wengine wamepata watoto mapema si kwa sababu walikuwa wanapenda kuzaa bali bali kilichotokea “ajali” ikasababisha waanze kuitwa “mama” ama “baba” wakati wa kudungunyuana walikuwa wanasikia raha ila ilipofika ujauzito wengine wakasema wakatoe ama wakatoa ujue ulikuwa na uchaguzi wakati wa kuamua lakini ukasahau unawajibika na matokeo ya kile ulichokiamua kwenye maisha yako.


Kuwajibika na matokeo ya yale tunayoyaamua ni wachache wetu wako tayari unapotaka kufanya maamuzi kwenye maisha jua kabisa wewe unawajibika na matokeo ya maamuzi unayochukua kwenye maisha. Kila ambacho unakichagua kukifanya jua kina matokeo na uwe tayari kupokea matokeo ya kile ulichokichagua kukifanya kwenye maisha.

0713 494110

HATIMAYE SAMUEL SASALI a.k.a PAPAA ATAKUWA AKITANGAZA UCHUMBA RASMI TAR 23/06/2013 PALE VCCT!!

Hello marafiki na wasomaji wote wa Blog hii!!
Leo ninawaletea habari njema  zilizoambatana na mwaliko  maalum kwa watu wote wenye mapenzi mema na Samuel Sasali, The Blogger, MC,Mzee wa Ideas mengi ambaye mara zote husema Mungu alimnyima urefu akamjalia Mdomo (kuongea sana) na kukosa aibu pia!!!
Baada ya sarakasi za kutosha za kutafuta mwenzi wa kumfaa hatimae pacha wangu amegota na kumpata mlimbwende wa pekee aliyewashinda wanawake zaidi ya Bilioni 4 duniani na kuwa wa pekee...Usukani mdogo unaoendesha Merikebu kubwa!!!
 Ndio ni binti huyu Dk Milembe John Madaha ambaye ameteka moyo wa kaka Mkubwa na kwa huyu Papaa amegeuka rapper,mwana mashairi na mtiifu sana!!
Kama una kumbukumbu nzuri, blog hii imewahi kum-ZOOM kijana huyu kama mmoja ya vijana wanaopaswa kuigwa na vijana wengine,fuata link umfahamu vema;

.http://chavalamedia.blogspot.com/2012/08/salaam-leo-katika-kipengele-hiki.html

Basi habari njema ndio hii, jumapili hii wewe na wenzako wote ambao ni marafiki wa kweli Samuel Sasali au ni msomaji  wake wa Papaa On Tuesday au ni Mwanachama wa Marafiki Huru au ni mpenzi wa Friends On Friday au umewahi kufundishwa na yeye popote pale,shuleni, chuoni au kanisani au hata kama amewahi kusherehesha shughuli yako yeyote ile..basi sasa ni saa ya kumuunga mkono kwa kumaanisha!!

Ni jumapili hii ya tar 23/06/2013 kuanzia saa nne asubuhi pale Mbezi Beach A katika kanisa la VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE (VCCT),Unaweza ukapanda gari mpaka mwenge na kupanda usafiri wa kanisa unaondoka hapo tatu na nusu ama ukachukua bajaji mpaka huko kanisa la hema,au ukapanda gari mpaka kawe mwisho na kupanda bajaji pia mpaka kanisani au ukashuka Mbezi Tanki bovu na kuchukua bajaji au bodaboda mpaka kanisani...lakini kama unakuja na private car njoo na barabara ya Mwai Kibaki(zamani old bagamoyo road) kisha baada tu ya daraja utaona kibao kushoto kwako kama ukitokea mwenge then fuata njia hiyo kwa hakika huwezi kupotea!!

Ni marufuku kuja mikono mitupu na ni marufuku kuja peke yako,namaanisha jaribu kubeba zawadi ya pongezi na usiache kuwajulisha wengine wanaomfahamu Papaa!!

Haitakuwa siku ya kawaida kwa hakika maana Papaa ni baadhi ya vijana nguli ambae tayari alikuwa kwenye kundi la ma-senior bachelors na sasa rasmi anaanza kuaga aga kundi hilo....na hata harusi yake itakuwa mwishoni wa October, kama hakutakuwa na badiliko lolote basi itakuwa 26TH OCTOBER.. hivyo mwenye macho na asome na kuelewa!!!

