CHOOSE TO ADVERTISE WITH US.....+255 713 883 797
NI MARUFUKU....KUVAA NGUO KIPUMBAVU!!!!
#....NI MARUFUKU!#
*Kwa kijana yeyote wa kiume kuvaa suruali chini ya makalio eti kata kei ama mlegezo....maana hiyo ilianzishwa na wafungwa wa marekani na ilikuwa dalili ya kiburi na Afrika kusini walikuwa wanavaa hivyo wafanyakazi wa Boers ili kurahisisha zoezi la kupigwa mihuri hapa juu ya matako baada ya kazi,na kwa sasa wanaume wasio riziki wa mashariki ya kati na ulaya wanavaa ili kuwavutia wateja wao kabla hawajaolewa....sasa wewe unavaa sasa hivi unamaanisha nini? Tena wengine unakuta boxer chafu kama nini....ukimuona kijana wa namna hiyo hata awe nani ama maarufu kiasi gani,ujue HAJITAMBUI!
*Kwa kijana yeyote wa kike kuvaa nguo za kulalia,nguo za ndani ama nguo zinazomdharilisha yeye na wasichana wengine wote....yaani mtu anatembea mjini na skintight tu,mwingine anatembea ameyaacha maziwa nje,tena makusudi...acheni ujinga ninyi,kama nguo ni ya ndani vaa ndani,thamani yako haiongezeki kwa kujichoresha na kuacha maziwa nje,kila mmoja anajua kilichopo ndani so kifiche tu,by the way chenye thamani hufichwa.....hizo ni tabia za makahaba na night stripers sasa wewe unayevaa hivyo una malengo gani? Wengine maumbo mabaya na wengine miili imejaa makovu,jamani ficha tu.
Sasa haijalishi ni nani wala nani,nimesema marufuku! Kama una akili timamu utazingatia hili lakini kama wewe ni mpumbavu basi unaweza kuendelea na nakuhakikishia usipobadilika mwisho wako utakuwa wa majuto...na kama utakuwa na watoto basi ndio utakuwa umeshawaharibu hata kabla hawajazaliwa!
SALAM HIZI NAZILETA BAADA YA MFUNGO KUISHA MAANA NAJUA KUNA WENGINE NDIO KAMA VILE WALIKUWA KIFUNGONI KUFANYA MEMA SASA WAMEACHILIWA KURUDI KULEKULE!
Na hata kanisani tusikuone na huo ujinga wako unless kama wewe ni agent na umetumwa kuharibu kanisa,potelea mbali ukinikasirikia lakini najua jambo moja tu.....MAMBO YOTE YATAPITA LAKINI NENO LA MUNGU HALITAPITA KAMWE!!
Na King Chavala MC
+255 713 883 797
Ujumbe huu unakujia kwa Udhamini mkubwa wa;
http://chavalamedia.blogspot.com
(c)2013
*Kwa kijana yeyote wa kiume kuvaa suruali chini ya makalio eti kata kei ama mlegezo....maana hiyo ilianzishwa na wafungwa wa marekani na ilikuwa dalili ya kiburi na Afrika kusini walikuwa wanavaa hivyo wafanyakazi wa Boers ili kurahisisha zoezi la kupigwa mihuri hapa juu ya matako baada ya kazi,na kwa sasa wanaume wasio riziki wa mashariki ya kati na ulaya wanavaa ili kuwavutia wateja wao kabla hawajaolewa....sasa wewe unavaa sasa hivi unamaanisha nini? Tena wengine unakuta boxer chafu kama nini....ukimuona kijana wa namna hiyo hata awe nani ama maarufu kiasi gani,ujue HAJITAMBUI!

*Kwa kijana yeyote wa kike kuvaa nguo za kulalia,nguo za ndani ama nguo zinazomdharilisha yeye na wasichana wengine wote....yaani mtu anatembea mjini na skintight tu,mwingine anatembea ameyaacha maziwa nje,tena makusudi...acheni ujinga ninyi,kama nguo ni ya ndani vaa ndani,thamani yako haiongezeki kwa kujichoresha na kuacha maziwa nje,kila mmoja anajua kilichopo ndani so kifiche tu,by the way chenye thamani hufichwa.....hizo ni tabia za makahaba na night stripers sasa wewe unayevaa hivyo una malengo gani? Wengine maumbo mabaya na wengine miili imejaa makovu,jamani ficha tu.
Sasa haijalishi ni nani wala nani,nimesema marufuku! Kama una akili timamu utazingatia hili lakini kama wewe ni mpumbavu basi unaweza kuendelea na nakuhakikishia usipobadilika mwisho wako utakuwa wa majuto...na kama utakuwa na watoto basi ndio utakuwa umeshawaharibu hata kabla hawajazaliwa!
SALAM HIZI NAZILETA BAADA YA MFUNGO KUISHA MAANA NAJUA KUNA WENGINE NDIO KAMA VILE WALIKUWA KIFUNGONI KUFANYA MEMA SASA WAMEACHILIWA KURUDI KULEKULE!
Na hata kanisani tusikuone na huo ujinga wako unless kama wewe ni agent na umetumwa kuharibu kanisa,potelea mbali ukinikasirikia lakini najua jambo moja tu.....MAMBO YOTE YATAPITA LAKINI NENO LA MUNGU HALITAPITA KAMWE!!
Na King Chavala MC
+255 713 883 797
Ujumbe huu unakujia kwa Udhamini mkubwa wa;
http://chavalamedia.blogspot.com
(c)2013
MSAADA WA DHARULA WA CHAKULA UNAHITAJIKA KWA WOTOTO YATIMA WA HOCET!!!!

SHALOM!
HABARI ZENU WAPENDWA!!
NINAAMINI MNA MOYO WA UPENDO, TENA WA KUWAJALI WENGINE KULIKO NINYI, NA HATA ZAIDI BIBLIA INASEMA UPENDO WA KWELI NI ULE WA KUWAPENDA WENGINE ZAIDI.
*****HANANASIFU ORPHANAGE CENTRE (HOCET)....HAWANA CHAKULA KABISAAAAA NA WEWE NA MIMI PEKEE NDIO TUNAWEZA KUWALISHA KWA SIKU 120, KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA****
LEO NINALO OMBI MAALUM KWENU, NI MUHIMU SANA SANA....KUNA KITUO KIMOJA CHA KULELEA WATOTO YATIMA (WATOTO WA MUNGU), KITUO KINACHOENDESHWA NA WATU TU WALIOJITOLEA, NA HAPO AWALI KILIKUWAQ KINAFADHILIWA NA WAZUNGU FULANI, LAKINI BAADA YA KUONA WATOTO HAO WAMEKAZANA NA MUNGU NA HAO WAZUNGU (WAFADHILI) WAKAWEKA MASHARTI, ETI KAMA WAKITAKA WAENDELEE KUPOKEA MISAADA YAO BASI WAACHANE NA HAYO MAMBO YA YESU YESU....NA KWA KUWA HAKUNA BABA MWINGINE ZAIDI YA MBINGUNI NA HAKUNA NAMNA BINADAMU ANAWEZA KUISHI KWA MISAADA YA BINADAMU MWINGINE BAADA YA KUMKANA MUNGU WA KWELI.
SASA WATOTO HAO WAKO KWENYE ENEO LAO LA SHULE WANASOMA NA WANAYO MIRADI AMBAYO BADO HAIJAANZA KULETA FAIDA ILI WAWEZE KUJIENDESHA WENYEWE, NAHIYO ITAKUWA HIVYO TU BAADA YA MIEZI MITATU AU MINNE KUANZAIA SASA.
WATOTO HAWA KWA SASA HAWANA CHAKULA KABISA, NA HATA LEO WAMEKULA KWA MSAADA WA KIJANA MMOJA ALIJITOLEA YEYE BINAFSI NA FAMILIA YAKE....MBALI NA GHARAMA NYINGINE ZA UENDESHAJI KAMA MISHAHARA/POSHO ZA WALIMU;
************************************************************************************************
KITUO HIKI KINATUMIA UNGA KILO 30, MAHARAGE KILO 14 NA SUKARI KILO 5....NA IKIWA NI WALI,BASI HUHITAJIKA KILO 30 ZA MCHELE KWA MLO MMOJA....NA PIA UNAWEZA KUCHANGIA MAFUTA NA FEDHA KWA AJILI YA VITU VINGINE VINAVYOWEZA KUHITAJIKA.
************************************************************************************************
NINAAMINI KWA MSAADA WA WATANZANIA WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA WATOTO WA KITANZANIA, WATOTO HAWA HAWATAKOSA CHAKULA KWA SIKU HIZI 120 ZA MPITO KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA WENYEWE, SIO LAZIMA ULETE MSAADA MKUBWA SANA, LAKINI NAAMINI UNAWEZA UKAJITOLEA CHAKULA KIASI JAPO KWA SIKU MOJA TU KAMA SIO TATU, YAWEZA KUWA WEWE BINAFSI AU KAMPUNI AU FAMILIA AU KANISA, LAKINI NINACHOKIAMINI NI KUWA KAMA KWELI TUNAAMINISHA KUMPENDA MUNGU NA KUWAPENDA WATOTO WATANZANIA TENA WANAOLELEWA KATIKA MALEZI YA KIMUNGU BASI LAZIMA WATOTO HAWA WATAISHI BILA HOFU YA CHAKULA KWA SIMU HIZI 120, NA KWA HAKIKA BWANA ATAKUBARIKI SAWASAWA NA IMANI YAKO KWAKE
YAK 1:27 "....DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGUBABA NI HII, KUWATAZAMA WAJANE NA YATIMA KATIKA DHIKI YAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO NA MAWAA"
MSAADA HUO UNAHITAJIKA SANA SANA, NAAM KWA NAMNA YOYOTE ILE UNAYOWEZA KUCHANGIA BASI USISITE,FANYA HIVYO...SADAKA YAKO YA KUWALISHA WATOTO HAWA HAITASAHAULIKA HATA KIDOGO, UNAWEZA KULETA MCHANGO WAKO WA CHAKULA PALE OFISI ZA NIIM COMPUTERS, MOROCO HOTEL AU UKATUMA MCHANGO WAKO WA FEDHA KWA NJIA YA SIMU, NAAM KWA MAULIZO ZAIDI
TAFADHALI WASILIANA NA WASIMAMIZI NA WARATIBU WA ZOEZI HILI KWA NO.