Mimi binafsi kwa niaba yangu mwenyewe na kwa niaba ya Blog hii na wafanyakazi wote wa Chavala Ideas Platform ninatamka baraka nyingi kwa rafiki yangu mkubwa na pacha wangu Samuel pamoja na Shemeji yangu,his wife to be ....Mungu awaonekanie katika kila hatua ya michakato hii mpaka hapo watakapooana!!!
Na kwa hakika tuko bega kwa bega,naam tuko tayari kutoa mchango wowote ule wa hali na mali utakaohitajika ili kufanikisha shughuli hii,KWA HAKIKA NINAMKUBALI SANA PAPAA KWA JINSI ALIVYO NA ALIVYO MCHAKARIKAJI,HE IS AMONG MY BEST FRIEND IN TOWN!!!
Kwa wale msiomfahamu zaidi basi msiache kutembelea Blog yake kila siku
"samsasali.blogspot.com"

NA MWALIKO HUU NIMEUTOA KWA HIARI YANGU KWA NIABA YAKE,HIVYO KAMA UKIKWAMA AU UKIWA NA SWALI LOLOTE NAMNA YA KUFIKA HAPO KANISANI BASI USISITE KUWASILIANA NASI,NASI TUTAKUSAIDIA KUFIKA!!

+255 713 883 797
King Chavala-MC

#.....NI MARUFUKU!!!#(02)....Kwa Mwanaume Kufungua au Kupekua Mkoba wa Kike!!!


HABARI ZENU!!!!
Ni marufuku kwa kijana yeyote yule wa kiume au mwanaume kufungua au kupekua pochi au mkoba wa kike kwasababu yeyote ile hata kama ni rasmi,kama sio chini ya usimamizi na ruhusa maalum sana ya mwenye mkoba au pochi hiyo!!



Ni tabia mbaya sana kupekua pekua either kutafuta pesa kwenye pochi ya dada yako au mama yako au kutafuta ushaidi wowote ule kwa pochi ya mpenzi au mkeo....Je unajua pochi au mkoba wa kike unabebaga vitu gani? Je unafikiri pochi ya kike ni kapu la sokoni au? Vipi kama vilivyomo humo vikikupandisha presha ama kukupofusha,nani atakusaidia? na utajiteteaje?...Vipi kama ukivunja vya kuvunjika au kumwaga vya kumwagika? Vipi kama ukikuta picha ya ndugu yako either mjomba au mzazi utafanyaje?
Kama vile ambavyo sio rahisi wewe kumruhusu binti kupekua wallet yako vivyohivyo na wewe heshimu yao...nimewahi kuona baadhi ya vijana na wanaume wakinyang'anya na kupekua kwa lazima mikoba ya wadada au pochi za wamama na kisha kuwatupia chini,nilikuwa safarini na niliumia sana....na siku moja nilikutana na rafiki yangu mmoja na nikataka kumpokea mkoba na akakataa kabisa na kunieleza mengi na hapo ndio nikakumbuka maonyo ya mama kuwa ni marufuku kubeba mkoba wa kike isipokuwa kwa kibali maalum tena mkoba wa mtu maalum kama vile mkeo au mpenzi rasmi!!
Yamkini unafanyaga haya lakini hujui kama ni tabia mbaya,na wakati mwingine huwa unadhani ndio kujali,basi nikwambie wazi kabisa....Ni marufuku,tena marufuku tena marufuku kabisaaaaa!!
ukome ukomae kabisa...na hii ni kwa faida yako kijana,carrying someone's handberg might be an attitude of a gentleman but "pekuling" and "tafutaing" is a habit of Wamataifa...sasa nimesema marufuku,kama unabisha unaweza kuendelea tu!
Hii ni marufuku maalumu kwa watu wenye akili timamu tu!!

@Kwa Hisani kuwa ya Chavala Ideas Platform <chavalamedia.blogspot.com> (c)2013

Chavala Ideas Platform presents "TANZANIA GOSPEL SINGERS' BREAKFAST"....3rd Episode!!