0713 26 1425 na 0754 527955, pia 0783 757051
KWA NIABA YA WASIMAMIZI WA KITUO HIKI NINAWASHUKURU HATA KABLA HAMJAFANYA JAMBO LOLOTE MAANA NAAMINI UMEGUSWA NA UKO TAYARI SASA KUWASAIDIA WATOTO HAWA...KAMA TUNAWEZA KUCHANGIA SHEREHE ZA HARUSI, NAFIKIRI HATMA YA WATOTO HAWA NI ZAIDI,MUNGU AKUBARIKI UNAPOMSHIRIKISHA NA MWENZAKO!!
Imeandikwa na
KING CHAVALA MC
KWA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.
Friends On Friday Twende Kazi
Friends On Friday Event Number Moko ya Vijana wa madhehebu yote ilifanyika Ijumaa ya Wiki Iliyopita na safari Hii Friends On Friday Inakujua tarehe 6 Sept, 2013 ikiwa na Jina "FOF Maridadi"
Blogger Ambwene Mwamwaja Afafanua Gospel Kitaa Blog Inavyokusanya Habari
Mtangazaji wa WAPO Radio na Mmiliki wa Blog Ya Gospel Kitaa, amefunguka na kueleza kuwa ana network Kubwa ya watu wanaompa habari karibu nchi nzima na Kuweza kuziratibu akiwa Nchini Uingereza. Blogger huyo maarufu Ambwene Michael Mwamwaja alieleza kuwa mbali na kupata taarifa hizo pia huzifanyia uthibitisho wa habari kabla hajazituma katika Blog.
Blogger huyo maarufu ambaye kwa sasa anaishi Nchini Uingereza yuko nchini kwa mapumziko mafupi ambapo alieleza kwa kina namna ambavyos aliweza iwakilisha Tanzania katika Tuzo za Africa Gospel Music Awards ambapo Mwanamuziki wa Injili Kutoka Tanzania Christina Shusho aliwakilisha Vema nchi ya Tanzania.
Mwamwaja ni Mmiliki wa blog ya www.gospelkitaa.blogspot.com aliyasema hayo alipokuwa akihojiwa na Kipindi nambari one cha Gospel Tanzania "Chomoza".
KUNA VITA NDIO, LAKINI PIA KUNA SHEREHE JESHINI....HONGERA LUTENI FRANK MNDEME!!!
Kwa namna ya kipekee, natamani uone ni jinsi gani Shughuli ya Kuoa inavyoheshimiwa hata na Jeshi....wanaamini mwanajeshi pia anahitaji msaidizi na mwenza, na ndio maana ukianza mafunzo ya jeshi,ama kujiunga na jeshi na kuwa mwanajeshi....unatakiwa kulitumikia jeshi ukiwa single kwa miaka 6 (Sijui kama katazo hili lina nguvu hata sasa) na ndio unaruhusiwa kuoa kiheshima!!
![]() |
Luteni Frank Mndeme na mkewe |
![]() |
Unaweza kuona jinsi heshima ilivyo... |
![]() |
Yaani hii ni Official Hongera! |
HUU NI MFANO WA HARUSI ZA KIJESHI, NIMEPATA PICHA CHACHE ZA NAMNA ILIVYOKUWA WAKATI LUTENI FRANK MNDEME ALIPOOA SIKU CHACHE ZILIZOPITA!!
Huyu ni mdogo wa Mathew Mndeme, mmoja wa waandishi wa Blog hii....Simple Man with always a story to tell!
CHAVALA IDEAS PLATFORM Inawatakia kila lakheri na fanaka ya maisha mema wanandoa hawa...furaha ya ndoa na upendo wa kweli udumu na kukua kila leo,Amen!
Hotline; +255 713 883 797
Papaa On Tuesday.....Kwanini Hatujifunzi Kutokana na Makosa?
Unakuta makosa ya matumizi mabaya ya Mshahara wako yanajirudia kila mwezi hakuna siku ambayo mshahara ukakutana, mshahara wa mwezi huu haujawahi kusalimiana na mashahara wa mwezi ujao wanapishana siku wiki nzima, makosa hayo yamekupelekea kwenye madeni ya kila mwezi unajikuta wewe ukishika mshahara huna chako umewashikia wengine hela zao unabaki kujisikia vibaya kujisikia vibaya hakukusaidii mwezi ujao usirudie makosa, kujifunza katika tatizo na kuamua kubadilika ndiko kutakusababisha kubadilika kutoka katika hali uliyonayo.
Kuna watu wamewahi jichukia nafsi zao na tabia zao, na kuna wengine waliwahi jiapiza kuwa hawata rudia tena lakini ndo utadhani wamejiapiza kufanya zaidi ya alivyokuwa anafanya mwanzo. Kujifunza ni mfumo wa kila siku lakini kujifunza kutokana na Makosa hata Serikali yetu imekuwa ni tatizo. Makosa yale yale yanayotokea kwenye Serikali na kupelekea upotevu wa fedha nyingi za Serikali, ndio huo huo pia utatokea mwakani na mwakakeshokutwa pia. Makosa yale yale yanayoitesa CCM ndiyo makosa hay ohayo yatatesa NCCR-Mageuzi ndo hay ohayo yataitesa CHADEMA na ndo hay ohayo yataitesa TLP. Sababu zile zile za kufeli kwa wadogo zetu kwenye shule za Sekondari mwaka huu ndo hizo hizo pia zitasababisha mwakani watu wafeli. Makosa yale yale tuliyofanya kwenye Uchaguzi wa mwaka 2010 ndo yale yale 2015 kwani kuna jipya??
Changamoto kubwa sana ambayo inainyemelea Tanzania yetu ni watu kupenda kuambiwa, yaani akiwa anaumwa yeye mwenyewe hawezi kujitesa kunywa maji, ila Daktari akimwambia asipokunywa maji atakufa basi atakunywa maji mpaka atawaboa, wengi wanaenda Gym siku hizi si kwa sababu wanapenda mazoezi aaah wanaenda “kujikinga na magonjwa” wakisha pungua unene wanarudia yale yale. Kama hauna “mood” ya mazoezi yatakushinda utafanya siku mbili tatu unaacha why?hatujifunzi kupitia makosa yetu.
Kila mtu anapaswa kujifunza kutokana na makosa, usiogope kukosea sababu ni sehemu ya kujifunza ukiogopa kukosea hautakuja kuweza ila ukikosea unajua kwanini ulikosea na nini au wapi urekebishe. Kabla ya kujua kuendesha baiskeli wengi walidondoka, kabla ya kuweza kuendesha gari wengi waligonga kwenye Reverse ila walipogonga ndivyo walivyozidi kujifunza. Kujifunza ni gharama,gharama ya kujifunza ni ndogo ukilinganisha na gharama ya kurudia kosa lile lile, kuna mambo ambayo pengine yana gharimu maisha yako kwa sasa kwa sababu tu kukosea kuchagua kitu Fulani, pengine gari ulilonunua linakugharimu sababu tu ya kukosea kuchagua, wengine wenzi wao wa maisha, wengine ni taaluma zao kila mtu ana “makovu yasiyokuwa na hisia” ambayo yanatesa watu wengi.
Zahma ambayo mtu ameipata kutafuta nyumba ya kupanga na kujikusanyia kodi ya nyumba ndo makosa hay ohayo yatatokea katika kutafuta nyumba na kukusanya kodi, kwanini?sababu hatuna utamaduni wa kujifunza kutokana na makosa. Makosa yale yale waliyofanya wazazi wetu katika umri wao wa kufanya maamuzi mazito ndiyo hayo hayo pia yatatokea na kwetu na kwenye vizazi vyetu. Usipojijengea utamaduni wa kujifunza hakuna wa kukufunza kwa kizazi chetu. Kwani wewe unafunzwa na nani makosa yale ambayo wewe uliyafanya ukaharibikiwa mapema si ajabu watoto wako pia yakawatokea kwa mwamvuli wa "uzungu" watoto wako katika umri wako ule wa kujua mema na mabaya watadondokea katika shimo lile lile. Tarehe ya mtoto kuzaliwa iko mbele kuliko anniversary ya Harusi yenu.
Kuna watu huwa wanasema usijifunze kwa walioshindwa maana na wewe utashindwa, kuna mtu aliwahi sema if you have never done any mistake,you have never tried something new. Kwanini uogope kujifunza kwa walioshindwa, kujifunza kwao kwenye mapungufu yao inasababisha mwerevu kujua njia gani aspite, kujifunza kwa waliofanikiwa peke yake ni mfumo ambao tumetengenezewa ili kutujengea ujasiri wa kuogopa. ndio maana kwenye interviews hata za ndoa utakuta wanaitwa watu ambao wamefanikiwa wanaonesha namna ambavyo wamefanikiwa mbona hatujawahi waita watu ambao wamechemsha tukawahoji kwanini walichemsha?kisa na mkasa eti hatuna jipya la kujifunza kwa walioshindwa ni kweli hatuna la kujifunza, katika kushindwa kwako mambo mengi ni kweli huwezi mfunza mtu?labda kama hatujajua makosa yetu ni yepi ndio maana hatuwezi wafunza wengine kile tulichokosea. Wote tunapenda story ya Petro aliyemkana Yesu mara tatu kisha akatengeneza, lakini hakuna mtu anayejifunza kwa Yuda aliyemkana Yesu kisha akajitundika kitanzi.
…//Papaa
0713 494110
UNAFIKI ULIOJIFICHA NYUMA NA MANENO YA MARAFIKI... "TUKO PAMOJA SANA"!!!
SALAM KWA WOTE!
Na amini watu wote tuko vizuri na bado tunakazana kuzifikia ndoto za maisha yetu!
Leo nimesukumwa kuzungumzia jambo moja hapa ambalo naona likiachwa hivyo litakuwa tatizo,tena tatizo kubwa.
UTANGULIZI;
Katika haya maisha hakuna mtu anaweza kuishi peke yake, sio tu kwa maana ya mwenza wa maisha ila namaanisha bila mtu mwingine yeyete, maana huwezi kuwa kila kitu na huwezi kufanya kila kitu mwenyewe kihusuyo maisha yako...una ndoto yako ya kumiliki Chuo kikuu ni sawa, lakini kuliweka hilo wazo kwenye maandishi ya kusomeka unahitaji watalaamu wa kuandika, kabla hujaanza kufanya lolote, unatakiwa upate mwongozo kwa wale waliotangulia na hapo unahitaji watu wengine.....kwa ufupi kila hatua utakayopiga utawahitaji watu,aitha kwa kuwaomba au kuwaajiri kwa maana ya kuwapa kazi na kuwalipa. hata ukitaka tu kutoka kwenda mjini lazima uhitaji dereva na konda na hata kama una gari binafsi kuna saa utamuhitaji muuzaji wa mafuta....KIMSINGI "KUISHI" NI KURAHISISHIANA MAJUKUMU KWA KILA MMOJA WETU KWA FAIDA YA KILA MMOJA WETU!.
Kwa msingi huo nataka utambue kuwa UNAHITAJIKA KUWASAIDIA WENGINE kama vile ambavyo na wewe UTAWAHITAJI WENGINE KUKUSAIDIA kufikia ndoto za maisha yako!
DHANA YA MAISHA;


UNAFIKI NISIOUPENDA.....
Kama umejitambua na unajiheshimu ni wazi kuwa na watu wanatambua hilo na sawasawa na kujiheshimu kwako ndio na watu wanavyokuheshimu. Ukiona mtu amekufuata na kukuuliza jambo lolote lile aitha anataka kulifahamu ama anataka ushauri wako au zaidi anaomba ushiriki wako....basi imekupasa kwanza kumshukuru sana Mungu kwa nafasi hiyo, hata kama hutafanya lolote katika haya anayoweza kuwa anayahitaji....nasemma hivyo ili ujue yafuatayo;
KWANZA UMETAMBULIWA KUWA UNAWEZA KUWA MSAADA KATIKA HILO.
PILI UMEHESHIMIWA SANA, MAANA WAKO WENGI LAKINI UMEONEKANA WEWE
TATU ULICHONACHO NDIO KAZI YAKE HASWA,MAANA TUMEPEWA ILI KUFAIDIANA.
Sasa kama ni hivyo basi ukipata nafasi hiyo mshukuru Mungu na baada ya hapo Omba hekima ya namna ya kujihusisha na jambo hilo na kama unaona huwezi kuhusika kabisa unaweza kumjibu kwa hekima SAMAHANI MIMI SITAWEZA, na yamkini ni vizuri hata ukimwelekeza kwa mtu mwingine unayeona anaweza kuwa na msaada!
Sasa usije ukadhani kwasababu una elimu ya juu sana au una umaarufu mkubwa au una kipaji sana au ni kiongozi maarufu au pesa kuliko wengine, ndio maana ukafuatwa wewe HAPANA!!
jIFUNZE Kuwaheshimu na kuwakubali wengine katika yote wanayofanya yanayostahili heshima....na mara zote HEKIMA NA MAWAZO MAZURI hutokana na watu tusiowadhania!
SASA SIKU HIZI KUNA NAMNA WATU HUKWEPA MAJUKUMU NA KUDANGANYA KWA NJIA YA MZUNGUKO, MTU ANAOMBWA JAMBO AU ANASHIRIKISHWA AU ANAALIKWA SEHEMU FULANI....HALI AKIJUA HANA NIA WALA MPANGO MOYONI AU NAFSINI MWAKE KWA KUSHIRIKI AU KUSHIRIKIANA....ANAISHIA KUTOA MATUMAINI FEKI ATI....."TUKO PAMOJA" AU "HAMNA NENO MTU WANGU" na hapo unamuaacha huyo ndugu akiwa na matumaini makubwa na ikifika saa ya jambo lenyewe usitokee kabisaaaa!!
Sasa ninafikiri ni wakati mzuri wa kujirekebisha sasa, kama huna nafasi au huwezi kumsaidia mtu kwa namna yeyete ile wewe sema tu....SAMAHANI NDUGU KWA HILI SITAWEZA!
Naamini hii itakusaidia pia kuwa HURU na kuwa MKWELI!
HIYO TABIA YA KUMWAMBIA MTU TUKO PAMOJA NA KISHA NYUMA YAKE UNAMNG'ONGA SIO HATA KIDOGO....TUJIREKEBISHE!!!
Ukiona inakufaa unaweza kuendelea nayo lakini kuna wakati itakugharimu tena sana, maana watu huwa wanaambiana yote yanayokuhusu na kama ni mambo ya kukalaisha basi ndio habari husambaa zaidi kuliko hata nzuri!
MFANO HAI;
Kuna mtu mmoja mahali fulani alikuwa anajifanya yuko bize kuliko hata ubize wenyewe, basi hata akiletewa kadi za michango ya harusi au shughuli mbalimbali alikuwa akijibu aaah tuko pamoja aisee....basi zingine anachangia na zingine hakuchangia na hata zile alizochangia nyingi hakuwa anahudhuria....naam hata ikitokea misiba jirani alikuwa anatuma rambirambi na kusema aaah jamani tuko pamoja kisha anaondoka....basi watu walimvumilia sana na hakuna nafasi watu walipata wasaa wa kumsema zaidi ya marafiki mmoja mmoja ambao aliwachukulia poa na kusema...aaah nimewaelewa jamani....tuko pamoja sana!
Basi ilitokea siku mmoja siku moja alipata msiba wa Baba yake mzazi ambaye alikuwa anaugulia kwake, watu walipata taarifa za msiba na wengi wao wakasema hapa ndio mahali pa kumuonyesha UPAMOJA WETU....basi wengi walifika na kutoa pole na kuacha rambirambi (tena nyingi kuliko kawaida) na wao walisema tuko pamoja katika majonzi haya na kuondoka zao....basi kwa kadri muda ulivyokuwa unakwenda alikuwa akipokea rambirambi na pole za watu wanaokuja na kuondoka kama vile ile ni shule ya kutwa ama kituo cha kupigia kura....basi pale msibani palikuwa doro kabisa na hapo ndio akaanza kuona kimbembe cha "TUKO PAMOJA"....basi msiba ulikaa siku ya kwanza yote hamna kitu,basi akawachukua vijana ili awalipe na wakachimbe kaburi, na wao walichukua pesa na wakamwambia tuko pamoja na wao wakaenda makaburini na kuanza kupiga stori, mpaka siku ya pili inaisha baada ya kufoka sana ndio wakachimba tena refu kupita kawaida...naam siku ya tatu ndio ya mazishi hakuna hata mmoja anajigusa kwenda, na hapo alienda kwa kiongozi wa mtaa na kumuomba awaite watu, naam watu walikuja na wakaenda mpaka makaburini kimyakimya,hakuna mtu kulia wala kuzungumza na walipofika pale....watu walimtolea madukuduku yao yooote na wakasema ili iwe fundisho kwa wengine,kabla ya kuzika....ALALE JUU YA UDONGO ULE WA KABURI PALE JUU,NA HAPO AKACHARAZWA BAKORA ZA KUTOSHA MBELE YA MKWEWE,WATOTO NA NDUGU ZAKE NA ndipo ibaada ya maziko ikaanza na kila hatua ya kuzika alipaswa kushiriki ili ajue huwa inakuwaje....alisaidia kushusha jeneza chini na kabla mtu yeyeote hajagusa chepeo,alianza yeye kufukua mpaka alipochoka hoi ndio wakamsaidia,na hilo lokawa fundisho kwake na kwa wengine wote mtaani kuwa pesa sio kila kitu,ila unahitajika wewe!!!
ACHANA KABISA NA HUO UNAFIKI WA KUSEMA TUKO PAMOJA HALI HUNA HATA KIMOJA KINACHODHIHIRISHA UPAMOJA HUO!!!
(Watu wawili hawezi kwenda njia moja isipokuwa wamepatana.....hivyo hamna Upamoja wa maneno bila matendo na mapatano)
AHSANTE SANA, UBARIKIWE SANA KAMA UMENIELEWA!!!