HII NI FURSA MAALUM KWA WAIMBAJI WOTE WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA, MNAKARIBISHWA KWA CHAI YA ASUBUHI JMOS YA TAR 15/06/2013 PALE VCC-VICTORIA KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI...NJOO UMSIKILIZE MWALIMU NA MWANAMUZIKI SAMUEL YOHA AKIONGEA KWA KINA KUHUSU MUZIKI...HAKUNA KIINGILIO!!
KWA MAELEZO ZAIDI 0713 883 797
AU TEMBELEA http://gospelstandardbase.blogspot.com

#.....NI MARUFUKU KABISAAAAAA!!#(01).....Kufanya Maamuzi kwasababu ya kumhurumia mwingine!!!!

HELLO GUYS!!
Ni marufuku kwa mtu yeyote yule mwenye akili timamu kufanya maamuzi yeyote yale muhimu yanayobeba mstakhabali wa maisha yake kwa kigezo cha "KUWAONEA HURUMA WENGINE KATIKA MAAMUZI YAO"


Kwa mfano;
Eti mtu anakubali kuingia katika mahusiano kwasababu tu mtu huyo amekufuatilia kwa muda mrefu,kwa hiyo unamuonea huruma mdada au mkaka wa watu.....hivi wewe una huruma kuliko hata neno huruma lenyewe,aliyekwambia huruma ni kiunganishi nani?
AU
Eti mtu amepata kazi nzuri ambayo mahali pengine ambapo atalipwa zaidi ya mara mbili ya alipo sasa na kazi ni uhakika,lakini mtu huyo anasita na kubaki hapo,kwa madai ya kuwa mwajiri wake wa sasa atajisikia vibaya,sasa wewe unaishi kumfanya ajisikie vizuri hali unateseka na maisha yako?
AU
Mtu anakuomba umsaidie kitu,na wewe unajua kwa hakika kitaharibu muda wako na labda na hadhi yako,lakini kwasababu unamuonea huruma huyo anayekuomba basi unakubali,angalia usije ukajitafutia laana,kuna mama mmoja aliwahi kumuokoa mwanae wa kiume ili asife kwa kutembea nae baada ya kijana huyo kunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume huku akimngojea mpenzi wake na bahati(sijui mbaya au nzuri) huyo mpenzi hakuja,na dawa hizo ukinywa usipotumika unaweza kuondoka(hivi ndivyo ilivyo),na mama huyo aliwasihi dada zake wamsaidie wakagoma ila yeye akaona ni bora amuokoe mwanae,sasa yaliyomkuta mama yule ni kupata mimba ya mwanae na ili kuficha aibu alitaka kutoa na katika kutoa sijui ilitokea defects gani mwilini basi akapalalaizi na kazi akaacha na maisha yote yakasimama na kubaki majonzi,sasa sijui huyu mama tunamsemeaje lakini hata sasa kijana alishakimbia kuficha aibu na mama ndio huyo anateseka kitandani!
SASA SIO KWA MIFANO HIYO TU BALI NA MINGINE MINGI,TAFADHALI USIFANYE MAAMUZI YA MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO KWA KUJIONEA AU KUWAONEA HURUMA WATU WENGINE...BE REAL AND BE YOURSELF!!!
Ni marufuku kujaribu kufanya ujinga huu......kama na wewe umenielewa sema kwa nguvu.......NI MARUFUKU KABISA!!!!

"23TH OF MAY" MARK THE BEGINNING OF A NEW YEAR TO KING CHAVALA!!!

Shalom!!!
NINAYO HESHIMA KUBWA SANA KUWASLIMIA WAZAZI WANGU WAPENDWA MR.ERASTO & MRS.OLIVER CHAVALA,NA ZAIDI KUWASHUKURU KWA MALEZI YOTE MPAKA HAPA NILIPO LEO.....KWA HAKIKA NINAWAPENDA SANA!!

Ninawasalimia ndugu jamaa na marafiki na washika dau wote wa Stand Up Comedy na King Chavala kote duniani!
Kila tarehe 23/05 ya kila mwaka,huwa ni siku ya muhimu sana maishani mwangu kwasababu ndio siku ambayo mshale wa mwaka hufika ZERO na kuanza upya tena,ni siku ambayo nilikuja ulimwenguni humu kuanza kazi iliyonileta,ndio siku inayoongeza umri wangu na kupunguza muda wangu uliobaki hapa duniani,ndio siku ya kumshukuru Mungu sana na wazazi kwa malezi bora na utunzaji wa zawadi hii muhimu!
TANGU SASA NA KUENDELEA TAREHE HII ITAKUWA SIKU YA U-SMART/USAFI DUNIANI,sasa kama zote huwa mnaita kutokana na majina ya waazinilishi basi hii itaitwa "CHAVALA DAY......Siku ya usafi duniani"

Labda natania kwasababu mimi ni comedian lakini namaanisha in term of future expectation!!
SIKU HII NI NZURI MNO,NAMI NIMEPANGA KUSHEREKEA NA MARAFIKI MBALIMBALI....Kwanza siku hiyo hiyo au siku nyingine kwa niaba ya hiyo(maana hiyo ni siku ya kazi); Nitakwenda kuwaslimia Watoto Wa Mungu(Yatima) na kutumia siku yangu nzima pamoja nao,lakini usiku wa Tar 23 hiyo nitakuwa CBE-TAFES FAMILY,PALE A.17,pamoja na wanafamilia tukisherekea pamoja na kujikumbushia enzi hizo za uanafunzi.

Na siku ya jmosi 25/05/2013 tutakuwa na safari ya kwenda Bagamoyo kwa ajili ya kujifunza na kutalii,basi kama wewe umezaliwa mwezi May au ungependa tu kwenda na sisi basi wasiliana nasi kwa haraka........safari ya kwenda na kurudi kwa 15,000/= tu....NA SAFARI HII TUTAAMBATANA NA WANAFUNZI WA CHUO CHA AFYA,HKMU-MIKOCHENI

Ahsante wote kwa kuendelea kuwa na imani na mimi,ahsanteni wote msiochoka kuniombea,kunichangia michango ya aina zote,ya hali na mali,AHSANTENI SANA MARAFIKI,KAKA NA DADA ZANGU,KILA MMOJA ALIYESHIRIKI KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE KUYAFANYA MAISHA YANGU YAFIKE HAPA NILIPO NA APOKEE SANA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI!!

MUNGU AMENIPA UPENDELEO WA UHAI NA UZIMA TELE,VIPAJI LUKUKI NA ZAWADI A KIROHO NYINGI,NAJUA ANAYO MAKUSUDI NA MIMI,OLE WANGU KAMA SITAFANYA KAMA VILE MUNGU ANITAKAVYO NIFANYE!

Maisha yangu ni kwasababu ya Mungu,ninaishi na Mungu na ni kwa ajili ya Mungu.....basi Mungu wangu na awabarikini nyote!!

HAPPY BIRTHDAY DEAR MIMI!!!
King Chavala-MC
+255 713 883 797

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA CHAKUMBWA NA DHAHAMA TENA!!!!