Fredy Erasto Chavala
<King Chavala(MC)>
+255 713 883 797
facebook; King Chavala MC
Twitter @kingchavala
CHRIS MAUKI LIVE IN INTELLECTUAL MEETING AT VCCT ON 4TH AUGUST 2013!!!

............We
all desire to move from the ground we are standing now to the higher
ground we've been dreaming about. But the going is never easy, thats why
you need to equip yourself everyday with new informations and skills...
Yesterdays intelligency can not solve todays challenges... On that groud Chriss Mauki
(A psychologist and Lecture from University of Dar-es-Salaam will be
sharing on a topic SETTING GROUND FOR YOUR TAKE OFF at VCCT Tarbenacle
this coming Sunday from 1630hrs.You will have a great time to exchange
Ideas and Network with other professionals.. CEOs, Managers, Business
people etc.. Please Plan not to miss, u will never be the Same.
"BY PROSPER MWAKITALIMA"
FOR MORE INFORMATION,PLEASE DIAL 0713 905118
KARIBUNI SANA NYOTE!!!
Papaa On Tuesday.....Wengi tu Waathirika Wa Makovu Yasiyokuwa na Hisia!!
Mabaka
Yasiyokuwa na Hisia ana Makovu yanayotokea bila mwanadamu mwenye kuwa
na uelewa kuwa kuna kitu kinaendelea kwenye mwili wake, hali hii
hupelekea mtu kutibu matokeo ya ugonjwa na sio ugonjwa wenyewe. Kati ya
dalili nyingi za wagonjwa wa ukoma ni waathirika kupata madhara pasipo
wao kuwa na taarifa (sense) katika miili yao. Wagonjwa wengi hata wale
wa Saratani Ya Ngozi hukuta tu wana mabaka ama makovu kwenye miili yao
ambayo yametokea pasipo wao ku-sense kama kuna mabadiliko katika miili
yao. Nilipokuwa Mbeya wakati fulani Pastor Matthew Sasali (Mdogo wangu)
alinikumbusha kuwa dhambi kwenye maisha ya mwanadamu ni kama makovu
yasiyo na hisia, huanza pole pole mwisho wake ni kama ambavyo inaelezwa
Mshahara wa dhambi ni Mauti.
Kila mtu kwa nafasi yake anaweza kuitazama Jamii ya leo na kuona, mambo mengi yanayotokea
sasa yalianza pole pole na kudhaniwa kuwa hayatakuwa na madhara makubwa
kwenye Jamii lakini kwa sasa matatizo hayo yamekuwa sugu vya kuchosha.
Issue za ufisadi zilianza pole pole kwenye Jamii yetu, leo hii kwenye
Jamii si ajabu mwovu anakumbatiwa na mwema anachukiwa, ukionekana
unaikosoa Serikali unaambiwa unahatarisha amani ya nchi. Leo hii watoto
wanadiriki kuwapeleka wazazi wao mahakamani, leo hii idadi ya mashoga
inaongezeka kwa kasi lakini kuna siku hali haitakuwa hivi sababu ni kama
Jamii imekufa ganzi. Watu wanaokamatwa na madawa ya Kulevya kila siku
wanakuwa wengi lakini mwisho wa siku tunazoea tu
Zamani
idadi ya wana cheat kwenye mahusiano ilikuwa ni ndogo sana na hata kama
mtu alikuwa anatoka nje ya ndoa ilikuwa ni Siri sana lakini siku hizi
yaani inajulikana kabisa ni nyumba ndogo, sio sasa wanandoa kuaminiana,
hali ngumu ya maisha na kupenda mafanikio ya haraka hataka yamepelekea
wanandoa wengi kusaliti ndoa zao, waume za watu hawaaminiki, wake za
watu mule mule, enzi hizo watu walikuwa wanaugopa Mungu kwa sana si
makanisani si misikitini, siku hizi kuna mambo yanatokea na watu kama
wanayapotezea lakini mwisho wa siku yatatengeneza maumivu na mateso
katika maisha na kutunyima furaha.
Angela
(sio jina kweli) niliwahi kukutana nae katika mojawapo ya mizunguko
yangu katika mashule na vyuo. Mdada huyu alikuwa ni kidato cha 6, baada
ya mimi kufundisha mambo kadha wa kadha ya maisha, dada huyu aliniomba
tuzungumze maana alikuwa anahitaji msaada. Katika maongezi yake
alinieleza kuwa alianza kuingiliwa kinyume cha maumbile akiwa kidato cha
kwanza, kwa wakati huo akiwa kidato cha sita alikuwa si kwamba si tu
anapenda mchezo huo bali amekubuhu, hajisikii raha kufanya mapenzi kwa
njia ya kawaida isipokuwa mpaka ameingiliwa kinyume cha maumbile. Na si
kwamba anapenda hiyo hali amejitahidi mbinu mbalimbali za kukataa hiyo
tabia ila alieleza huwa inaondoka na kurudi. Nilipomdadisi ilikuaje
mpaka akaingia katika huo mchezo alieleza boyfriend wake waliyeachana
ndiye aliyemfundisha na kumzoesha, alijua ni kitu cha kawaida na
kinaweza kuepukika lakini si hivyo. Unafanyaje pale mume wako wa ndoa
ama mchumba wako akataka kukuingilia kinyume cha maumbile, umewahi sikia
habari hii mara ngapi lakini ni kama watu wanaipotezea, hili ni kovu
linalotokea bila kusikia maumivu ya kidonda. Na mwisho wa siku tutakuwa
tumesharudi katika enzi za Sodoma na Gomora
Leo
hii umesikia mara ngapi matamko mbalimbali ya kidini yakitolewa kila
mmoja akimtishia mwingine, lakini hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa
kukomesha hali hiyo. Inawezekana hisia za kuhisi madhara yake kwenye
Serikali yetu zimekufa lakini kidonda hiki kina madhara makubwa hapo
baadae zaidi ya madhara ya ugonjwa wa Saratani. Kuna siku raia watajitoa
mhanga ndipo tutashuhudia kitu ambacho leo tunakidharau, watu wanapigwa
mabomu, watu wanapigwa risasi, risasi inaua, kuna siku watu watachoka
kukaa hai kufa kwao si tatizo sana, kwa kusema hivi lazima Jamii ianze
kutazama huu mwamko wa Kijamii kwa sasa na kila mtu kudai haki yake kwa
mabavu hata pale palipohitaji subira na busara tutafika wapi?hii hali
tusipoiona kuna siku yataibuka mambo.
Leo
hii kuna matatizo ambayo pengine yalianza zamani na kudhaniwa kuwa ni
madogo, wanaume wengi wanaoangalia pornography hawakuanza jana, ni kitu
ambacho wengine kimeshajengeka kwao, kuna wanaume wao kujichua ni kama
wameshikiwa risasi kuwa wasipofanya watakufa. Wengine ni wafanyakazi na
vyeo vyao lakini sasa wanateseka na tabia hiyo wengi wao hawapendi
kufanya hayo lakini wakati wanaanza walidhani ni kitu kidogo ambacho
hakiwezi kuathiri maisha yao. Wengine mpaka kwenye ndoa hawasikii raha
bila ya kujichua wao wenyewe. Haya ni Mabaka tuliyoyadharau kwa kudhani
hayana madhara leo hii yameacha alama zisizofutika kwenye tabia zetu.
Tabia
zetu wakati mwingine zimekuwa ni tatizo la kudumu, wengine wetu
uaminifu sasa imeanza kuwa issue, maana kuna wengine walianza tu
polepole kwa ahali ilivyo sasa sio kwamba hawataki kuwa waaminifu, No
wanapenda sana kuwa waaminifu issue inakuja tu kuwa wameshaathirika na
kutokuwa waaminifu, kwa kuupuuzia kwao mambo madogo madogo wamejikuta
wamepoteza opportunities nyingi sana kwenye maisha yao. Watu
wanatamani kukuamini lakini tabia huwa zina athiri sana maisha yetu ya
kila siku. Ndoa zetu zimeathirika na tabia zetu kazi zetu zimeathirika
na tabia zetu, mahusiano yetu na Mungu yanasua sua kutokana na tabia
zetu. Can Something good come out of you?
Asilimia kubwa ya Vijana wa Sasa wamesha experience maumivu kwenye mioyo yao juu ya mahusiano. Siku moja tukiwa kwenye Conversation kali kwenye Facebook Wall yangu, mmoja wa Marafaki zangu aliongea akisema kwa namna moja ama nyingine suala hili la kuumizana linatokana na Wanaume kutokuwa na Msimamo katika kile wanachokitaka. Kuto kuwa na Msimamo ni Matokeo ya kitu ambacho kinaendelea kwenye Jamii, kwanini watu hawana misimamo katika kusema sitaki A nataka B, Wadada wengi wamejikuta wakitupia wakaka lawama kwa kuwauzisha Sura mwisho wa siku inakula kwa Mdada. Kizazi hiki kinaona ndoa ni jambo la fahari kuliko jambo la fungamano ndo maana unakuta ndoa ilifungwa kwa mamilioni ya fedha baada ya mwaka watu wanataka kutoka, nani alaumiwe. Mioyo ya wengi imeshajeruhiwa na kubutuliwa kama kombolela hakuna tena penye sehemu ya kupenda. Ukitaka kujua una kovu lisilokuwa na hisia ni pale unapopata mpenzi mpya halafu ukabaini ameanza tabia kama za yule aliyekimbia kuna kitu kunaingia ndani yako ghafla si unajua uking'atwa na nyoka???
Asilimia kubwa ya Vijana wa Sasa wamesha experience maumivu kwenye mioyo yao juu ya mahusiano. Siku moja tukiwa kwenye Conversation kali kwenye Facebook Wall yangu, mmoja wa Marafaki zangu aliongea akisema kwa namna moja ama nyingine suala hili la kuumizana linatokana na Wanaume kutokuwa na Msimamo katika kile wanachokitaka. Kuto kuwa na Msimamo ni Matokeo ya kitu ambacho kinaendelea kwenye Jamii, kwanini watu hawana misimamo katika kusema sitaki A nataka B, Wadada wengi wamejikuta wakitupia wakaka lawama kwa kuwauzisha Sura mwisho wa siku inakula kwa Mdada. Kizazi hiki kinaona ndoa ni jambo la fahari kuliko jambo la fungamano ndo maana unakuta ndoa ilifungwa kwa mamilioni ya fedha baada ya mwaka watu wanataka kutoka, nani alaumiwe. Mioyo ya wengi imeshajeruhiwa na kubutuliwa kama kombolela hakuna tena penye sehemu ya kupenda. Ukitaka kujua una kovu lisilokuwa na hisia ni pale unapopata mpenzi mpya halafu ukabaini ameanza tabia kama za yule aliyekimbia kuna kitu kunaingia ndani yako ghafla si unajua uking'atwa na nyoka???
Wengine
wamekuwa wakihangaika na matumizi mabaya ya fedha kiasi kwamba
wanajitahidi kujidhibiti wanashindwa, kosa alilofanya mwezi uliopita
amejikuta na mwezi huu amelifanya, wengine wamejitahidi kuacha matumizi
ya hovyo lakini imeshindikana kilichotokea wamekubali kuwa hawawezi
kubadilika, ilipoanza ni kama haikuwa na madhara lakini wengine sasa its
too mucha na still hawaoni kama watasaidika katika hilo, wamekubali
matokeo. Wengine tabia za kuzira, ajabu unakuta mtu mkubwa kabisa eti
anazira, lakini hakuanza leo tabia hii imekuwa polepole bila ya watu
wenyewe kujijua imejijenga ndani yao. Wengine ni hofu, wamejawa na hofu
mpaka unnecessary. Kuna rafiki yangu yeye kila kitu anaogopa hasa
inapofika suala la ndoa yale aliyoyasikia kutoka kwa watu na
aliyoyapitia yamemjaza hofu kuwa katika dunia hii kama kuna mwanaume
ambaye yupo kabisa hawezi cheat na akabaki kuwa mwaminifu kwake peke
yake. Hofu anabadili namna ya kutazama mambo, hofu inamadili namna ya
kuishi na kuongea na kuamua mambo mengi, hofu ikikujaa unaweza ukaufunga
hata uwezo wako wa kuwaza na kupambanua mambo, hofu inatawala.
Inawezekana
kuna jambo ulishawahi dhani umelisamehe na kuliachilia lakini kila lile
jambo linapotajwa kuna mkwaruzo ndani ya moyo wako hutokea, kama
umewahi umizwa na mapenzi ukiwasikia watu wanaongelea mapenzi unatamani
usimkumbuke mtu aliyekutenda, ikitokea umemuona njiani anakuja unatamani
kubadilisha njia, yamkini uliwahi dhurumiwa ama pata hasara ya biashara
yale maumivu bado yameganda kwenye nafsi, inawezekana ni ofisi
waliyokufukuza sometimes back ukisikia jina la ofisi moyo unakuuma.
Makovu haya ya nafsi hu-develop tabia ambayo yamkini hukuwa nayo hapo
awali. Umejengeka na kuto samahe, umejengeka kuwa na tahadhari nyingi
zaidi, Umejengeka kuto amini amini mwenzi wako akishika tu simu unajua
anachat na wanawake wake unatamani kumwamini lakini nafsi yako imesha
develop tabia iliyotengenezwa kutokana na jeraha. Ukimsikia mtu anasema
"wanaume wenyewe wote vimeo" jua ana jeraha ama ukisikia mtu anasema
"wanawake wote wanafanana" jua ana jeraha lake la kwenye nafsi kila mtu
amejawa na hofu ya kuogopa kutoneshwa jeraha la nafsi alilowahi kupitia
hapo kabla.
Wengi
tunateseka si kwa sababu tunataka kuteseka, hofu zinatawala maisha
yetu, kujilaumu kumekuwa ni sehemu ya maisha yetu,kutokuamini wengine
imekuwa ni sehemu yetu. Wengine wanafanya biashara wakiwa wameshajiandaa
kupata hasara, wengine wameingia katika ndoa wakiwa wamejiandaa
kusalitiwa, wengine wameingia katika ajira wakiwa tayari kuiba. Mabaka
yasiyo na hisia yamekuwa kiasi kwamba tuko tayari kuumia au kuumizwa
hata kuumiza kila mtu yulo tayari kwa lolote ovu kutokea kuliko wema.
Haya mambo yalianza polepole katika maisha na jamii yetu sasa
yameshatuathiri. Unayosikia leo Tunisia au Misri hayakuanza tu ghafla
ila yalianza polepole.
Hakuna
mtu anayekufahamu vizuri kuliko wewe mwenyewe unavyojifahamu ipo haja
ya kujichunguza na kubadilika kabla mwaka haujafika mbali.
…//Papaa
0713 494110
samuel_sasali@yahoo.com
MWISHO WA SEPTEMBER NDIO MWISHO WA KUTOA MICHANGO KWA SAMUEL SASALI!!!
Hello habari zenu!
Natumai nyote mko vizuri mnaposoma habari hii!!
Naamini habari ya habari za Useja wa Papaa ziliwasikitisha sana na mlitamani mseme ila hamkuweza, naam maombi yenu Mungu akajibu na akampata Mchumba, ndio ni mchumba mkubwa tu wa kutosha Kitanda ,dressing table na kabati na bado sehemu ya kutembea inabaki.
Mlipozidisha maombi macho yake yakafungukia paleeeeee HKMU Mikocheni, naamini wengi habari ziliwafikia na hata kwasababu ya ufukunyuku wengine mkajua hata kabla yeye mwenyewe hajajua.
Alifuata taratibu zote za kijamii na kifamilia,Mali akalipa (Kama anadaiwa atamalizia mwenyewe) na shughuli za kuthibitisha kuwa yuko serious zilifanyika nyumbani kwa binti na baadae kanisani kwa kumvisha pete ya thamani sana, ndio kwasababu anampenda sana.
Ahsante kwa kushiriki hayo yoooote yaliyopita kwa maneno na simulizi......sasa ni wakati wako wa kushiriki kikamilifu tena kwa hali na mali.
Tarehe ya Harusi imeshatangazwa, 26th October 2013 pale Victory Christian Centre Tabernacle (VCCT) pale Mbezi beach A kwa Dr.Huruma Nkone na baadae taafrija kufanyika katika bustani kubwa ya pale Lamada Hotel,Ilala-boma saa moja mpaka tano usiku.
Yawezekana wewe ni rafiki,jirani,shabiki,msomaji wa blog, ndugu, mwanahabari mwenzie, labda mnoni mwenzie au mtoto wa mchungaji mwenzie au unasali pamoja nae,au mmewahi kupiga picha pamoja au umewahi kumwona na kumfurahia hata mara moja tu au basi ni rafiki yako katika mitandao ya kijamii au humjui kabisa ndio unamjua leo....ni sawa tu anaitwa Samwel Sasali,Papaa,The Blogger....basi hii ni nafasi yako kushiriki shangwe hii sambamba na marafiki wote wa muhimu hapa mjini kama vile Wachungaji,Wafanyabiashara,Wanasiasa,waimbaji,wanafunzi na wengine kadha wa kadha bila kumsahau Askofu Mkuu wa TAG,Dr Barnabas Mtokambali na burudani live itaendeshwa na John Lissu na bendi yake.
Nafasi ni chache sana ukilinganisha na Uwingi wa matafiki wa kijana huyu, hivyo nakushauri uchukue kadi yako mapema na uchangie kabla ya Septemba 30, maana baada ya hapo hata kama utakuwa na hela nyingi mkononi utakosa kadi.
Naomba kusisitiza tena na tena kama rafiki, kama pacha wake na kama mwanakamati kuwa NI MUHIMU KUSHIRIKIANA NA MWENZETU, NI MUHIMU KUCHANGIA LAKINI KWA SABABU YA UWINGI WA MARAFIKI UKILINGANISHA NA IDADI TUNAYOITAKA,NAAMINI UTAZINGATIA KUCHANGIA MAPEMA NA KUPATA KADI YAKO.
Kadi zinapatikana kwa Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi,Bwana Noell Tenga, Bwana Harusi Mtarajiwa, Samuel Sasali, Renee Lyatuu,James Temu(Uncle jimmy) na Kwa King Chavala.
Hata kama siku hiyo haufikiri kuwepo harusini,haitakuwa vibaya kama ukichangia japo 50,000/=na kuendelea kwa kadri Mungu alivyokubariki.
Kwa Bloggers na wanahabari msiache kunitafuta maana nina kadi zenu!!
KUMBUKA;
Ni hao tu niliowataja ndio watakupa kadi na sio mwingeyo, Tunatamani chango wako usiwe chini ya 50,000 ili tuweze kufanikisha shughuli ya mwenzetu!!