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA CHAFUNGWA KWA MUDA USIOJULIKANA!!
chuo cha uhasibu arusha kimefungwa leo saa 12 jioni kutokana na kutoelewana kwa wanafunzi wa chuo hicho na mkuu wa mkoa Arusha.
jambo hili limetokea baada ya wanafunzi wa chuoni hapa kutaka kuandamana kwenda kwa mkuu wa mkoa kudai madai ya usalama wao kua mdogo kutokana na mauaji yaliyofanywa kwa mwanafunzi mwenzao HENRY KOGA kuchomwa kisu cha shingo na watu wasiojulikana na kumpola LAPTOP na mali zake nyingine.
kitendo hicho kiliwakumbusha machungu wanafunzi wa uhasibu kutokana kupita kipindi kifupi kupita tangu aliyekuwa mwanafunzi wa chuo hicho OCTAVIAN BUKAJUMBE kuchomwa kisu na kuuawa mazingira ya chuo hicho hata miezi miwili haijapita.
Kabla fujo na mabomu ya machozi kuanza kurushwa kila mahali wanafunzi walikutana chuoni eneo linaloitwa FREEDOM SQUARE wakipanga namna ya kuandamana kwenda kwa mkuu wa mkoa. RPC alifika pamoja na UONGOZI wa CHUO wakijaribu kuwazuia wanafunzi wasiandamane.
wanafunzi walionyesha kutowasikiliza wakimtaka MKUU WA CHUO ambaye alitafutwa bila mafanikio. kelele za wanafunzi zilipungua pale Mbunge wa jimbo la Arusha Godbless LEMA kufika chuoni hapa mnamo mida ya saa 4 asubuhi na kuwatuliza kwa kumpigia simu mkuu wa mkoa wa arusha kufika chuoni na kusikiliza madai ya wanafunzi hao. hasira za wanafunzi zilipanda baada ya mkuu wa mkoa kufika na kusema "hawezi kuongea na watu wasio na nidhamu" pia hawezi kuongea bila kipaza sauti akisahau kuwa wanafunzi hao wanauchungu na hasira za mwenzao kuuawa kinyama.
Mabomu yalianza kupigwa baada ya mkuu wa mkoa huyo kuonyesha kutojali kile wanafunzi wanachotaka. ndipo walipoanza kuzomea na kurusha chupa kwa mkuu wa mkoa na askari kuanza kupiga mabomu ya machozi...
Baadhi ya maafa yaliyotokea ni baadhi ya wanafunzi kuzimia na wengine kujeruhiwa na kuibiwa mali zao wengine wamekamatwa..wanafunzi waliobaki wametakiwa kurudi nyumbani kwao mikoa mbalimbali ndani ya Tanzania kwa muda usiojulikana.
Matukio ya uporaji na kujeruhiwa limekuwa tatizo sugu kwa wanafunzi wa uhasibu zaidi kwa wanafunzi wa kiume wasiokuwa na MABWENI chuoni hapo hivyo kulazimika kupanga maeneo ya karibu na chuoni hapo. ambapo hupata matatizo hayo wanapokuwa wakirudi magetoni mwao na wakati mwengine wamekuwa wakivamiwa huko huko kutokana na kutokuwa na usalama wowote.
Kimekuwa ni kilio jwa wanafunzi hao waweze kujengewa BWENI la wavulana mahali hapo bila kupata majibu yeyote.
Historia ya Marehemu
Jina: HENRY KOGA
Mwenyeji: IRINGA
Alikuwa anasoma: SHAHA YA FEDHA NA BENKI (mwaka 2)
Aliuwa: KWA KUCHOMWA KISU NA VIBAKA
Muda: KATI YA SAA 4 NA SAA 5 USIKU

JIHADHARINI SANA NA HAWA WEZI WA MTANDAONI!!!!

Hello it is high time now!
Natumai wasomaji wangu wote mko poa!
Leo natamani niwaonyeni watumiaji wote wa mitandao ya kijamii hususani facebook,Google+ na emails, kuna watu mashuhuri duniani wanaitwa HACKERS, hawa wanaweza kukutumia email kana kwamba wao ndio operators wa hiyo site ambayo wewe una email yako,na wanaweza kudai kutaka kufanya mabadiliko na hivyo wakaomba majina,umri pamoja na password na hapo ukiwapa wanaingia kwa account yako na kuitumia vibaya labda kuomba msaada wa kifedha kwa watu kwenye account yako then wewe huwezi kufungua tena!

PILI kuna hawa wanaitwa CYBER THIEVES hawa wanatumia njia ya kuwatumia watu eti wameshinda bahati nasibu,basi watakuomba details zako na ukiingia tu mkenge basi umeliwa,pia katika kundi hili wapo wengine hujifanya wana deal za muhimu hivyo huomba urafiki na hata kukupigia simu na hapo watakuja na hadithi za eti kuna fedha benki na mrithi kafariki so wanataka uwe wewe,hapo usipokuwa makini watakuwa wanakuibia taratibu...mimi Chavala niwewahi kuibiwa karibuni $4000 mwaka 2006 ndani ya kipindi cha miezi kama sita hivi,maana niliaminmi kuna deal kweli,nikawa natuma pesa tena wanakupa document nyingine nikatuma tena na tena na tena na baadae wakapotea na hapo ndio nikawa niimeibiwa mazima...haikuwa kazi rahisi maana nilikaribia kuchanganyikiwa,but sasa ninawajua hivyo nakuonyeni usijaribu kujisumbua ...HAKUNAGA PESA YA RAHISI KIASI HICHO POPOTE!!