Kwa Mawasiliano zaidi;
Samuel Sasali 0713 494110/0686 255 269
Happy Lwendo; 0717 149085
Noell Tanga; 0713 261425
IMETOLEWA NA KING CHAVALA KWA NIABA YA KAMATI NA CHINI YA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.
Natumai nyote mko vizuri mnaposoma habari hii!!
Naamini habari ya habari za Useja wa Papaa ziliwasikitisha sana na mlitamani mseme ila hamkuweza, naam maombi yenu Mungu akajibu na akampata Mchumba, ndio ni mchumba mkubwa tu wa kutosha Kitanda ,dressing table na kabati na bado sehemu ya kutembea inabaki.
Mlipozidisha maombi macho yake yakafungukia paleeeeee HKMU Mikocheni, naamini wengi habari ziliwafikia na hata kwasababu ya ufukunyuku wengine mkajua hata kabla yeye mwenyewe hajajua.
Alifuata taratibu zote za kijamii na kifamilia,Mali akalipa (Kama anadaiwa atamalizia mwenyewe) na shughuli za kuthibitisha kuwa yuko serious zilifanyika nyumbani kwa binti na baadae kanisani kwa kumvisha pete ya thamani sana, ndio kwasababu anampenda sana.
Ahsante kwa kushiriki hayo yoooote yaliyopita kwa maneno na simulizi......sasa ni wakati wako wa kushiriki kikamilifu tena kwa hali na mali.
Tarehe ya Harusi imeshatangazwa, 26th October 2013 pale Victory Christian Centre Tabernacle (VCCT) pale Mbezi beach A kwa Dr.Huruma Nkone na baadae taafrija kufanyika katika bustani kubwa ya pale Lamada Hotel,Ilala-boma saa moja mpaka tano usiku.
Yawezekana wewe ni rafiki,jirani,shabiki,msomaji wa blog, ndugu, mwanahabari mwenzie, labda mnoni mwenzie au mtoto wa mchungaji mwenzie au unasali pamoja nae,au mmewahi kupiga picha pamoja au umewahi kumwona na kumfurahia hata mara moja tu au basi ni rafiki yako katika mitandao ya kijamii au humjui kabisa ndio unamjua leo....ni sawa tu anaitwa Samwel Sasali,Papaa,The Blogger....basi hii ni nafasi yako kushiriki shangwe hii sambamba na marafiki wote wa muhimu hapa mjini kama vile Wachungaji,Wafanyabiashara,Wanasiasa,waimbaji,wanafunzi na wengine kadha wa kadha bila kumsahau Askofu Mkuu wa TAG,Dr Barnabas Mtokambali na burudani live itaendeshwa na John Lissu na bendi yake.
Nafasi ni chache sana ukilinganisha na Uwingi wa matafiki wa kijana huyu, hivyo nakushauri uchukue kadi yako mapema na uchangie kabla ya Septemba 30, maana baada ya hapo hata kama utakuwa na hela nyingi mkononi utakosa kadi.
Naomba kusisitiza tena na tena kama rafiki, kama pacha wake na kama mwanakamati kuwa NI MUHIMU KUSHIRIKIANA NA MWENZETU, NI MUHIMU KUCHANGIA LAKINI KWA SABABU YA UWINGI WA MARAFIKI UKILINGANISHA NA IDADI TUNAYOITAKA,NAAMINI UTAZINGATIA KUCHANGIA MAPEMA NA KUPATA KADI YAKO.
Kadi zinapatikana kwa Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi,Bwana Noell Tenga, Bwana Harusi Mtarajiwa, Samuel Sasali, Renee Lyatuu,James Temu(Uncle jimmy) na Kwa King Chavala.
Hata kama siku hiyo haufikiri kuwepo harusini,haitakuwa vibaya kama ukichangia japo 50,000/=na kuendelea kwa kadri Mungu alivyokubariki.
Kwa Bloggers na wanahabari msiache kunitafuta maana nina kadi zenu!!
KUMBUKA;
Ni hao tu niliowataja ndio watakupa kadi na sio mwingeyo, Tunatamani chango wako usiwe chini ya 50,000 ili tuweze kufanikisha shughuli ya mwenzetu!!
Kwa Mawasiliano zaidi;
Samuel Sasali 0713 494110/0686 255 269
Happy Lwendo; 0717 149085
Noell Tanga; 0713 261425
IMETOLEWA NA KING CHAVALA KWA NIABA YA KAMATI NA CHINI YA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.
ZOOMING ZONE 0004.......Na PROSPER A. MWAKITALIMA, The T-shirt Printer tycoon!!!
HELLO HABARI!
NAAMINI MKO POA NA MNAENDELEA VIZURI, NILIKUWA KIMYA KWA
MUDA NA HII NI KWASABABU ZOOMING ZONE SIO MAKALA YA KILA SIKU AMA KILA MTU,
HIVYO LEO LENZI IMEMULIKA KIJANA MMOJA HAPA MJINI NA HUYU NDIO ATAKUWA……Zooming
Zone 004
![]() |
Zooming Zone 0004....Na Prosper A.Mwakitalima |
Huyu sio mwingine basi ni kijana mjasiriamali “SWAHIBA”
anayetamba na kujulikana sana kwa KUCHAPISHA T-SHRTS vizuri, nzuri na zenye
maneno mazuri hapa Mjini, Tanzania.
Naam pia ndio huyu ambaye habari zake zilivuma sana hapa
mjini kwa kupona“kufufuka” toka katika ajali mbaya sana sana pale maeneo ya
River side Ubungo 23/11/2011 iliyohusisha
lori la mafuta na gari yake ndogo,ajali ambayo ilichukua maisha ya watu kadhaa
akiwemo mama mmoja mjamzito ambaye alikatika kichwa(ilitisha sana kwa kweli)….lakini
Jambo la kushangaza ni kuwa kijana huyu alipona kabisa maana hakuvunjika mfupa
wala mshipa Zaidi ya michubuko kadhaa tu,hakuna aliyeamini hata leo lakini huo
ndio ukweli!
![]() |
Huwezi kuamini lakini huu ndio ukweli! |
Huyu pia ni mmoja wa washika dau na wawezeshaji wa Mtoko wa
marafiki Mjini uitwao “FRIENDS ON FRIDAY
(FoF)”, na ndio mbeba maono na mkurugenzi wa “SIFA TANZANIA”Mfululizo wa matamasha ya kumwinua Yesu hapa nchini
Tanzania.
Huyu ni PROSPER
ALFRED MWAKITALIMA a.k.a SWAHIBA a.k.a “The Next Billionaire” (King
Chavala tu anaruhusiwa kumwita “MY PS”)
NILIBAHATIKA
KUFANYA NAE MAHOJIANO HIVI KARIBUNI KWA KINA NA NIKAPATA MENGI SANA NA HAYA NI
MACHACHE KATIKA MENGI, AMBAYO NAAMINI YANAWEZA KUKUSAIDIA KUMFAHAMU VIZURI NA
YAMKINI KUJIFUNZA MENGI KUTOKA KWAKE, HUYU NI KIJANA WA KIPEKEE AMBAYE NI MFANO
WA KUIGWA NA VIJANA WA KITANZANIA…..FUATANA NAMI KATIKA MAELEZO YANGU KUHUSU
Papaa On Tuesday....Wakati Wa Jambo Ukipita, Itakusumbua..Kila Jambo na Wakati Wake!
Nina
Kila Sababu Ya Kumshukuru Mungu aliyetupa nafasi hii ya leo Kwa ajili
ya kuweza kulitimiza tena Kusudi la kuumbwa kwetu na kuwepo duniani.
Papaa
On Tuesday ya leo ni Tafakari ya rafiki yangu wa Siku Nyingi Mussa
Billegeya ambaye ni Mbunge Mtarajiwa wa Jimbo moja miaka michache ijayo
katika Kanda Ya Ziwa. Tafarakari hii aliitoa katika forum ya Marafiki
Huru.
Kuna
Msemo wa Kibiblia usemao kila jambo lina wakati wake, Naamini huu msemo
huwa uko sahihi kabisa. Lakini kifalsafa, Wanadamu huwa tunafarijiana
kwamba Ukiwa Hai Bado, It's Never Too Late!
Hivi Majuzi rafiki yangu Mussa akiwa Ofisini pale MANCON na Mkurugenzi Prosper Mwakitalima, wakiwa wanazungumza mambo mbali mbali ya maisha ikafika time ya kuongelea suala moja linahusiana na Kuoa. Prosper aligusia huo msemo, na kueleza kwamba hata kuoa huwa kuna wakati wake, na mtu asipooa wakati wake wa kuoa unapofika, inaweza ikamsumbua kuja kuoa baadaye - hata kama atakuwa anataka!
Juu ya Msemo huo ninajenga Papaa On Tuesday ya leo!
Ni kweli kabisa kwamba kila jambo lina wakati wake, NA KILA WAKATI KATIKA MAISHA UNA JAMBO LAKE! Tangu utoto hadi uzee. Ni muhimu sana kuelewa jambo la kila Wakati (na sio tu wakati wa kila jambo)!
Kuna namna nyingi sana za kutambua wakati wa jambo unapofika, na mara nyingi, watu wengi, huwa tunakuwa na bahati ya kufahamu kwamba wakati wa jambo fulani maishani mwangu umewadia, au basi, huwa tunaweza kufahamu kwamba Jambo la Wakati Huu ni hili! Kwa bahati mbaya sana, watu wengi huwa tunaona kama vile linalowezekana leo hata kesho litawezekana - KOSA!
Wakati wa jambo unapowadia, huambatana na mambo mengi ikiwa ni pamoja na Nguvu ya Kulitekeleza, Hamu ya Kulitekeleza, Msukumo wa Kulitekeleza, Akili ya Kulitekeleza, Mafunuo ya Kulitekeleza, Faida za Kulitekeleza, Watu wa Kukusaidia kulitekeleza, Kibali cha Kulitekeleza... n.k n.k. Hali hii hujitokeza kwa jambo lolote katika maisha pale wakati wake unapofika - liwe ni wazo la kusoma, biashara, huduma, kuoa/kuolewa n.k.
Ni Sawa sawa na Mwanamke Mjamzito unapofika wakati wa kujifungua haijalishi alikuwa anaenda salon, ama anaenda Kanisani Wakati Wa Kujifungua ukifika kuanzia akili na kila kiungo kinataarifa kuwa wakati wa ku-deliver umefika hata angekuwa anapenda chips mayai saa hizo hazina tena nafasi sababu wakati wa jambo kutokea umefika katika maisha.
Kwa Nini Watu Huzikosa Hizo Nyakati/Fursa?
Kama nilivoeleza hapo juu, watu wengi huwa wanapoona wakati huo umefika, huanguka katika mtego wa kudhani ni kawaida kwa huo wakati kufika, hivyo huo wakati hautaondoka mpaka WAO watakapofanya jambo husika.! Watu wengi huwa hawaelewi kwamba wakati wa kila jambo hupita ili kupisha wakati wa Jambo jingine! Linalowezekana leo, sio sahihi kudhani kwamba litawezekana HATA KESHO, Kesho inaweza kuwa ni wakati wa Jambo lingine! Kwa watu wengi, pale wakati unapofika, huwa hawapendi kufanya haraka kulifanya jambo husika kwa sababu, wengi, huwa wanapenda kwanza KUU-ENJOY huo wakati ambao wanakuwa wanayaona mafanikio yao waziwazi vichwani na ndotoni mwao, hivyo hawaoni sababu ya kufanya haraka KUFANYA KWELI....
Ngoja-ngoja yao huendelea mpaka wakati wa jambo unapopita, huku wao wakiamini kwamba wakati huo hautaondoka KWA SABABU HAWAJAFANYA - KOSA!!!! Wakati huwa haumsubiri Mtu, Mtu anapaswa kwenda na Nyakati!
Ni kitu cha hatari kudhani kwamba kwa sababu leo unajisikia nguvu, msukumo, hamasa na una fursa ya kufanya jambo, ukadhani kwamba hali hiyo itaendelea siku zote - la, Hasha! "Kesho" unaweza ukaamka na ukashangaa ile nguvu, msukumo na hamasa uliyokuwa nayo jana imepotea ndani mwako, zaidi tu kwamba umebakia na kumbukumbu ya picha nzuri ya vile ambavyo hali ingekuwa iwapo ungelikuwa umechukua hatua na kufanya jamvo husika!
Nini Huwa Kinatokea Pale "Wakati Wako" wa Kufanya Jambo Unapokupita!
Kwa kawaida, mtu anapopitwa na wakati wake wa kufanya jambo hubaki na picha nzuri na "ladha" ya lile jambo ambayo aliipata wakati lilipomjia au wakati wake ulipokuwa umefika. Mtu hubaki akijifariji - nitafanya tu, nitafanya tu, kwa maana tayari nilishapata picha na mpango wa namna ya kufanya!!! Ndio maana kuna tahadhari kubwa sana ya Wadada ama Wakaka ambao wakati wa Kuoa ama kuolewa Ulipofika wakadhani bado wanamuda basi ule msukumo nao ukaisha ndio maana unaweza kuta mtu anabaki kusema tu enzi zangu ilikuwa a,b,c enzi zetu a,b,c ndio maana unakuta mtu ana kazi nzuri, ana mshahara mzuri ana maisha mazuri unashangaa kwanini huyu mtu hatafuti mwenza, kumbe ule msukumo wa kufanya ulishapita. Huwezi kuwa kijana siku zote wazazi wetu wengi wamebaki na story tu enzi zetu bana, enzi zetu bana basi na huo wakati nasi utatukuta ambapo watoto wetu watashangaa kwanini hatukununua viwanja kwa ajili ya miaka 10 ama 20 ijayo, watasema baba au mama ulikuwa wapi wakati wenzako wananunua??kila siku tunasema tutafanya kesho ama mwezi ujao mwisho wa siku hatufanyi. Lakini anapokuja kutaka kujaribu, hushangaa jinsi ambavyo jambo lile lile ambalo juzi alikuwa analiona rahisi sana, leo linaweza kuwa gumu mno, zito mno, lenye kukatisha tamaa na kuanza hata kushawishika kwamba yawezekana yale matokeo mazuri na faida aliyokuwa anaidhania juzi labda haikuwa sahihi au haikuwa kweli! Mtu huanza kujifariji "Labda zilikuwa ndoto tu za mchana" au kama sungura "Sizitaki Mbichi hizi" wakati akiwa anakata tamaa na hata kuamua kuliacha lile jambo kabisa!
Kama ni Biashara, mtu hushangaa vile inavyoweza kuwa ngumu, wakati mwingine akijihisi kwamba hana mawazo mazuri au uwezo wa kuifanya, japo ni majuzi tu alikuwa anaiona kwamba ndiyo inaweza "kumtoa" kimaisha! Kama ni Kuoa/Kuolewa, mtu huweza kushangaa ghafla akaanza kuona kama vile Hakuna Mtu Anayefaa Kumuoa, kama Vile yeye hajakakaa kikuoa-oa vile (au ki-kuolewa-olewa vile); Anazidi kuona kama vile Hakuna watu wenye Sifa za Kuwaoa au wa Kumuoa yeye n.k. Kumbe???/ Kwenye Biblia tunasoma habari ya Mtu mwenye Kupooza ambaye alikaa kwenye birika miaka na miaka na Kila Mara Malaika alikuwa anakuja kutibua maji ndani ya kisima hicho anayekuwa wa kwanza kuingia yeye anakuwa mzima. Swali la Kujiuliza huyu kilema aliyekaa zaidi ya miaka 30 pale pembeni ya birika kweli kabisa alikuwa serious kupona??au alikuwa ana enjoy kuwepo pale, sababu hata Yesu alipomuuliza Wataka kuwa mzima akaanza story nyingi kuwa hakuna wa kumsogeza hakuna wa Kumsaidia. Mara nyingi sana tumekuwa tukilaumu wengine ndio wametusababishia hali tuliyonayo kumbe wakati ulipokuwa umefika hatukuwa tayari kwenda na wakati huo. Kwenye Kiingereza wanasema Golden Chance Never Come Twice. Nilisema wiki iliyopita miaka 10-15 ijayo utakuwa ukijilaumu kwa mambo ambayo ulitakiwa uyafanye leo ukadhani bado una muda. Uzee hauna taarifa, utu uzima hauna hodi ikilala ukiamka utu uzima huu hapa. Wazazi wanakaa na watoto wao kila siku ghafla wanashangaa watoto wamesha balehe ama vunja ungo still wao hata kiwanja hawajanunua. Wiki iliyopita niliandika "Kama wengine Wanaweza Kwanini Wewe Usiweze" kuna watu ambao session hii kwa maana ya majira haya wanajisikia kabisa kufanya jambo fulani la kimaendeleo lakini wamejawa na woga wa kuamua. Hata siku moja Woga hawezi kukupa maendeleo kwenye maisha. Mara 2 kwenye maisha yangu baada ya kumaliza shahada yangu ya Kwanza nilijiunga na Masomo ya Masters ajabu nikakosa amani kabisa ya ndani ya kusoma nika Postpone mwaka ukaja Mwaka uliofuata Siku soma tena baada ya kuingia class siku ya kwanza. Kila mwanadamu ana "inner voice". Sema kwa kuto kujua utasikia tunasema, Unajua nilisikia kakiktu ndani ama machale yalinicheza, ndio maana asilimia kubwa ya watu waliowahi kutapeliwa ukiwauliza mpaka unatapeliwa ulikuwa hujui??atakuambia kuna kitu nilihisi nikapuuzia. Kuwa makini sana na nyakati tulizonazo maana kila Jambo Lina Majira yake na Kila Majira yana Mambo yake.
MALAIKA AKITIBUA MAJI, USIENDELEE KUJIULIZA NINI CHA KUFANYA, ZAMA UPONE, IKIKUPITA MWAKA HUU, UNAWEZA KUSUBIRI HATA MIAKA 40...!!!
Think Differently and Make a difference.
Papaa
0713 494110
samuel_sasali@yahoo.com
Facebook. Samuel Sasali
Tweeter: Samsasali
Sype: Sasalijr.
Hivi Majuzi rafiki yangu Mussa akiwa Ofisini pale MANCON na Mkurugenzi Prosper Mwakitalima, wakiwa wanazungumza mambo mbali mbali ya maisha ikafika time ya kuongelea suala moja linahusiana na Kuoa. Prosper aligusia huo msemo, na kueleza kwamba hata kuoa huwa kuna wakati wake, na mtu asipooa wakati wake wa kuoa unapofika, inaweza ikamsumbua kuja kuoa baadaye - hata kama atakuwa anataka!
Juu ya Msemo huo ninajenga Papaa On Tuesday ya leo!