Na kipindi cha karibuni wapo kwenye mitandao ya kijamii hususani facebook,ni wanaume wanacreate accounts na kuomba urafiki na hata kama sio rafiki basi wanakutumia inbox na kuomba ukaribu na wewe kwa account nyinginezo wanazokupatia,na ukirogwa tu kuanza kuwasiliana watakuvuta mpaka watakuibia,maana wanajua watu wengi wanawaamini sana wasichana na kupenda ngono za reja reja!!

HAPA CHINI NAKUPA MIFANO HALISI YA MAIL HIZO,NA HIZI ZIMETUMWA KWANGU!!!

*****************************************************
Griscilla Andrew

Hello
My name is Miss Gabriella,i saw your profile today and after going through it, i fill more interest to contact you ,i will like you to please send me an email at my email address
via (gabriellaandrew20@yahoo.com) for me to send you my pics and to tell you more about me. wait for your replied thanks.
*************************************************
Vivian Jones Vivian

Hello Dear
It really is a pleasure to come along your profile, and I Miss Vivian by name, a nice looking young girl in search of friend.This is why I decided to contact you on this site, so we can be friends and also get to know each other. Age, race and religion is never a problem for me, and the only thing that matters is true love. Please contact me at my private email (joness.vivian @ yahoo.co.uk) for ease of communication, and so I will give you my pictures and more details about me, I still hope for your reply, have a nice day, write me on my email address.
Your new friend Vivian
****************************************************
Sliverline Williams

Hello Dear ..,
How are you?
My name is Sliverline. I am a female and I would like to add you as my friend and to establish a long lasting relationship with you.You are free to email me back via my email address.; sliver_lineon@ymail.com ;please If you are interested in knowing more about me OK? so I can send you my picture and tell you more about me. I'll be waiting to hear from you with love,

Yours lovely,
Sliverline.
kiss____¶¶¶¶¶__AM___¶¶¶¶¶ IN
_____¶¶■޶¶¶¶¶Å½■޶¶¶¶¶■޶¶-
____¶¶■Ž█████޶Ž████Ž- ¶¶
___¶¶■Ž███████Ž█████- Ž■ ¶¶
___¶¶■Ž████████████- Ž■ ¶¶
____¶¶■Ž███████████Ž- ¶¶
_____¶¶■Ž█████████Ž■ ¶¶
_______¶¶■Ž██████Ž■ ¶¶
_________¶¶■Ž███Ž■ ¶¶ LOVE
__________¶¶■Ž`█Ž■ ¶¶
___________¶¶¶¶¶¶¶¶
*****************************************************
Alice Koly

I saw your profile i pick interest on it and if U don't mind i will like you to write me on this mail ID( alice_koly@ yahoo. com ) am waiting to read from you,because i have something VERY VERY important and urgent to tell you In my reply i will send U more of my beautiful picture

Please try write me direct to my email address so that i can be able to responds back to you OR you can give me your own Email so that i will replied you direct to your Email ID you give me my e-mail ( alice_koly @ yahoo.com )
*********************************************************
Peaceful Peace

My dear,
Thanks for your reply, Please i have very important issue to discuss with you, But i want you to write me later through my private email( peacetagro@ hotmail.com ) It's important,so through email is the possible way for me to communicate with you.
***********************************************************
Nnice Chansa

Hello,its my pleasure to contact you,after going through your profile,i am looking for a honest person,and i think i have found you, you can get me back through my email (annicegabriel@live.com) as soon as possible ,so that i will tell you better about my self and also send to you picture,please do not reply me here in this site,just write to my email ok.

(annicegabriel@live.com)



JIHADHARINI SANA JAMANI MSIJE MKASEMA HAMKUONYWA!!!


KWA LEO NI HAYO TU!!


kING cHAVALA
+255 713 883 797