Ni kweli kabisa kwamba kila jambo lina wakati wake, NA KILA WAKATI KATIKA MAISHA UNA JAMBO LAKE! Tangu utoto hadi uzee. Ni muhimu sana kuelewa jambo la kila Wakati (na sio tu wakati wa kila jambo)!
Kuna namna nyingi sana za kutambua wakati wa jambo unapofika, na mara nyingi, watu wengi, huwa tunakuwa na bahati ya kufahamu kwamba wakati wa jambo fulani maishani mwangu umewadia, au basi, huwa tunaweza kufahamu kwamba Jambo la Wakati Huu ni hili! Kwa bahati mbaya sana, watu wengi huwa tunaona kama vile linalowezekana leo hata kesho litawezekana - KOSA!
Wakati wa jambo unapowadia, huambatana na mambo mengi ikiwa ni pamoja na Nguvu ya Kulitekeleza, Hamu ya Kulitekeleza, Msukumo wa Kulitekeleza, Akili ya Kulitekeleza, Mafunuo ya Kulitekeleza, Faida za Kulitekeleza, Watu wa Kukusaidia kulitekeleza, Kibali cha Kulitekeleza... n.k n.k. Hali hii hujitokeza kwa jambo lolote katika maisha pale wakati wake unapofika - liwe ni wazo la kusoma, biashara, huduma, kuoa/kuolewa n.k.
Ni Sawa sawa na Mwanamke Mjamzito unapofika wakati wa kujifungua haijalishi alikuwa anaenda salon, ama anaenda Kanisani Wakati Wa Kujifungua ukifika kuanzia akili na kila kiungo kinataarifa kuwa wakati wa ku-deliver umefika hata angekuwa anapenda chips mayai saa hizo hazina tena nafasi sababu wakati wa jambo kutokea umefika katika maisha.
Kwa Nini Watu Huzikosa Hizo Nyakati/Fursa?
Kama nilivoeleza hapo juu, watu wengi huwa wanapoona wakati huo umefika, huanguka katika mtego wa kudhani ni kawaida kwa huo wakati kufika, hivyo huo wakati hautaondoka mpaka WAO watakapofanya jambo husika.! Watu wengi huwa hawaelewi kwamba wakati wa kila jambo hupita ili kupisha wakati wa Jambo jingine! Linalowezekana leo, sio sahihi kudhani kwamba litawezekana HATA KESHO, Kesho inaweza kuwa ni wakati wa Jambo lingine! Kwa watu wengi, pale wakati unapofika, huwa hawapendi kufanya haraka kulifanya jambo husika kwa sababu, wengi, huwa wanapenda kwanza KUU-ENJOY huo wakati ambao wanakuwa wanayaona mafanikio yao waziwazi vichwani na ndotoni mwao, hivyo hawaoni sababu ya kufanya haraka KUFANYA KWELI....
Ngoja-ngoja yao huendelea mpaka wakati wa jambo unapopita, huku wao wakiamini kwamba wakati huo hautaondoka KWA SABABU HAWAJAFANYA - KOSA!!!! Wakati huwa haumsubiri Mtu, Mtu anapaswa kwenda na Nyakati!
Ni kitu cha hatari kudhani kwamba kwa sababu leo unajisikia nguvu, msukumo, hamasa na una fursa ya kufanya jambo, ukadhani kwamba hali hiyo itaendelea siku zote - la, Hasha! "Kesho" unaweza ukaamka na ukashangaa ile nguvu, msukumo na hamasa uliyokuwa nayo jana imepotea ndani mwako, zaidi tu kwamba umebakia na kumbukumbu ya picha nzuri ya vile ambavyo hali ingekuwa iwapo ungelikuwa umechukua hatua na kufanya jamvo husika!
Nini Huwa Kinatokea Pale "Wakati Wako" wa Kufanya Jambo Unapokupita!
Kwa kawaida, mtu anapopitwa na wakati wake wa kufanya jambo hubaki na picha nzuri na "ladha" ya lile jambo ambayo aliipata wakati lilipomjia au wakati wake ulipokuwa umefika. Mtu hubaki akijifariji - nitafanya tu, nitafanya tu, kwa maana tayari nilishapata picha na mpango wa namna ya kufanya!!! Ndio maana kuna tahadhari kubwa sana ya Wadada ama Wakaka ambao wakati wa Kuoa ama kuolewa Ulipofika wakadhani bado wanamuda basi ule msukumo nao ukaisha ndio maana unaweza kuta mtu anabaki kusema tu enzi zangu ilikuwa a,b,c enzi zetu a,b,c ndio maana unakuta mtu ana kazi nzuri, ana mshahara mzuri ana maisha mazuri unashangaa kwanini huyu mtu hatafuti mwenza, kumbe ule msukumo wa kufanya ulishapita. Huwezi kuwa kijana siku zote wazazi wetu wengi wamebaki na story tu enzi zetu bana, enzi zetu bana basi na huo wakati nasi utatukuta ambapo watoto wetu watashangaa kwanini hatukununua viwanja kwa ajili ya miaka 10 ama 20 ijayo, watasema baba au mama ulikuwa wapi wakati wenzako wananunua??kila siku tunasema tutafanya kesho ama mwezi ujao mwisho wa siku hatufanyi. Lakini anapokuja kutaka kujaribu, hushangaa jinsi ambavyo jambo lile lile ambalo juzi alikuwa analiona rahisi sana, leo linaweza kuwa gumu mno, zito mno, lenye kukatisha tamaa na kuanza hata kushawishika kwamba yawezekana yale matokeo mazuri na faida aliyokuwa anaidhania juzi labda haikuwa sahihi au haikuwa kweli! Mtu huanza kujifariji "Labda zilikuwa ndoto tu za mchana" au kama sungura "Sizitaki Mbichi hizi" wakati akiwa anakata tamaa na hata kuamua kuliacha lile jambo kabisa!
Kama ni Biashara, mtu hushangaa vile inavyoweza kuwa ngumu, wakati mwingine akijihisi kwamba hana mawazo mazuri au uwezo wa kuifanya, japo ni majuzi tu alikuwa anaiona kwamba ndiyo inaweza "kumtoa" kimaisha! Kama ni Kuoa/Kuolewa, mtu huweza kushangaa ghafla akaanza kuona kama vile Hakuna Mtu Anayefaa Kumuoa, kama Vile yeye hajakakaa kikuoa-oa vile (au ki-kuolewa-olewa vile); Anazidi kuona kama vile Hakuna watu wenye Sifa za Kuwaoa au wa Kumuoa yeye n.k. Kumbe???/ Kwenye Biblia tunasoma habari ya Mtu mwenye Kupooza ambaye alikaa kwenye birika miaka na miaka na Kila Mara Malaika alikuwa anakuja kutibua maji ndani ya kisima hicho anayekuwa wa kwanza kuingia yeye anakuwa mzima. Swali la Kujiuliza huyu kilema aliyekaa zaidi ya miaka 30 pale pembeni ya birika kweli kabisa alikuwa serious kupona??au alikuwa ana enjoy kuwepo pale, sababu hata Yesu alipomuuliza Wataka kuwa mzima akaanza story nyingi kuwa hakuna wa kumsogeza hakuna wa Kumsaidia. Mara nyingi sana tumekuwa tukilaumu wengine ndio wametusababishia hali tuliyonayo kumbe wakati ulipokuwa umefika hatukuwa tayari kwenda na wakati huo. Kwenye Kiingereza wanasema Golden Chance Never Come Twice. Nilisema wiki iliyopita miaka 10-15 ijayo utakuwa ukijilaumu kwa mambo ambayo ulitakiwa uyafanye leo ukadhani bado una muda. Uzee hauna taarifa, utu uzima hauna hodi ikilala ukiamka utu uzima huu hapa. Wazazi wanakaa na watoto wao kila siku ghafla wanashangaa watoto wamesha balehe ama vunja ungo still wao hata kiwanja hawajanunua. Wiki iliyopita niliandika "Kama wengine Wanaweza Kwanini Wewe Usiweze" kuna watu ambao session hii kwa maana ya majira haya wanajisikia kabisa kufanya jambo fulani la kimaendeleo lakini wamejawa na woga wa kuamua. Hata siku moja Woga hawezi kukupa maendeleo kwenye maisha. Mara 2 kwenye maisha yangu baada ya kumaliza shahada yangu ya Kwanza nilijiunga na Masomo ya Masters ajabu nikakosa amani kabisa ya ndani ya kusoma nika Postpone mwaka ukaja Mwaka uliofuata Siku soma tena baada ya kuingia class siku ya kwanza. Kila mwanadamu ana "inner voice". Sema kwa kuto kujua utasikia tunasema, Unajua nilisikia kakiktu ndani ama machale yalinicheza, ndio maana asilimia kubwa ya watu waliowahi kutapeliwa ukiwauliza mpaka unatapeliwa ulikuwa hujui??atakuambia kuna kitu nilihisi nikapuuzia. Kuwa makini sana na nyakati tulizonazo maana kila Jambo Lina Majira yake na Kila Majira yana Mambo yake.
MALAIKA AKITIBUA MAJI, USIENDELEE KUJIULIZA NINI CHA KUFANYA, ZAMA UPONE, IKIKUPITA MWAKA HUU, UNAWEZA KUSUBIRI HATA MIAKA 40...!!!
Think Differently and Make a difference.
Papaa
0713 494110
samuel_sasali@yahoo.com
Facebook. Samuel Sasali
Tweeter: Samsasali
Sype: Sasalijr.
Subscribe to:
Posts (Atom)